Zitto Kabwe ajisalimisha polisi

Zitto Kabwe ajisalimisha polisi

Katika Taarifa ya Habari ya TBC1 ya Saa kumi Jioni Kamanda wa Polisi wa Kanda maalum ya DSM amekaririwa akisisitiza kwamba Polisi bado wanamtafuta Zitto Kabwe na kwamba watahakikisha anakamatwa ikiwa hatajisalimisha kama kweli yeye ni mzalendo....
-----------------------------------------------------------

UPDATES

Mwenyekiti moja ya kamati za Chama ametuma ujumbe huu

Habari.
Nimepata simu ya Kamanda wa Polisi Wambura saa tisa na nusu. Na akaniomba nimfikie Kiongozi wa Chama na kumwambia afike kituo cha polisi cha kati.

Mimi, Kiongozi wa Chama na Mwanasheria tuko njiani kuelekea kituoni.
Kiongozi wa chama ameomba tuwe watulivu tukawasikie wanachoitaji na tutawajuza yanatoendelea.

Sasa ni wapi Zitto amejisalimisha Polisi? Au wewe ni muandishi wa Shigongo?
 
Sasa naanza kuamini kuwa hakushinda kihalali,
Kama angeshida kihalali asingehangaika hivi na wapinzaniiiiiiiiiiiiiiiiiii
Nilikuwa nawaza jambo hili sana mkuu, huenda nilitokwa povu bure kumtetea wakati ule, napata wasiwasi na ushindi wake,
Kwanini anawaogopa namna hii wakosoaji wake?
 
Bajeti inapitishwa kwa nguvu za jeshi la polisi....ina maana ccm haina imani na wabunge wake?
 
Hivi kama zitto amevunja sheria si apelekwe mahakamani? Sarakasi za nini?
 
Asichokijua Magufuli ni kwamba atapambana na wapinzani na hatashinda isipokuwa atashindwa yeye kuwatumikia wananchi kwa kuwa atapoteza muda wake mwingi kujibu shutuma toka kwa hao wapinzani. Ni kheri aachane nao.
 
Wewe unasema nini, hakuna cha moto wala nini, lazima serikali iwawadabishe mpaka mtakapojifunza kutii sheria
Badala ya kujikita katika kuweka mikakati na mipango ya utekelezaji wa ilani ya chama chake,anahangaika na wapinzani ambao hawajabeba hata rungu!2020 sijui atasingizia wapinzani ndio wamemkwamisha?!
 
Back
Top Bottom