Zitto, Habibu Mchange hana sifa za Kukunadi

Jiwe la Ukara

Member
Jul 15, 2011
44
31
Na. Martin M. Malima

Tangazo la Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Zuberi Kabwe la kugombea Urais kama atapitishwa na Chama chake cha Chadema linaripotiwa na vyombo vya habari kuzua tafrani ndani ya Chadema. Binafsi sina hakika na uwepo wa tafrani hii ndani ya Chadema kwani naamini Chadema ni zaidi ya Mzee Edwin Mtei na wanachadema wachache katika mitandao ya kijamii.

Baada ya Tangazo hili wamejitokeza marafiki wawili wa Zitto wakitetea na kuunga mkono Tangazo hilo. Hawa ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema na Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Dkt. Kitila Mkumbo na aliyekua mgombea wa ubunge wa Chadema katika uchaguzi mkuu 2010 Jimbo la Kibaha Mjini Habibu Mchange. Ingawa ninayo maoni juu ya makala ya Dkt. Kitila Mkumbo lakini katika makala haya nitajadiri makala ya Habibu mchange. Nitajikita kujadili kama Habibu Mchange anazo sifa za kisiasa za kumnadi Zitto na hoja alizotoa kumnadi.

Kuna mwanasiasa mmoja wa Chadema aliwahi kuniambia kuwa ukitaka kukosana na Habibu Mchange basi mpinge au tofautiana na Zitto. Mwanasiasa huyo aliniambia kuwa Mchange huwa yuko tayari kutofautiana na mtu yeyote ambaye aliwahi au huwa anatofautiana na kile anachokiamini hata kama suala linalojadiliwa ni kweli.

Kwa kile kinachoitwa ‘siasa za makundi’ ndani ya Chadema Mchange anajipambanua kama mfuasi mtiifu kwa Zitto. Katika siasa za majukwaani na nje ya majukwaa ufuasi wake unaonekana. Kumwamini mtu flani katika jambo lolote la kisiasa, kijamii na kiuchumi ni kawaida. Ila si kawaida kumwamini mtu kiasi cha kutokutofautiana nae au kushindwa kuona udhaifu wake. Katika harakati za kisiasa mwanisiasa anapaswa kuwa na marafiki wanaoweza kuthubutu kumwambia madhaifu yake.

Anapswa kuwa na marafiki ambao zaidi ya kumpongeza kuthubutu kutangaza nia, pia watamwambia kuwa kusema kuwa waliozaliwa kabla ya uhuru wasigombee urais ni ubaguzi wa rika. Mtu mbaguzi wa namna yeyote ile hafai kuogoza. Leo atawabagua watu kwa umri wao, kesho kwa dini, jinsia, taaluma , makabila, mikoa na wilaya zao. Sitashangaa akianza kuwabagua hata kwa vyuo walivyosoma. Maama aweza kusema wenye kufaa kuongoza ni wale waliosoma Chuo kikuu cha Mzumbe pekee, na sio Chuo Kikuu cha Zanzibar. Kama Mchange ‘ni ndio Mzee’ kwa Zitto ni wazi kuwa si mtu wa msaada sana katika harakati za kuelekea Ikulu ya Magogoni mwaka 2015.

Zitto na Machange ni wanasiasa wanaofanana katika baadhi ya mambo. Ukifuatilia kauli zao katika vyombo vya habari na mitandao ya kijamii utagundua. Hawa ni wanasiasa wanaoamini wanafahamu kuliko wengine. Wanawaona wale wasiorandana na mawazo yao kuwa hawajui. Katika mitandao ya kijamii Mchange huwaita wale anaotofautiana nao viraza. Katika makala yake amewaita“…wavivu, waoga na wafitini…”. Ni maneno makali yanayowafaa wauaji, mafisadi na walarushwa.

Katika harakati za kisiasa mwanasiasa anakutana na watu wenye lugha za kuudhi na kukatisha tamaa. Kwa bahati mbaya hakuna ‘mwongozo wa spika’ katika siasa za ushindani. Chadema kama chama kinachojiandaa kuchukua dola kimekumbana na maneno ya namna hii kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM), na hivi karibuni kutoka Chama cha Wananchi (CUF). Uvumilivu katika kutoa mawazo ni turufu katika siasa. Zitto anahitaji watetezi watakao kua tayari kukabiliana na wananchi watakao kuwa na maswali mazuri kwake na ya kuuzi.

Wapo watakoa hoji uhusiano wake na mmoja wa wakurugenzi wa Idara ya Usalama wa Tiafa, Jack Zoka, anayetuhumiwa na Chama chake kupanga mpango mchafu wa kumuua Katibu Mkuu wa Chama Dkt. Wilbroad Slaa, Mbunge wa Ubungo John Mnyika na aliyekua mbunge wa Arusha, Godbless Lema. Anachotakiwa kufanya Zitto ni kuandaa majibu ya kuridhisha na kushawishi na sio dhihaka za Mchange.

Uadilifu na uajibikaji wa Habibu Mchane

Katika kuwahikikishia watanzania kuwa anaweza kuwa Kiongozi Mkuu wa nchi, Zitto anajinasibu kuwa ni muadilifu. Sio mla rushwa. Bila shaka hana urafiki pia wanarushwa au watuhumiwa wa ufisadi. Mchange anaposimama kumnadi Zitto anapaswa afanane nae pasipo shaka.

Habibu Mchange aligombea nafasi ya Mwenyekiti wa Baraza la Vijana la Chadema (Bavicha) Taifa. Kabla ya mchakato Mchange alinza kampeni chafu za rushwa. Aliwatumia baadhi ya wajumbe pesa kinyume na taratibu za uchaguzi ndani ya Chadema.
Wajumbe wa kamati ndogo ya CC ya Chadema chini ya wanasheria nguli Mabele Marando, Prof. Abdalah Safari ilimkuta Mchange na hatia ya kutumia Sh. 2, 561,000 kama hongo kwa kuwasafirisha baadi ya wajumbe kutoka mikoani hadi Dar es Salaam na kuwaandalia malazi.

Barua ya Mwenyekiti wa Baraza la Vijana Mkoa wa Mwanza Liberatus Mlebele kwa Katibu Mkuu wa Chadema, Dkt. Wilbroud Slaa ulikua ushahidi tosha kumwengua Mchange katika uchaguzi huo. Katika barua yake Mlebele aliambatisha kiwango cha pesa, namba ya simu aliyotumia Mchange kutoa rushwa kwa wajumbe na nakala ya kitabu cha wageni cha Hitel ya Bondeni One ya Magomeni.

Mchange alikili mbele ya CC ya Chadema kwamba simu iliyotajwa na Mlebele kupeleka fedha ni yake, na kwamba alimhonga Mlebele kiasi kilichotajwa na kulipa sehemu ya gharama za hoteli, na kumuagiza akusanye wajumbe wa mkutano wa uchaguzi. Ni zaidi ya mwaka mmoja sasa Mchange hajaweza kuwashawishi wanachadema na vijana asilimia 60 wa Tanzania anaoamini watampeleka Zitto Ikulu kua ni mwadilifu. Mchange anaposimama kumnadi Zitto huku anaelea katika lindi la tuhuma za rushwa ambazo hajawi kuzikanusha ni dhihaka.

Zitto ni Naibu Katibu Mkuu wa Chadema na Mwenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma kwa vipindi viwili mfulizo mpaka sasa. Kama ishara ya ya utendaji wake mzuri mwaka 2010 aliteuliwa kuwa Naibu Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni. Anapotangaza kugombea urais anamaanisha kuwa ameshinda majukumu aliyonayo anahitaji ridhaa ya kupatiwa majukumu zaidi. Itakuwa ni turufu nzuri kwa Zitto kama watakao mnadi ni watu wenye rekodi nzuri ya utendaji kama yeye.

Sababu nyingine ilyopelekea Mchange kufutwa katika uchaguzi wa BAVICHA Taifa ni kushindwa kuwajibika katika nafasi yake kama Mwenyekiti wa BAVICHA wilaya ya Temeke. Katibu wake alimtuhumu Mchange kushindwa kutimiza wajibu kwa kutokuudhuria vikao tangu kuchaguliwa kwake. Tafsiri ya madai haya ni kwamba Mchange ni Mshindwa Kazi, anayemnadi Zitto, Mshinda Kazi. Hili ni doa katika harakati za Zitto.

Mchango wa Zitto katika kujenga Chama

Makala ya Mchange inaonesha kuwa hamfahamu vizuri Zitto. Chadema ni taasisi. Kazi za kueneza sera za chama zinafanywa na wote kama timu moja. Mafanikio ya chama hiki ni matokeo ya ushiriki wa wanachama wote wa chadema, na sio viongozi wa makao makuu pekee. Unapozungumzia mafanikio ya Chadema huwezi kumwondoa mwanachama mtiifu wa kijiji Kajiungeni, Urambo, Tabora. Hivi ndivo Zito anavyoamini pia.

Kuna tabia inazuka miongoni mwa wanachama wa Chadema ya kutambua mchango wa mtu mmoja mmoja katika mafaniko ya chama. Kuliwahi kujitokeza hoja katika chombo kimoja cha habari juu ya nani alitoa wazo la Chadema kwenda kumuona Rais Jakaya Kikwete kuhusu Sheria ya Mabadiriko ya Katiba. Mara baada ya hoja za Chadema kukubaliwa na Rais ilizuka hoja ya kibinfsi ya kwamba nani mwanzilishi wa hoja ya kwenda kumuona Rais. Wengine walisema ni Zitto Kabwe na wengine marehemu Regia Mtema. Kimsingi sikuona mantiki katika hoja hii kwa kuwa Chadema ni taasisi.

Mchange anakuja na hoja za kibinafsi na u-mimi toafuti na mtazamo wa Zitto anayemtetea. Anaamini kuwa kazi ya kujenga chama aliifanya Zitto wakati wa Oparesheni Sangara aliyoiassisi yeye (Zitto). Anakwenda mbali kwa kuwataja baadhi ya wabunge wa Chadema kama udhihirisho wa kazi nzuri ya Zitto. Anakiweka Chama na wanachadema wengine pembeni.

Ni kweli matunda ya Oporesheni Sangara yalionekana wakati wa Uchaguzi Mkuu 2010, lakini si kipimo sahihi unapowaataja wabunge kama uthibitisho pekee. Mwamko wa wananchi kupigia kura Chadema ndio matunda dhahiri. Watanzania walijitokeza kwa wingi kuipigia kura Chadema katika nafasi za udiwani, ubunge na uraisi. Isingekwa mifumo mibovu ya uchaguzi tuliyonayo, vinginevyo pengine Chadema ingekuwa inashika dora au kuwa na idadi kubwa zaidi ya wabunge na madiwani.

Mwanachama makini ni anayeheshimu na kushiriki kikamilifu kazi za kisiasa. Kazi hizi ni kueneza sera na falsafa za chama kwa wanachama wapya. Chama kinapaswa kubadirika kimkakati na mbinu katika kueneza siasa. Chama chenye kutumia mbinu zile zile za kisiasa kinakbiliwa na changamoto ya ubunifu ambayo inapelekea kifo cha kisiasa. Kampeni ya Vuguvugu la Mabadiriko (Movement for Change) au M4C ni kazi halisi ya kisiasa iliyobuniwa na Chadema. M4C ni nimwendelezo wa Oparesheni Sangara. Mwanachama wa Chadema anaposhindwa kukubali mkakati wa chama kujitanua na kuwafikia wananchi wengi zaidi anakosa nia njema kwa chama.

Mchange anajikanganya. Anaikubali Oparesheni Sangara, anakejeli M4C. Anasema kuwa kushiriki M4C si kipimo cha mtu kutokupitishwa kugombea Urais. Anajenga hoja kuwa kazi ya kueneza chama si kigezo cha kuteuliwa kugombea urais. Tangazo la Zitto ni kugombea kupitia Chadema. Kama angetangaza kugombea kama mgombea binafsi hoja ya Mchange ingekuwa na mashiko, lakini kwa kuwa Zitto ataomba ridhaa ya wanachadema ili ashinde zaidi ya kuishia kugombea, hana budi kushiriki harakati za kueneza na kujenga chama mpaka vijijini. Naamini Zitto anafanya hivyo.

Kwa kile kinachoonekana ni kujibu hoja za watu wanaopinga hoja zinazotolewa na wapinzani wa Zitto, kuwa (Zitto) amekuwa hashiriki katika mikutano ya Kampeni ya Vuguvugu la Mabadiriko, Mchange anasema kuwa kazi ya kukuza chama inafanywa bungeni na katika vikao vya ndani vya chama. Kwa lugha nyepesi M4C si chochote. Ninavyofahamu M4C si mikutano inayoratibiwa na Chadema makao makuu peke yake. Hii ni kampeni inayopaswa kufanywa katika ngazi zote za chama na inaendelea hata wakati huu ambako hakuna timu kutoka makao makuu inayoongozwa na Dkt. Slaa au Freeman Mbowe. Ukiichukulia M4C kama kampeni inayopaswa kuongozwa na timu kutoka makao makuu, utaoona ushiriki hafifu wa Zitto, lakini ukichukilia kampeni hii kwa mapana yake lazima utaona ushiriki mzuri wa Zitto.

Mchange anaingia katika mtego wa wanaompinga Zitto. Anakubaliana na hoja ya Zitto kutokushiriki katika M4C na anafanya kazi ya kumtetea kwa kushusha harakati za chama chake, Chadema. Tafasiri ya hoja ya Mchange ni kwamba kampeni ya kueneza chama ya M4C ni kampeni dhaifu isohitaji ushiriki wa Zitto.

Ni kweli wabunge wa Chadema wamefanya kazi kubwa bungeni. Watanzania wachache wanaofuatilia vikao vya bunge ni mashuhuda. Hata hivyo mchango mzuri wa wabunge wa bungeni haiwezi kutumiwa na chama makini kama njia ya kutegemea kueneza chama. Kazi ya siasa inafanywa waliko wananchi. Huko ndiko unaweza kuona uhalisia wa maisha ya watanzania. Si nia yangu yangu kuzalau bunge, lakini ni wazi kuwa bungeni utaambiwa ‘Uchumi unapaa’ wakati uhalisia ni kwamba kipato cha wananchi wa kijiji cha Ngoma wilayani Ukerewe ni Tsh. 800 kwa siku. Mwanasiasa Mchange anaamini ndani ya bunge na vikao vya ndani vya chama ndio njia za kueneza chama hadi vijijini na M4C.

Moja ya Changamoto inayoikabili Taifa ni watanzania wengi kukosa nishati ya umeme. Chombo cha habari kinachomwezesha mtanzania kufuatilia vikao vya bunge moja moja ni televiheni. Katika nchi ambayo nishati ya umeme ni tatizo huwezi kutumia televisheni kama njia kuu ya kupeleke ujumbe wa ushawishi. Chombo pekee cha habari kinachoweza kuwafikia wananchi wengi kwa muda mmoja ni redio. Kwa bahati mbaya hakuna redio inayorusha moja mikutano ya bunge. Katika mazingira haya njia mwafaka ya kuwafikia watanzania popote walipo ni mikutano ya siasa. Mchange anaona anachofanya Zitto Bungeni kinatosha, na hakuna haja ya M4C.

Katika siasa unapata ujasili pale mawazo yako yanapokubalika. Unapata nguvu zaidi pale wanakubaliana na wewe wanakuelewa vizuri na hoja zako kwa ufasaha, na wana sifa na hoja za kushindana na wale wanaokupinga. Sina hakika kama Habibu Mchange ametumwa na Zitto au ametumia tu haki yake ya kikatiba kutoa maoni, lakini nikionana na Zitto nitamwaambia “Zitto, Habibu Mchange hana sifa za kukunadi”.
 
oko sawa katika issues analysis naweza kukuteua kuwa political strategist wangu wakati wa uchaguzi wa ubunge 2015
 
yani siju nikupo ngeze vipi,sio kwasababu umekandia mchange, hapana lakini kwa jinsi ulivyojenga hoja na kuzichambua bila ya kupepesa maneno.umefanya zizuri saaaaaaaaaaaaaaannnnnaaaaaa.
 
Hoja nzuri na ninaamini Hbibu kakupata ila kutokana na kichwa ngumu hatabisha kinafiki but all in all.....mesage sent.....
 
Hakika mkuu ww unamjua huyu kijana mchange. Nakumbuka wakati anagombea BAVICHA aliweka mtandao wa kupokea vijana na huku akiwapa pesa VIA MPESA yeye mchange tunamjua hana pesa za kuhonga je alihongwa na nani hilo ndo swali 2lijiuliza sisis watu makini. Tukajua baadae kuwa ZITO alikuwa nyuma yake ktk mpango wa kuteka ngome ya Vijana kwani alishamleta JULIANA M/M/KITI BAVICHA Na inasemekana akawa mwandani WAKE. MUNGU halali usingizi ule mpango ukavuja na MCHANGE akawa out of the Rase.

