Zitto atua Igunga CCM wazidi kuweweseka

Zitto atua Igunga CCM wazidi kuweweseka

Nawafagilia barabara mkikosa kazi za kufanya muanzishe maandamano! Nawaandalia barabara nzuri za kwenda kuwamwagia watu tindikali na kwenda kuwapiga viongozi wenu
Najua lazima tuwe na binadamu kama ww Rejao!!maana hata science inadhihirisha hilo ili kufanya mambo yaende kati ya jamii flani lazima viumbe mtofautiane!!la sivyo "competition for resources will be high"lakini naimani ukweli unaujua.Ni utoto tu ukikua utaacha.
 
Hapa nilipo natafuta tiketi ya ndege ya Precision Air kwenda Igunga mimi na wanaharakati wenzangu kutoka Arusha tukampe Taffu muheshimiwa Zuberi Zito Kabwe! "Wao wanapesa sisi tuna Mungu! Hakika tutashinda. Have a nice weekend all!
 
CCM wakitaka kushinda IGUNGA wampeleke Lowassa na Chenge kuokoa jahazi, Mkama, Nape and the likes wasikanyage kule.
 
Nape anapwaya mara 360 kwa Zitto kabwe. Tena na kale katabia kake ka kutafuna tafuna midomo kama Mr Msoga ndio kabisa!
 
&lt;br /&gt;<br /> &lt;br /&gt;<br /> Hili jamaa sijui Lina akili gani hata silielewi.bila shaka limehongwa t shirt ya ccm.<br /> Achana nalo.
<br /> <br / kagewa moja ya suti alizohongwa muheshimiwa
 
Ndugu Watanzania,

Napenda kuchukua nafasi hii kuwaasa kuwa walioko Igunga watumie busara kubwa katika kutafuta kura. Chadema msikubali kuchafua CV yenu kwwa sababu za watu wachache wajinga wanaowatia vishawishi. Nawapongeza kwa kumkamata DC, kazi yenu kubwa iwe kukamata bila kupiga wala kukwaruza mahali. Kamata, piga picha, chukua movie, pelekea polisi kwa taratibu zingine japo najua zimwi likujualo....

Lakini nimesikitishwa sana na baadhi ya kauli za viongozi wetu. Imenisitikisha zaidi hasa kwa huyu anayeitwa sijui Kiravu sijui nani. Lugha aliyotumia yeye kujibu tuhuma za Chadema yeye ndo anaonekana MHUNI zaidi kuliko Chadema. Chadema hawakuwa na jinsi, lazima kilichotokea kingetokea tu maana wao wako kazini na wanajua utaratibu wa kampeni unasema nini wakati mikutano ya hadhara inaendelea. Lazima vijana wapate jazba kutokana na historia ya CCM. Sisi tuseme wao kule Igunga walikuwa na hasira lakini kiravu kwenye majibu yake alikuwa kwenye kiti chake.

Kiravu katika lugha ya maadili amekosa adabu, hana staha, amekosa heshima na kauli yake ya kuwaita Chadema wahuni asifikiri anamwita mtu mmoja au chama ajue anawaita watanzania zaidi ya milioni 2 na nusu waliokipa Chadema kura na rais wake. Viiongozi walioko serikalini wajifunze yanatokea Libya. Ghaddafi hakujua kama atatoka kwenye siagi-Kiravu acha jazba, yatakuja kukutokea puani. Kiravu na wenzako jitahidi kusoma alama za nyakati-mwisho wako unakuja, CCM haitaongoza milele, wala Rais Kikwete hatarudi tena kuwa Rais.

Namwambia Kiravu kuwa vijana waliomkata DC siyo wahuni, ni wasomi wana Degree zao tena siyo moja mbili na wengine zaidi, wamepigika na wanajua wanachokifanya. Asidharau dharua tu akifikiri serikali itamlinda, ajifunze yanayowatokea kina Chenge, Lowassa, Rostam, Ballal, Karamagi, Msabaha, na wengineo. Kiravu acha kiburi kwenye kiti ulichokalia, TENDA HAKI Mungu atakupigania. CCM siyo ALFA na OMEGA, mwisho wake unaweza kufika saa na wakati usiojua, siyo lazima 2015, hata kesho watanzania wakiamua wote mtaenda mafichoni.

MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU TUBARIKI SOTE TUNAOPIGANIA HAKI ZA WANYONGE.

Asanteni sana kwa kunisoma!
 
Mkuu kama ni cv atanishinda kwa kubebwa na baba yake,nasema hivi kama sio baba yake kumsafishia njia asingejaribu kuwa hapo alipo,endelea kupigia debe watoto wa washua na kamshahara kako ka manispaa

Umemjibu vizuri sana huyo kilaza.
 
wana magamba wameshikwa na kisebusebu na kiroho papo. jembe kijana limetua, bado mnyika nae yuko njiani
 
mhh swala la Mwigulu Nchemba, linanikumbusha kutukana wakunga, aliongea maneno mengi sana ya kashfa na matusi zidi ya CDM, Mungu huwa angojei ufe malipo ni hapa hapa duniani.

Nasikia sasa anahangaika na wife/girlfriend wake kusawazisha huku chama kikimsubiri kumbebesha mzigo wa kushindwa kwa uchaguzi kwa ufisadi wake wa mapenzi na kejeli. Watu wa Mungu wanateseka na maisha magumu halafu unawaletea kejeli. Siasa uchwara zinalipwa hapa hapa duniani.

CDM songa mbele kwani siasa za kizee za CCM na umasikini zinapitwa na wakati.

...plz mkuu naomba unijuze japo kwa ufupi hayo madudu ya aibu aliyofanya huyo Mwingulu Nchemba...
 
pambaf! acheni unafiki wenu nyie wachaga wa cdm,sio ninyi mnaomuona zitto msaliti wa chadema mpaka huwa mnashambulia kama paka mwizi? linapokuja swala la kuwasaidia wachaga kuchukua 'inji' au jimbo zitto anakuwa msafi na,lakini ndani ya chadema akitaka uongozi mnamtungia kashfa za kijinga,unafiki na upumbav mkiongozwa na yule mnafiki waaaaahed kubenea na kijarida chake cha mwanahalisi,mfano mzuri hii issue ya juzi mliyoileta hapa majuzi ya yeye kusaidiwa na BARRICK,hata slaa ole wake asije kufkiria kuwa mwenyekiti wa chadema! hakyamungu mtasema katumwa na anatumiwa,zitto,slaa,lwakatare na wote mliokimbilia huko mnatumiwa,utadhani mna macho yasiyoona,masikio yasoskia,bongo zisizozingatia! poleni vilaza wa chadema nchini kote
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom