Katika mijadala ya asubuhi ya kituo cha televisheni cha STARTV Jumapili iliyopita, wageni waalikwa katika mjadala ule walimulalamikia Mh.Zitto kwa kukurupusha hoja ambazo anashindwa kuzisimamia.Kudhibitisha hili ni kuwa katika bunge lililopita alisema atawataja walioficha pesa uswizi kama serikali haitawataja lakini wiki mbili zilizopita Mh. Zitto amesikika kupitia StarTv hiyohiyo kuwa hatawataja.
Hatujakaa sawa anaibuka na habari za kuwalaumu wazungu kwa wizi. Njia bora ilikuwa Mh. Zitto anahakikisha tunajisafisha sisi kwanza kwa kuwashughulikia wezi tunaowajua na kuziba mianya ya wizi kama Mh.Zitto alivyokuwa amenuia huko Bungeni ndipo sote kwa pamoja tuwageukie wazungu wezi.
Kitendo hiki cha Mh.Zitto kuwarukia wazungu wakati hili la kuwashughulikia wezi wa ndani kinatoa tafsiri mbaya sana juu yake juu nia aliyokuwa nayo kuhusu tuhuma alizozitoa bungeni za pesa za wizi zilizofichwa Uswisi, binafsi naona Zitto anataka kutumia mwanya huu wa kuwashambuliwa wazungu kufifisha suala zima alililojiapiza kushiriki kulikabili yaani suala la watanzania kuficha pesa za wizi Uswisi na kwingineko.
Zitto kuruka ruka na hoja ambazo azisimamii bado anazidi kudororesha imani ya raia wa Tanzania kuwaamini vijana katika shughuli za kuikwamua nchi yetu kutoka kwenye lindi la matatizo mengi ya kijamii, kiuchumi, kisiasa na kadhalika.
Kwa mara nyingine namtahadharisha Zitto aache mtindo wake huu wa kudidimiza nia ya watanzania ya kuwaamini vijana kuwa na uwezo wa kukwamua nchi yao kwani yeye bado anabeba taswira ya Mwanasiasa Kijana. kama hawezi kujirekebisha basi ajiuzulu masuala yote ya Siasa na aendelea na shughuli zake nyingine.
---MpigaKelele