Zitto anataka kusaliti CHADEMA?

Status
Not open for further replies.
Pia katika Taarifa hiyo ya habari japo kwa mwisho nimekuta Jaji Mkuu Agustine Ramadhani akimalizia kueleza kuwa; "Suala la mabadiliko ya Katiba linawezekana, kwani Tayari nchi nyingi zimefanya na kuzitaja Kenya na Uganda na kusema linazungumzika na lina namna yake ya kujadiliwa," Mtangazaji akauliza iwapo kitendo cha wabunge wa Chadema ni kosa Kisheria, Jaji mkuu anajibu "Siyo kosa kisheria, pengine lingeandaliwa katika kanuni za Bunge lakini pia anaamini kuwa hakuna kosa na ndiyo maana Spika hakusema lolote, lakini sana sana tunaweza kulielezea kama ni swala la maadili tu lakini si sheria".
Hii ni kwa Mujibu wa TBC 1 habari ya saa 2 usiku.



Jamani mbona saa mbili usiku haijafika !!
 
kwa siasa za Zitto sidhani kama chama kinaweza kufanikiwa katika adhima yake ya kufikia malengo ya katiba mpya na tume mpya si vizuri kuwa-let down wenzio
 
Zitto akate au akubali ni binadamu kama binadamu wengine ila ukweli unabaki pale pale kuwa tunahitaji katiba Mpya
 
Hili ndilo ambalo baadhi yetu tumekuwa tukisema. Ukweli suala la kutoka nje ya Bunge halikuwa uamuzi wa Wabunge wote. Pia yale maelezo ya Dr Slaa kwenye clip ya Mwanakijiji nayo pia hayakutoa ufafanuzi juu ya madai hasa ya CHADEMA. Hapa pia ningependa nimsikie Dr Mkumbo. Naamini analo la kuongea. Si hivyo tu, maamuzi yao yamekuwa hayaeleweki nusu wamo na nusu hawamo.
 
Zitto alisema kuwa wanasubiria hatma yake katika chama na kusema kuwa hiyo ndiyo gharama ya demokrasia. Ila amekanusha kuwa jambo hilo lisifikiliwe ni mgawanyiko bali mtazamo tofauti wa mawazo.


please rekebisha title yako mgawanyiko amethibitisha wapi???? Angalia kwenye nyekundu
 
Jamani mbona saa mbili usiku haijafika !!

Nilizoea Taarifa ta Habari TBC kuanza saa 2 lakini kweli nadhani haikuwa saa mbili leo imeanza mapema maana nami nilikuwa na tune kwa bahati mbaya ndo nikakuta jaji anaongea.
 
jamani hapa cha ajabu nn? kutofautiana na kuonyesha wazi msimamo wako na so kuburuzwa tuuu unaondoa kuonekana mnafiki!!! ni chama gani chenye democrasia hii, hakuna... fanya hivyo CCM uone, muulizeni 6, ni majeruhi wa haya kutofautiana na misimamo kandamizi ya cc, wee wach bana!! Hii CDM ni D ya kweli
 
Zitto anataka kuleta challenge za namna gani tena? au ndiyo yale mambo yetu ya kuitwa na kula pilau?
 
zitto ameongea vizuri sana... tatizo humu jamvini tunataka mambo ya upinzani yaende kama mechi ya kinondoni muslim na tambaza

na hayo ya kupingana yangetokea ccm kesho ungesikia mtu katolewa chamani
ni kweli uliyosema halafu kuna njama za kumuandama zitto humu jamvini .
Hata wao ccm waligawanyika kwa suala la Sita kuenguliwa na wamesema ni demokrasi ila hakuna aliye waandama.mbona demokrasia ni hiyo hiyo aliyotumia zitto na wenzake? waungeni mkono na siyo kumwandama Zitto
 
Hivi unajua kwamba naanza kuwachukia Zitto na Shibuda? Haki ya nani vile.

Msaliti dawa yake ni KIFO shen$%%^ kabisa!
Huna sababu ya kuwachukia. Kuna watu vichwa vinafanya kazi. Wanamptisha waziri mkuu na wanaomba serikali inayoongozwa na mtu wasiyemtambua asikilize madai yao!!!!! Kuna haja ya kufikiria upya strategies za namna hii. Zitto anatambua wazi kuwa strategy hii ni fake maana February watakuwa bungeni na wanahitaji kujadili hotuba ya Rais. Wakisusa kwa CCM ni mteremko tu maana hata utendaji wa serikali hawataujadili na kwa kifupi CCM watapeta zaidi. Nadhani aliyeshauri strategy hii alisahau kuangalia mbeleni. Mnakumbuka kura za maruhani Zenji? CHADEMA wanayaweza haya?
 
Suala la wabunge wa CHADEMA kutoka bungeni usiwe mjadala wa ajabu, message sent to wezi wa kura.

Nawashanga CCM kuandamana, tunaomba kama mpo serious basi jaribuni kuwasimamisha wabunge wa CHADEMA kama alivyosema anayejiita katibu mwenezi then YOU WILL SEE MOTO!
 
Siku zote nasema namkumbuka Zito toka Daruso, hajabadilika, sidhani kama atabadilika. Huyo ndio Zito.
 
Katika kuonesha hali ya masikitiko Mh zitto zuberi kabwe amepingana na kitendo cha chadema kutoka nje ya bunge, akiongea na TBC leo Zitto amesema yeye kama yeye hakubali kitendo cha chadema kuwalk out

Big Up ZITTO :lock1::lock1:hapo umeonesha ukomavu wa siasa
karibu chamani:clap2:

Kabwe alionesha hali ya masikitiko alipogigwa mabomu na wachakachuaji, alipona madhara baada ya mdogo wake kujitoa mhanga. Kwa nini unadhani ukomavu wa kisiasa ni kuiunga mkono ccm tu? je mafisadi ni wakomavu wa kisiasa? wewe ni taahira miongoni mwa mataahira wachache wenye uwezo wa kusoma na kuandika lakini hawana uwezo wa kutathminini wanachokiandika.
 
I dont see an issue (hapa tuna make a mountain out of a mole hill) kutokukubaliana ni kawaida kura zikapigwa wengi wakashinda thats normal lakini i think Zitto angekaa kimya tu there is no need awaambie vyombo vya habari what went behind the scenes

nakubaliana na wewe, hakukuwa na haja ya kueleza haya yote kwa waandishi wa habari. kwani yeye ni msemaji wa chama?
 
tunapopotosha ukweli namna hii, hatutakaa tuendelee... TBC1 wameweka vizuri sana, there was a voting going on, he didnt support the motion and that was democracy

It is highly disappointing mtu kusema hivi aisee

One thing for sure, Zitto has defied many for very long time and he will continue to do so kwani hana akili fupi kama baadhi yetu humu. in addition, hii ya kutoka nje ya ukumbi inawauma nini wakati mmeshaamua kwamba mtapitisha motion ya kuwasuspend?
 
Dogo asituzingue anataka kuwa KIHEREHERE sana km amechoka atimuke walikuja na wakaondoka kwani yy nani? Mwenendo alionao sasa unmpeleka pabaya km hakukaa chini na kufikiria cha kusema kbla hajaulizwa. Umaarufu wake naona unazidi kushuka kila siku na ataishia km kina TUNTEMEKE SANGA .
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom