Zitto Kabwe awalipua wazungu!

Zitto Kabwe awalipua wazungu!

Just thinking aloud!!

Hivi kama baba mwenye nyumba akialika wageni (bila kujali rangi au asili yao) waje nyumbani kwake kisha akawaruhusu waingie ndani ya nyumba yake na wawe huru kuchukua au kufanya kitu chochote watakachoona kina manufaa kwao ni halafu wale wageni wakaiba pesa na kubaka watoto ni nani wa kulaumiwa? Ni baba mwenye nyumba au ni wale wageni aliowaalika na kuwapa ruksa ya kuingia popote wanapotaka na kufanya chochote wanachoona kinafaa?

Hivi baba au mama mwenye nyumba akichukua raslimali ya nyumbani kwake akaipeleka nje (iwe kwa nyumba ndogo, kidumu au popote anapojua yeye) na kuiacha familia yake ikiwa maskini haina msaada ni nani wa kulaumiwa? Ni mwenye nyumba au wale wanaopelekewa mali ili watumie na zinazobaki waendeleze majumbani kwao?

Nadhani imefika wakati waafrika tukaacha kutafuta mchawi nje ya nchi na kuelewa ule msemo wa wahenga kuwa kikulacho ki nguoni mwako.

Kila dola inayoondolewa afrika ama ina baraka ya waafrika walioteuliwa kuwawakilisha wenzao kusimamia raslimali za nchi zao au inatoroshwa na hawa wawakilishi wenyewe na kupelekwa kwa wazungu, waarabu, wachina, etc. Tuache kupoteza muda wetu kutafuta wachawi ulaya, amerika na bara hindi wachawi wetu wapo humu humu nchini.
.
Eti hawa ndio viongozi tunaowategemea,wasomi wanaonyumbulisha na uelewa mkubwa.Ni ujinga mkubwa, Hivi leo hii Buzwagi,na Barick wanaovuna maelfu ya ton ya dhahabu kanda ya Ziwa wamelazimisha serikali ya Tanzania kulipa mrahaba wa 3%,na exemptions kibao?,how about Tanzanite One?,how about hoteliers?, ambao hata wapishi na wazibua vyupa wanaletwa toka philipines na China>,Ni sera zetu eti za Uwekezaji,huku misamaha ya kodi kibao,na tuna tegemea misaada kwa 42% ya bajeti na 80% ya bajeti ya maendeleo.75% ya development bajeti ni capacity building kulipana posho na kununua mashangingi ,V8 na Nissani ni ujinga Kabisa.Wazungu ndio wanatakiwa watushangae sisi kwa ujinga wetu.Tazama fedha za change ya Rada kama siyo wazungu wenyewe TZS 74bilion zingepotea tu.
Nchi ya Swiss yenyewe imeandaa sera ya namna hiyo ya kuvutia wawekazaji katika sekta ya fedha na ni kitu cha hospitality,honesty,secrecy, kama Tanzania nayo inaweza kufikia hatua ya namna hiyo ya kuaminiwa na nchi na watu duniani ni jambo jema.Otherwise MATATIZO MENGI YA AFRIKA/TANZANIA SULUHISHO NI WATANZANIA WENYEWE NA HAKUNA MCHAWI WA MATATIZO YA WAAFRIKA/WATZ.ALUTA CONTINUA, ALUTA CATABUU
 
Watanzania tuwe wazuri wa kumpa mtu sifa yake kama tulivyowazuri wa kubeza.Alichokifanya Zitto Kabwe ni udhubutu ambao wengine tumeshindwa.Jamani Mnyonge ,Mnyongeni lakini haki yake mpeni! Hongera Zitto Kabwe!
 
Namsubiri Kiongozi wa Kwanza mwenye akili. Atakayehamasisha Watanzania wachange tusenti twao (wa alfu moja, mbili, tano, kumi, n.k) kuwa mtaji wa uwekazaji katika nyanja watakaichagua kuliko huu upumbafu wa kuandika kwenye karatasi/mitandao, kusoma kwenye Podium/iPad, kuwaponda wazungu majukwaani alafu ukishuka unakwenda kuwaomba misaada!

Tuliwahi kuchangishwa tukaanzisha NICO. Vihela vyetu vikaishiwa kuliwa na akina Mosha yule CTI & Co.
 
Tuliwahi kuchangishwa tukaanzisha NICO. Vihela vyetu vikaishiwa kuliwa na akina Mosha yule CTI & Co.

Kukosea ndiyo kujifunza. Kibaya ni kushindwa kujua ulianguka wapi na kujifunza usianguke tena. Ingekuwa kila likifanyika kosa, dawa ni kuacha kabisa jambo, basi Edson asinggundua balbu na leo tusingekuwa na taa za umeme....Alikosea zaidi ya mara 1000 lakini alipoulizwa alijibu "Nimejifunza sababu 1000 kwa nini sijafanikiwa"
 
Robbing Africa - How! The real meaning of this word is a crime. And starting
among us, plans and collaborate with the people which we are saying are
robbing us. The proceed of bribery and theft by the Government officials,
and smuggling our country money a cross-border, that's Illicit financial flow
is a hidden resource for our development. You can say this is a main point
of our poverty in Tanzania and all Africa.
 
watanzania tuwe wazuri wa kumpa mtu sifa yake kama tulivyowazuri wa kubeza.alichokifanya zitto kabwe ni udhubutu ambao wengine tumeshindwa.jamani mnyonge ,mnyongeni lakini haki yake mpeni! Hongera zitto kabwe!

word...zitto for president
 
Uporaji? We Zitto acha unafiki! Ni nani mporaji kati ya viongozi wetu na wazungu? Mfano rafiki yako Idrisa alipopora fedha za rada mbona hukupiga kelele! Na huyo katibu wa chama chako cha magamba kinachokupa kichwa anapopora meno ya tembo mbona hupigi kelele? Na mtoto wa huyo rais wako anayekupa kichwa anapopora mbona hupigi kelele. By the way kwani wazungu hutushikia bunduki? Mikataba kama ile ya madini si nyie mliipitia?
MHIMBIMBILI nieneo baya sana na zuri sana,Kunawakati utakutana na watu wanalia sana,Kunawakati utakutana na nyuso za furaha.
Sasa hapa tumekutana na uso wenye majonzi,kweiki na mapovu ...Taratibu haya ni maisha tu hata ungesema Nchi nzima ni marafiki wa Zitto au kaka yake Zitto au Ni ndugu zake zitto kamwe hautaongeza vichwa viwili mwilini mwako.Utabakiwa na hicho tu kilichojaa kamasi
 
If therein is anything to salute ZZK, you will then need to salute many ****** in town.

U a mong them!!!Inakuuma sana Kamanda kuona Unaitwa Mgambo..Zitto anaitawa FBI.
Jitahidi sana labda ipo siku nawewe huyo babu ataipigiwa salute
 
zitto amekuwa jasiri kuwaeleza wazungu maovu na hila wanazotumia kuzipata raslimali za africa. Ni viongozi wangapi wenye ujasiri wa kufanya hivyo? Wengi wa viongozi wetu wamebaki ni vibaraka wa wazungu na husifia hata vile visivyikuwepo, na kusisitiza ushirikiano usio na tija, ushirikiano wakinyonyaji! Ushirikiano wa bwana na mtwana nuawezekana? Hongera zitto!
zitto ni mzalendo,mtiifu,mwelewwa,msomi,jasiri n.k kawa taifa hili anazungumza mambo kitaifa na si kwa misingi ya uchadema na ccm.
Zitto kabwe my next president 2015
 
katika mijadala ya asubuhi ya kituo cha televisheni cha startv jumapili iliyopita, wageni waalikwa katika mjadala ule walimulalamikia mh.zitto kwa kukurupusha hoja ambazo anashindwa kuzisimamia.kudhibitisha hili ni kuwa katika bunge lililopita alisema atawataja walioficha pesa uswizi kama serikali haitawataja lakini wiki mbili zilizopita mh. Zitto amesikika kupitia startv hiyohiyo kuwa hatawataja.