SS kazi ya mchange ni kuhakikisha anachafua Viongozi wengine ili mtu wake aendelee kuonekana anafaa kuwa RAIS. Juzi alionekana MBEYA akaenda mpaka kwa MTU wake wanaefanya uasi huu ndani ya kijana aliyegombea ubunge MBOZI EAST anaitwa MTERA MWAMPAMBA lakini hali waliyoikuta mbeya MCHANGE mwenyewe alisikika kukiri kuwa MBEYA ni ngumu kuingilika na hata huyo rafiki yake mwampamba na Juliana shonza walizuiliwa kufanya kampeni za udiwani ktk kata MOJA Huko mbozi. Ukiangalia kwa makini unajiuliza Mchange anapata wapi pesa za kuzunguka na kari aina ya PRADO Mikoani na huku source yake ya kipato ni mashaka.

MM sina tatizo na ZITO kutamani kuwa prezidal lakini njia anazotumia ni MBAYA SANA . hata udini unaotamkwa ndani ya chama WAKINA mchange ndo wanautumia kufikia malengo yao. Na ktk KUNDI hilo kuna habari baadhi yao MWIGULU huwa anawapatia pesa ya kujikimu tutazidi kufuatitia ukweli.
 
huu ndiyo uthubutu tunaouhitaji,si kutamka maneno huku umeficha mdomo.kweli na umesema kwa dhati ya moyo wako na pia tunamtaka mh.zitto atueleze ni kwanini anataka kugombda wakati akijua fika kwa mujibu wa katiba iliyopo hatukuwa na sifa?na kamhakikishia kupunguza umri?pongezi kwa uliyeleta mada maridhawa.sijawahi kumwamini ndg. zitto na hata wapambe wake wengi ni mashaka matupu mh.kafulila janga,bw.mchange walakini,mh.jk tatizo sijui akina zoka balaa.je nahitaji cheti cha darasa la saba kuamini kuwa huyu anayependwa na watu hawa ni mwema? kuna ajenda ya siri hapa si bure hakika.
 
mpepo

Makala aliyoandika Mchange hakuiandaa yeye. Mchange hana rekodi ya uadilifu katika utendaji. Kwenye uchaguzi wa BAVICHA pia kuna wanawake aliwatapeli kupitia SACCOS akatokomea na hela hadi wakaenda kumshtaki makao makuu

CHADEMA Tunavyopambana na ufisadi chama kisingeeleweka mbele ya jamii kwa kuwa na kiongozi mwenye tabia hizo katika jamii.

Gari aliyokua akiitumia Mchange kwenye uchaguzi wa BAVICHA ilikua gari ya Zitto. Hivi makundi yanayofadhiliwa na naibu katibu mkuu yatakifikisha wapi chama? Mbaya zaidi wanaamini watachukua chama au kugombea urais kwa kuwatukana viongozi wakuu wa chama na kukihujumu chama. CHADEMA kitaendelea kulindwa na wanachama na vijana wanaojua ni nini maana ya mabadiliko baadala ya tamaa binafsi

Ukisoma Makala ya Mchange ungeona jinsi alivyoongea kama Nape kwa kuikejeli M4C. Wakati yeye yupo nje ya harakati hizi alitegemea yeye na Mwampamba na Gwakisa wataebda Mbozi na kujiimarishia mtandao wa kukivuruga chama. Hadi leo Mwampamba yupo Mbozi kwa lengo la kuandaa mazingira ya kukihujumu chama hasa alipoona sasa uongozi wa kule umesimama kidete.

Mambo haya ndiyo chanzo cha vijana hawa kuanzisha kampeni za kutukana chama pale wanapoletwa katika mstari. Wapo radhi hata kushirikiana na CCM na mahasimu wa CHADEMA kuivuruga chadema kwa maslahi yao
 
Last edited by a moderator:
Mwampamba, Mchange, Juliana, Gwakisa ss hv Wanaganga njaa kwa kukishambulia chama na nina wahakikishia iko siku tutaleta ushahidi wa uhakika jinsi Mwigulu anavyowatumia na picha kabisa.

Ila kwa Mbozi, Mwampamba mambo yamemuwakia kwa kitendo cha kutukana viongozi wa kitaifa hasa Dr slaa. na vijana wa eneo la anapoishii MLOWA (sijui kama nimepatia) walitaka kumtandika kwani wanasema walijitoa sana wakati alipogombea walijinyima kwa ajili yake lakini ss ameonyesha dharau kubwa WANASEMA ni heri alishindwa kwn angeshinda angewadhalilisha na asahau kugombea japo sasa anajitahidi kuomba msamaha ili wao wanasema wako tayari kumsamehe ila DR SLAA ndo aende akamuombee msamaha, hapo ndo anakwama.
 
Habibu Mchange ni kijana mdogo, Limbukeni aliyekulia maisha ya shida pale kwenye kota za shirika la elimu Kibaha, ana ndoto kubwa kubwa za kuwa tajiri kupitia mlango wa siasa wakati kumbe dirisha analotaka kulitumia silo bali kaingia choo cha kike, Yeye kama anapewa pety cash na Zitto basi ujinga huo wamalizane ki vyao na si kuyumbisha CDM, Wakati wa uchaguzi wa 2010 CDM haikuwa imeandaa mtu mahususi kugombea na ndipo kwa haraka haraka kijana huyu akachukuliwa in a harsh way ili tu kuziba pengo pasikosekane mgombea.

wakati ule alikuwa mtiifu kweli kumbe nyang'au mkubwa kaficha kucha kwenye masaburi yake, ukifuatilia kwa umakini story za Uchaguzi kuna watu wa Kibaha wanaamini kuwa alishinda Ubunge pale Kibaha na palikuwa na mvutano mkali sana ndani ya chumba cha kuhesabia kura, lakini kitu cha ajabu dakika za mwisho alipokuja Mzee Makamba kijana akawasaliti wapiga kura na Tangazo likatolewa kuwa CCM imeshinda...

ukichanganya hiyo tuhuma yake ya kutoa rushwa ili achaguliwe kwenye BAVICHA hakika Mchange si msafi wa kumpigia debe kiongozi yeyote ndani ya CDM wachilia mbali huyo Zitto wake, Mchange ni dubwashana fulani ndani ya CDM na ni wakumdharau kama yule mbunge wa CDM kule Maswa
 
Jiwe la Ukara Good nimekukubali, watu wanadhani na kuamini eti M4C lazima itoke makao makuu, kumbe popote pale ulipo unatakiwa kueneza Chama kwa kuwaelimisha watu juu ya Sera, Falsafa na mikakati ya CHADEMA baada ya kuchukua dola 2015.

Kiukweli watu pia hawajamuelewa Zitto but Zitto is a good Strategist na ataisaidia sana CHADEMA hasa katika kupata mgombea urahisi, nyie mnaojifanya wafuasi wake, mnatakiwa kumuelewa kwani yeye ni sehemu ya taasisi inayoitwa CHADEMA otherwise mtaanguka na kumuacha Comrade Zitto standstill
 
Zitto anauwezo mkubwa sana katika siasa za Tanzania vijana wengi hawana uwezo huo,wanachokifanya ni kumpiga majungu katika harakati zake.
 
Zitto anauwezo mkubwa sana katika siasa za Tanzania vijana wengi hawana uwezo huo,wanachokifanya ni kumpiga majungu katika harakati zake.

uwezo lazima uende na nidhamu,kukosa nidhamu kwa mambo yako kunaondoa uhalali wa uwezo wako.hawezi pigwa majungu kama yeye si muanzisha majungu.mtu yeyote anaekuwa ktk jumuiya ya watu lazima atambue kuwa nidhamu pekee ndiyo itamsaidia kufikia malengo.
 
