ZZK,
Ukiwa tukiwa wakweli na ukiwa mkweli, hakuna uhusiano wa moja kwa moja kati ya mengi uliyoandika na maendeleo. Rwanda wanapiga hatua ya maendeleo kuliko sisi na uhuru walio nao kujieleza umebinywa sana, yet ukipima maendeleo kiuchumi wanafanya vizuri sana kuliko sisi. Uhuru tulio nao ni mkubwa mnoo. Hiyo hofu sijui iko wapi maana wanaokosoa watawala ni wengi na wapo.
Dr.Kitima wa TEC alikosoa kwa uwazi pale UDSM kwenye kongamano la miaka 3 ya JPM, kuwa uwekezaji wa miradi ambayo haikisi uwezo wa Watanzania kumudu bidhaa na huduma toka viwandani kuna haja ukangaliwa kwa jicho la pili na yupo.
Humu JF mara kibao tunakosoa mambo ambayo tunadhani hayaendi sawa na tuko tunaishi bila hofu yoyote.
Mimi ntakuelewa sana kama ukija na hoja ambayo itaongeza ajira kwa vijana na kwa kuwa serikali ilikuwa na uwezo wa kuzinunua korosho zote in 2days kama waunuzi wangegoma kununua kwa 3,000; basi kumbe tuihimize serikali kutumia fedha hizo kuwakopesha Watanzania kuja na miradi (Project Financing) ya kuongeza thamani ya mazao ya kilimo ikiwemo Pamba, Kahawa, Korosho na kuuza zikiwa zimeongezewa thamani, athari yake kiuchumi itazalisha ajira zaidi, atarejesha ndani fedha za kigeni nyingi zaidi kuliko mauzo ya korosho ghafi au pamba ghafi. Matokeo yake fedha zingerejeshwa na tax base ingepanuka.
Binafsi nakuona umekuwa too much subjective kuliko kuwa objective kwa kutoa mifano relevant na mifano mbadala kuliko kuwa na hisia hasi.
Tanzania iko salama na hofu unayoisema kuna wengine hatuioni