Hatujakaa sawa anaibuka na habari za kuwalaumu wazungu kwa wizi. Njia bora ilikuwa mh. Zitto anahakikisha tunajisafisha sisi kwanza kwa kuwashughulikia wezi tunaowajua na kuziba mianya ya wizi kama mh.zitto alivyokuwa amenuia huko bungeni ndipo sote kwa pamoja tuwageukie wazungu wezi.

Kitendo hiki cha mh.zitto kuwarukia wazungu wakati hili la kuwashughulikia wezi wa ndani kinatoa tafsiri mbaya sana juu yake juu nia aliyokuwa nayo kuhusu tuhuma alizozitoa bungeni za pesa za wizi zilizofichwa uswisi, binafsi naona zitto anataka kutumia mwanya huu wa kuwashambuliwa wazungu kufifisha suala zima alililojiapiza kushiriki kulikabili yaani suala la watanzania kuficha pesa za wizi uswisi na kwingineko.

Zitto kuruka ruka na hoja ambazo azisimamii bado anazidi kudororesha imani ya raia wa tanzania kuwaamini vijana katika shughuli za kuikwamua nchi yetu kutoka kwenye lindi la matatizo mengi ya kijamii, kiuchumi, kisiasa na kadhalika.

Kwa mara nyingine namtahadharisha zitto aache mtindo wake huu wa kudidimiza nia ya watanzania ya kuwaamini vijana kuwa na uwezo wa kukwamua nchi yao kwani yeye bado anabeba taswira ya mwanasiasa kijana. Kama hawezi kujirekebisha basi ajiuzulu masuala yote ya siasa na aendelea na shughuli zake nyingine.



---mpigakelele

ungekuwa mwanachama wa chadema ningekupa kazi ya kusafisha washroom ya katibu mkuu kila siku.
Kwa sbabu ni mwana ccm ambaye akili zako na upembuzi wa mambo umejikita kwenye hasira dhidi ya viongozi wa chadema hasa wale wanaotetea haki za watanzania nakupandisha cheo kuanzia leo wewe ni houseboy wa kudumu wa nape nauye

zitto sio level yako,zitto hajawahi shindwa jambo.zitto anafocus mbali kwa manufaa ya taifa
 
Tukija kuzinduka ktk madini yatakua yamebaki mashimo tuu,,,inasikitisha sana ukipita pale Tanzanite One unawaona mama wa Kimasai na watoto wao wakipita na Punda kwenda kutafuta maji,,,nn maana ya mwekezaji?Mzungu hawezi kukupenda hata siku moja amesha2pa UHURU wa miaka 51 ya BENDERA na wanaonufaika na Tanzanite One ndo huyo m1 wapo ni mtoto wa Kigogo mzito kabisa!

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
ungekuwa mwanachama wa chadema ningekupa kazi ya kusafisha washroom ya katibu mkuu kila siku.
Kwa sbabu ni mwana ccm ambaye akili zako na upembuzi wa mambo umejikita kwenye hasira dhidi ya viongozi wa chadema hasa wale wanaotetea haki za watanzania nakupandisha cheo kuanzia leo wewe ni houseboy wa kudumu wa nape nauye

zitto sio level yako,zitto hajawahi shindwa jambo.zitto anafocus mbali kwa manufaa ya taifa

Hapa mbinu zako za kujibu hoja zinakushitaki kuwa wewe ni "concetrated/pure ACID" uliyekuwa re-engineered na wapinzani wa CDM na sasa unatafuta njia ya kuitoboa CDM. Bahati nzuri umeisha shutkiwa. Kila mtu anajua ni viongozi wa chama gani watumiao lugha isiyo na staha majukwaani, kwa maneno mengine ni rahisi sana kujua wewe umekuwa re-engineered na watu gani.