Makala yako imeyakosa kachumbari hii hapa.
Umeainisha vizuri kabisa kwamab Zitto ni ngao,kifua cha CHADEMA .Umemuunga mkono kutangaza nia ya Urais kwa asilimia mia moja.Nakupongeza kwa hilo.
Lakini umesahau kwamba nyumba haijengwi kwa tofali nzima tu,hata vipande vinahusika sana.
Zitto hajatangaza kuwa mchange ni mnadi wake wa kisiasa,WEWE WASEMA!
Zitto na mchange uhusiano wao upo wapi hujatueleza hapa
CHANZO CHA MCHANGE KUONEKANA NI SEHEMU YA ZITTO
Mchange anaonekana,ataendela kuonekana kama ulivyomchambua kwamba ni sehemu ya zitto hadi pale MCHANGE ATAKAPO AMUA KUFUATA AKILI YAKO YA KUMUUNGA MKONO MBOWE AU DR.SLAA
SIKU MCHANGE AKISIMAMA JUKWAANI AKAMUUNGA MKONO MBOWE NA SLAA NDIPO HAPO WEWE NA WAUMINI WENZAKO WOTE MTAKAPO SEMA MCHANGE NI KIJANA MZURI,MWANASIASA BORA.

LAKINI IKUMBUKWE WAZI NI BORA HAMSINI NZIMA KULIKO MIAMOJA MBOVU.KWA UCHAFU ALIONAO DR.SLAA KUANZIA KWENYE MSINGI WAKE WA KIDINI HADI MWENENDO WAKE NDANI YA CHAMA HATA MIMI SIWEZI KUTHUBUTU KUMUUNGA MKONO AU KUMFANYA AWE MODEL WANGU WA KISIASA
KWA NAMNA MBOWE ANAVYOKIGEUZA CHAMA KAMPUNI,ANAVYOWAJAZA WACHAGGA PALE MAKAO MAKUU NA KWENYE UONGOZI MBALIMBALI WA CHAMA MIKOANI,NAKUHAKIKISHIA HATA KWA MJEREDI SIWEZI KUMUUNGA MKONO.

MCHANGE KACHAGUA FUNGU LILIO JEMA ANAMSAPOTI NA KUMTETEA MTU AMBAYE HANA KASHFA ZA AKINA DR.SLAA AU MBOWE.
ZITTO NDIYE KIONGOZI PEKEE NDANI YA CHADEMA AMBAYE ANAKUBALIKA KWA VIJANA,WAZEE NA VIONGOZI WENZAKE KASORO HAO WAWILI NAO NIKWASABABU ZITTO ANAONEKANA KUWA NA POLITICAL CAPITAL KUBWA SANA NDANI YA NCHI NA NDANI YA CHAMA.

MCHANGE NI MWANASIASA SAFI AMBAYE SI MNAFIKI KABISA,AMEONESHA YEYE ANAMKUBALI NANI ANAMSAPOTI NANI KATIKA ULINGO WA KISIASA HASA UKIANGALIA SIASA ZA NCHI HII ZILIVYOKUWA ZA KINAFIKI.

ZITTO HATA MIMI NAKUUNGA MKONO,NAKUSAPOTI KISIASA NA WEWE NDIYE ULINIFANYA NICHUKUE KADI

NACHUKIZWA NA MWENENDO WA DR.SLAA
1.KASHFA YAKE YA KUSALITI DINI YAKE
2.KASHFA INAYOENDELEA HADI SASA YA KUONGOZWA NA MCHUMBA WAKE
3,KASHFA YA KUTENGENEZA MTANDANO WA MAJUNGU NA FITINA NDANI YA CHAMA
4.KASHFA YA KULA HELA ZA CHAMA
5.KASHFA YA KUFUKUZA VIONGOZI WA CHAMA KATIKA NGAZI MBALIMBALI ZA UKURUGENZI,MKOA NA TAWI KWA SABABU TU JOSEPHINE HAPENDANI NAO,ZITTO ANAKUBALIKA.
6.KASHFA YA NDOA,KUIBA MKE WA MTU,KUTELEKEZA FAMILIA[[/QUOTE]/QUOTE]
NDUGU WANA JF NAOMBA TUWE WAWAZI KWA KASHFA HIZO KWELI UNAWEZA UKATEGEMEA MTU KAMA HUYU KUWA KIONGOZI BORA?ANAWEZA KUWASEHEMU YA UONGOZI BORA? UNAWEZAUKAPOTEZA MUDA WAKO WA KUMSAPOTI?

