Zitto asikitika wanaombeza Nape

Zitto "ANAYEMLIPA MPIGA ZUMARI,NDIYE ANAYECHAGUA WIMBO" KWA KIMOMBO "HE WHO PAYS THE PIPER CHOOSE THE SONG"
Kama(ZITTO) wewe unamlipa mpiga zumari (NAPE),nafikiri utakuwa umechagua wimbo gani uimbwe,kama haumlipi huwezi chagua wimbo,au ni ile sumu ya wote wabunge vijana,kwa hiyo mtakuwa na vision moja,ok But NAPE ALIWAHI SEMA "Ukiwa mnafki ujanani,utakuwa mchawi uzeeni".Napita tu
 
By.
Zitto Kabwe: Kwenye siasa ya nchi Kama zetu busara ya mapambano ni Jambo la msingi sana. Kama Nape wa CCM anaunga mkono hoja ya upinzani kuhusu posho, asibezwe wala kuzodolewa. Anapaswa kuungwa mono ili kuongeza Jeshi na kumkinga dhidi ya wapenda posho ndani ya chama chake. Akibezwa, siku nyingine Batak ga mono Jambo hata Kama ni jema kwa nchi. Hii ndio huitwa hekima za harakati. Nimesikitishwa sana na wanaobeza kauli ya Nape kuhusu posho za Wabunge
Kabla hatujaanza kumpiga madongo Zitto, haujatuhakikishia chanzo cha habari yako ulipokitoa labda ni ya kwako wewe kama bourne.
 
zitto,ningependa ujue hapa hakuna anayembeza nape.sisi kama jamii ya wasomi, lazima tuangalie mambo from all directions.wote tunajua nape katumwa na ccm. Wote tunajua asilimia kubwa ya wabunge ni ccm na hawa wabunge ndio vinara wa kutetea hii posho.leo uje utuambie ccm inapinga posho? Big no. Ukiniambia hiyo ni kauli ya nape hapo nitamuunga mkono. Mimi nimekosa imani na misimamo ya ccm tangu ulipoanza msemo wa ''kuvua gamba'' this is just a very interesting comedy.
nimeipenda hii, kaka uko sahihi, nape katumwa tu baada ya hawa jamaa wa ccm kupima upepo, hakuna ubishi walomtuma ndo wapenda posho wakubwa, kwani malalamiko ya zito juu ya posho ni ya mda mrefu, uyo nape alikuwa wapi??? Nape muongo mkubwa uyo
 
wasioelewa siasa ndo watakaombeza nape, lakini mpevu yeyote wa siasa (kama mimi) hawezi kumbeza nape hata kidogo, kwani nape anastahili kupongezwa yeye na chama chake kwa kuuuonesha umma wa watanzania juu ya msimamo wa chama hicho cha kijani na njano....!!

Tatizo hatuelewi ni msimamo wa nape au wa ccm,mfn.alitutangazia ishu ya kujivua gamba kama sera ya chama cha kijani chama chake hichohicho kikasema amejitungia,so which is which??
 
Siasa ni game la kusisimua sana. Mara unanaswa mara unajinasua. Ukitaka kuucheza vizuri lazima uwe makini sana. Very interesting.
 
mbunge wa kigoma kaskazini, Zitto Kabwe (Chadema), ameutaka umma usimbeze katibu wa Halmashauri kuu ya Taifa (NEC) ya CCM Itikadi na Uenezi Nape Nnauye juu ya tamko lake la kupinga posho mpya za wabunge kwa kusema kuwa alichofanya ni hekima za harakati. Aidha Zitto amesema kuwa hoja hiyo isifanywe ya chama bali posho hizo zifutwe.


My take;tuweke siasa pembeni kwenye masuala yenye maslahi kwa taifa.ongezeko la posho kwa wabunge ni janga la kitaifa.

source;habarileo na facebook
 
ni kweli zitto yuko sahihi na Nape yuko sahihi,tunatakiwa kuweka pembeni siasa pindi tunapojadili masuala muhimu kwa taifa kama hili ndo mana hata viongozi hawa wakuu wa vyama vikuu hapa nchini bila kutarajia wamejikuta wakuungana.wabunge wetu wanaipeleka nchi kuzimu kabisa.hapa watasema heri tule majani lakini posho kwa wabunge ziongezwe.
 
Nape yuko sahihi kabisa lakini kinachowafanya watu wakose imani nae ni hawaonekani kuwa na nia dhabiti ya kuzuia hizi posho. Mara nyingi Nape hutumia kauli kama "CHAMA KINAIGIZA SERIKALI KUFANYA a,b,c...", mbona hatusikii wakisema "TUNAIGIZA SERIKALI ISIONGEZE POSHO ZA WABUNGE" badala ya wanatoa misimamo kama wao sio "WENYE DUKA"

We need real conviction not wind dependent rhetorics.
 
Kwa cheo alicho nacho Nape, siwezi kumuunga mkono kwa kauli moja moja anayoitoa. Katika siasa kubwa mtu huungwa mkono kwa msimamo wake wa ujumla, sio kwa kauli moja moja. Ndio maana nadhani hata leo hii RA akiibuka na kupinga posho watu bado hawatampongeza kwasababu msimamo wake wa ujumla unajulikana.

Leo Dr Slaa akiunga mkono suala la posho watu watakaa kitako kusikiliza hoja zake, kwasababu msimamo wake wa ujumla watu wanaufahamu.

Zitto leo ukisimama na kusema JK ni Rais mzuri, watu hawatashangaa kwasababu huo umekuwa ndio msimamo wako (haitakuwa news), lakini leo ukitoa kauli kuwa JK ni rais mbaya sana, itakuwa news kwasababu utakuwa umepinduka kutoka kwenye msimamo wako unaojulikana
 
Zitto,

Ningependa Ujue hapa Hakuna anayembeza Nape.

Sisi kama jamii ya wasomi, Lazima Tuangalie Mambo from all Directions.

Wote tunajua Nape katumwa na CCM. Wote tunajua asilimia kubwa ya Wabunge ni CCM na hawa wabunge ndio vinara wa kutetea hii Posho.

Leo uje utuambie CCM inapinga Posho? Big No. Ukiniambia hiyo ni Kauli ya Nape Hapo nitamuunga mkono.

Mimi nimekosa Imani na Misimamo ya CCM tangu ulipoanza msemo wa ''Kuvua gamba'' This is just a very interesting comedy.
Nashindwa kuelewa, msimamo wa Nape ni wa Nape binafsi au NI msimamo wa CCM?
 
Mheshimiwa Zitto hapa sintokubaliana na wewe hata kidogo... Nape ni MNAFIKI na hata siku moja huwezi kumpa sifa Mnafiki ambaye anayasema haya kwa malengo yake binafsi na anapokea posho vile vile, sawa na viongozi wa Chadema wanaopinga Posho lakini WANAZICHUKUA tena wengine wameisha pokea posho mpya. Mnafiki siku zote hugonganisha pande mbili zivurugane kwa faida yake na ndio siasa za bongo.

Mimi naomba jibu kutoka Chadema na NCCR, hizo posho mnazopokea sasa hivi bila kutaka zinapelekwa wapi?.. chama kina mpango gani wa kukusanya fedha za posho za wabunge ili kuzirudisha kwa wananchi maana kusema tu wakati mnazitumbua haitoshi...Mimi ningependa sana kuelewa haswa matumizi ya Mbunge yamepigwa hesabu vipi.. 1. Mshahara umekadiriwa kutokana na nini? ikiwa anapewa gari halafu posho ya Usafiri na mafuta, posho ya vikao vya bunge na sijui posho ya nini na nini maana nasikia kuna posho aina tatu.

Leo imefikia kiasi kwamba kila msomi leo anakimbilia siasa na Ubunge kwa sababu kuna ndiko kwa kutokea kimaisha. Na imefikia hadi watoto hawapendi Udaktari wala uinginia kwa sababu siasa za kupiga domotindi zinalipa..
 
Mheshimiwa Zitto hapa sintokubaliana na wewe hata kidogo... Nape ni MNAFIKI na hata siku moja huwezi kumpa sifa Mnafiki ambaye anayasema haya kwa malengo yake binafsi na anapokea posho vile vile, sawa na viongozi wa Chadema wanaopinga Posho lakini WANAZICHUKUA tena wengine wameisha pokea posho mpya.

Mimi naomba jivu kutoka Chadema hizo posho mnazopokea zinapelekwa wapi, chama kina mpango gani wa wabunge kuzirudisha kwa wananchi maana kusema tu wakati mnazitumbua haitoshi...Mimi ningependa sana kuelewa haswa matumizi ya Mbunge yamepigwa hesabu vipi.. 1. Mshahara umekadieiwa kutokana na nini? ikiwa anapewa posho ya Usafiri, mafuta, posho ya vikao vya bunge na sijui posho ya nini na nini...kiasi kwamba kila msomi leo anakimbilia siasa na Ubunge kwa sababu kuna ndiko kwa kutokea kimaisha. Na imefikia hadi watoto hawapendi Udaktari wala uinginia kwa sababu siasa za kupiga domotindi zinalipa..

Well said, Busara na hekima ziko hapa. Brother wakati mwingine unapotea-ga sana hapa jamvini
 
Back
Top Bottom