Nakubali kuwa Mh. Zitto siyo level yangu, kwa vyote anaweza akawa level ya juu ama akawa level ya chini yangu. Namheshimu ZZK kama mwanasiasa kijana wa taifa letu ambaye anaweza kutoa mchango muhimu kwa Tanzania. Ni kwa heshima hiyo hiyo ninakuwa ari ya kumkosoa mara anapoonekana kuishusha heshima ninayompa.
 
mganga aloiloga serikari yetu ashakufa so kupona ni ndoto!!!!!!! But t can only end once kama tutapata serikari makini yenye watu makini and not hawa Chukua Chako Mapema CCM
 
U a mong them!!!Inakuuma sana Kamanda kuona Unaitwa Mgambo..Zitto anaitawa FBI.
Jitahidi sana labda ipo siku nawewe huyo babu ataipigiwa salute

Pengine umeamka na kurukia vitu, bila hata kuelewa ukidhani unamlinda Zitto.Hapo ndipo tunapodharauliwa sana waTZ.Ujuaji umetuzidi. Stement niliyo comment haikuw ana cha tofauti au cha ajabu kwa zitto kusema kuwa kuwa "wageni waangaliwe kwa makini".Mbona kila mtu anaongea tena kwa miaka mingi kabla Zitto hajawa mwana siasa wala kuzaliwa.SIoni haja ya watu wenye fikra duni kama zako waanze tumezesha kwa nguvu kuwa ni bonge la Idea.

Kweli unachosha na ni mfano mzuri wa ujinga wa ZItto na wanaomzunguka, yupo to artificial and naive.Uzalendo hausemwi na kelele za mtu au kujipima mwenyewe.Hata zitto kujihusisha na mambo ya kizalendo hakumfanyi kuwa mzalendo.Lbda tuu kukurahisishia ni kwamba hata polisi mwizi hushawishika kushika wezi ambao hawajampa maslahi ya huo wizi.
 
Kweli maji hufuata mkondo. Zito ananikumbusha Jakaya alivyokwenda South Africa akakurupuka eti wazungu watulipe kama fidia ya biashara ya utumwa. Jamaa akawa hata hajui ni sehemu gani ya Tanzania ambako wazungu walikuja kuchukua watumwa. Alionekana kama katoka pangoni. Kwa nini hawa watu wanakosa ujasiri wa kuhoji Waarabu waliojizolea watumwa lukuki Africa na kwenda kuwaua kikatili huko kwao?

Haki huokoa Taifa. Achieni upendeleo. Mzani wa haki humpendeza Mungu. Kuwadai wazungu na kuwaacha mataifa mengine kama waarabu na mafisadi wa ndani ni dalili za chuki binafsi dhidi ya Wazungu na kutokuwa na nia ya dhati ya kukomboa taifa.

Idadi ya Watanzania wanaofikiria kwa kutumia makalio inazidi kuongezeka, hivi wee Tabby ndo fahamu zako zinakutosha kweli, inavyoonyesha hujawahi kutoa presentation yoyote katika maisha yako, itawezekanaje Zito afanye presentation kwa wazungu then azungumzie waarabu, likely, angelikuwa kule kwa wale walioiba Twiga asingelizungumzia wazungu angeliwapasha hao waarabu-ndo technic za presentation wakati mwingine huwa unaangalia hadhira husika na ujumbe unaotaka kuutoa. Sasa kwa akili zako si angeonekana chizi iwapo angeliwahutubia wazungu then message ingewahusu waarabu.

Zito hajazungumzia tu utoroshaji wa fedha peke yake unaofanywa na waafrika wenyewe, ameenda mbali mno kwa kuzungumzia utoroshwaji wa fedha ambao unafanywa na "whites" kupitia MNCs kwa njia mbalimbli kama vile round tripping, transfer pricing and thin capitalization ambazo kwa pamoja zinaleta umaskini mkubwa sana kwa mataifa yanayoendelea hususan resource rich countries{Hizi hata ****** wenu hazijui zinzvyofanyika}.Msijizoeshe kuandika ujinga tu humu humu jamvini ikiwa kitu hamuwezi kukichambua na kukielewa mkae kimya, mnakera wengine kwa sababu hicho alichosema Zito ndiyo "African Debate" kwa sasa. Wanaleta misaada ya uongo, yenye condition nyingi tu kama za ushoga, kwenda uchi, uzalilishaji nk, wakati in broad perspective wanachochukua ni zaidi ya wanachokileta. Kwa mwaka huu pekee, binafsi nimehudhuria mikutano mingi ya namna ya zito iliyofanyika nchi tofauti ikiwemo mmoja uliwahi kufanyika hapa Doha, na kila mwafrika apatapo nafasi hoja ni hiyo so whites wenyewe wanaumiza vichwa kwamba "waafrika wamegundua janja ya wazungu" ndo maana ikitokea presentation ya namna hiyo wanachanganyikiwa sana. Wewe na Tukutuku muwe watu wa Dunia zaidi na mpanuke akili achaneni na shallow thinking. Hakuna cha mzungu, mwarabu wala mwafrika, yeyote anayeiba rasilimali za waafrika hali ya kuwa watoto na wamama kule vijijini na mjini wanaishi maisha ya "wanyama" katika karne hii hawatufai. Lets join this move, a day will come we shall make it.
 
Zinadine, na wenzako wote wenye tabia za kijinga kijinga za kudhani kwamba matusi ndiyo ujenzi wa hoja. Elewa kwamba huwezi kusuppress Ideas za watu wengine ama kuinfluence kwa matusi. Wewe ndiiye mjinga unayedhani kwamba unajua kila kitu na kuamini approach zako za ku tackle ubaidhirifu na wizi ndizo sahihi. Hakuna mtu atakaye kujoin hand kwa communications za matusi.

Najua una affiliations na waarabu ndiyo maana matusi kwako ni asili na hiyo tabia ya kuwakumbatia waarabu hapa haina nafasi. Wewe sema unachoona ni sahihi na mimi nitasema the way I see ni sahihi. Huna authority ya kuniamrisha kwa matusi eti nisiwaseme waarabu na jinsi wanavyokumbatiwa. Nitasema waarabu they are a big problem kwa maendeleo ya dunia ukubali ukatae. Matusi yako hayalazimishi nikuunge mkono katika ubaguzi wako na chuki zako binafsi kwa wazungu.

Matatizo yapo ndiyo lakini siyo ulazimishe tuishie kwa wazungu peke yake, na eti watu wengine wasiguswe. Tuna uhuru wa kuzungumza the way we feel kama ambavyo wewe unafeel. Tuna hiari ya kuzungumza maadui wetu wa maendeleo wakiwemo waarabu, na watanzania wenyewe namna wanavyoshiriki ama kufacilitate uharamia wa maendeleo yetu. Tuna uhuru wa kujadili entrace ambayo tunadhani zinaweza kufanya kazi katika hilil vile tunavyotaka. Na wala si wewe wala mtu yeyote atasema eti miungu waarabu wasiguswe wakati ndio tatizo kubwa sana na maisha ya binadamu.

Matusi yako na waarabu wenzio na watu wa aina yako yanawatosha ninyi huko huko. Na wala si njia sahihi ya kuimarisha hoja, kunyamazisha watu ama kuinfluence forum. Please behave. Tumechoshwa na tabia zenu waarabu.
 
Hakuna haja na sababu za kujificha! anzisha wewe na sisi Great thinkers tuko tayari kujadili hoja zako lakini ziwe na source...!

Pole sana kadogoo. Hakuna haja ya kujificha vinginevyo basi hakuna haja ya kuwa katika forum na suala la source wala siyo issue ya kuleta arguments hapa.

Nilimaanisha kwamba nitaondoka katika forum kidogo na mara nikirudi, nikutaarifu ili uwe available kusoma na kuchangia katika zile threads nilizoseme nitazianzisha. Pengine utaelewa ni utawala gani kati ya Wazungu, Waarabu, na CCM ambao umedidimiza maendeleo ya nchi yetu. Unaposema wazungu walitawala kimabavu, kisa unatetea waarabu, na kusahau kabisa ugandamizaji unaofanywa na viongozi wa serikali ya ccm, na athari za tawala zingine za kigeni naona kama kuna umuhimu mkubwa wa wewe kuona zaidi ya unavyodhani unahitaji.
 
Back
Top Bottom