MH:FREEMAN MBOWE YEYE NI MKIMYA SANA,ANAFANYA MAPAMBANO KWA MTINDO WA NOISE OF SILENCE.ANAWATUMIA AKINA HECHE,ANAWATUMIA AKINA DR.SLAA,ANAWATUMIA AKINA HAWA MWAIFUNGA,N.K WAPAMBANE NA ZITTO LAKINI ZITTO HANA MAKUU KABISA UKIMWITA HECHE HAPA ATAKWAMBIA ZITTO NDIYE KIONGOZI BORA KWAKE KWA SABABU ANAJUA NI NAMNA GANI AMEMSAIDIA KISIASA.
LAKINI AKIWA MBALI NA ZITTO ANATUMIKA KUMCHAFUA,KWA MANTIKI HIYO MCHANGE YUPO SAHIHI KUONESHA WAPI AMESIAMAMA NENDENI MKAMUONDOE.
 
Libasket b,

Kutokana na jinsi unavyojenga hoja wewe, Nazirona, na Mchange kwenye facebook, na hata makala yake kwenye gazeti la Raia Mwema wiki chache zilizopita, sioni ni kwasababu gani unadiriki kumwita Heche Kilaza. Kati ya watu wachache ndani ya CHADEMA ambao wanafanya kazi kubwa sana na nzuri sana ya ujenzi wa chama ni John Heche. Hili la kazi nzuri na kubwa anayofanya Heche ni dhahiri kwa kila mwananchi na hata CCM wanajua hilo, kwani hata ndani ya CCM hakuna kijana mwenye uwezo wa kufanya kazi kama anavyofanya Heche.

Hivyo basi, kwa baadhi ya watu wenye uelewa mdogo sana katika mambo ya kisiasa, wanaokaa kusubiri kulipwa fadhila kwa kazi ya kuwachafua wenzao kwenye media, hatuwezi kushangaa kwani hakuna kitu mnachoweza kufanya.

Mimi kila ninaposoma makala ya Mchange na hata hawa wanaochangia thread hii hata bila kuelewa ni nini dhumuni la thread mama kabla ya kuchangia upuuzi wao. kila ninapofanya analysis ya maandiko kama ya kwenu, hakika nashawishika kuamini kwamba hata kampeni meneja wa katibu wa mtaa hamuwezi kuwa, kwani mna uwezo mdogo mno wa kuwaeleza wananchi kuhusu uhalisia wa ni kwanini wamchague mgombea wenu.

Pia naomba niwafahamishe wote mnaowabeza watu kama Mnyika na Heche kwa kazi wanazofanya waache, kwani hakuna namna watafanikiwa kufikia utendaji wa hawa watu. Kuhusu Ben, ni ukweli kwamba simjui na hata yeye hanijui, lkn ninaposoma michango yake hapa JF, napata picha fulani kwamba atleast yuko organised upstairs kuliko hili kundi la Mchange na hata hawa wenye uelewa mdogo wanaotupotezea muda kusoma upuuzi wao hapa wakati hata makala mama hawakuielewa na wamebaki kutukana watu.

Naomba msamaha kwa wale watu makini nitakaokuwa nimewahudhi labda kwa lugha ambayo siyo nzuri, lkn hawa jamaa wenye uelewa mdogo wanatupotezea thamani ya thread mama ambayo imesheheni mambo muhimu ya kujifunza, na badala yake wao wameanza kuleta kebehi hata kwa watu wanaofanya kazi kubwa sana ya kujenga chama-CHADEMA.
 
Si busara kabisa kwa mtu yeyote ndani ya CDM kuzungumzia nani atagombea kwa sasa! Uchaguzi ukifanyika leo bado hatujawa na uhakikika wa 100% kushinda. Maana yake kuna kazi nzito mbele yetu ambayo lazima ifanyike kwanza.

Ingekuwa busara kama kila mmoja angeelekeza mawazo yake kuwa nini kiendelee kufanywa na CDM kuhakikisha kuwa tunakuwa na uhakika wa majority watakaoipiguia kura CDM miezi sita kabla ya uchaguzi.

Kuna kazi ya kupenyeza CDM katika kila kijiji na kuwa na kuwa na hakika kuwa wamejiandikisha na watakipigia kura chama badala ya kujadili mgombea kwa sasa. Ni busara kampeni zikawa za kichama kwa sasa badala ya za ki-mtu.
 
Back
Top Bottom