Zitto amtembelea Lema gerezani baada ya kunyimwa dhamana

Zitto amtembelea Lema gerezani baada ya kunyimwa dhamana

dah yaani mbowe na lowassa na wanachadema kibao wamemkaushia....siasa ni ngumu sana
 
Naona hii nchi binaadamu ni Wanasiasa tu, hao Wapiga kura Gerezani huwa wanatembelewa lini? au mpaka Mwanasiasa aingie humo ndio Wanasiasa wenzake wakamsabahi?
 
Zitto nowadays hapatikani kabisa FB
 
Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema kwa mara nyingine leo (jana) amenyimwa dhamana na imeamriwa na mahakama kuwa akae mahabusu mpaka Februari mwakani kesi yake itakapotajwa tena.

Mahakama imetoa uamuzi huo baada ya kuridhishwa na vigezo vya kisheria ambavyo vilitolewa na mawakili wa Jamhuri ambao waliweka pingamizi Lema asipewe dhamana.

Zitto Kabwe ambaye ni Mbunge wa Kigoma Mjini (ACT-Wazalendo), alimtembelea Lema gerezani leo na haya ndiyo ameyaandika kuhusu Lema, kesi yake na hali ya kunyimwa dhamana.

ZITTO KABWE:

Leo (jana) Ijumaa Desemba 2/2016 nimepata fursa ya kumsalimu ndg. G Lema, mbunge wa Arusha Mjini Katika Gereza la Kuvu la Arusha. Nimemtembelea Kama mbunge mwenzangu na kumhakikishia solidarity katika harakati za kutafuta na kulinda haki.

Lema ana ari kubwa ya mapambano. Anasikitishwa sana na ukiukwaji mkubwa wa haki na mahakama kuonekana kuendeshwa na Serikali. Yeye ameona ni bora akae ndani mpaka hapo dola itakapopenda kumpa dhamana. Kosa lake lina dhamana na hakimu alimpa dhamana.

Ameomba tutazame mahabusu wengi wanaokaa ndani miaka mingi bila kesi zao kuendelea. Tuwatetee.

Amemshukuru Mungu Kwa kumpa mke jasiri anayempa moyo na ndio ngome yake kwa sasa.

Nimemwomba Lema aone kuwa hii struggle sio yake peke yake bali anawakilisha watu wengi wanaotaka haki kutendeka katika uendeshaji wa nchi yetu. Siku zote haki hushinda.

CHANZO: Maandishi Genius
Awamu ya tano inaimatisha upinzani kwa stahili ambayo baadae watashindwa kbs kuudhibiti....maana wanatengeneza watu jasiri,watakaokuwa tayari kupambana,kukaa jela na hata kufa!muda utatuambia!
 
Kuna vitu wanasiasa wetu wanatakiwa kijifunza kutoka kwa Zitto lakini cha ajabu kuna baadhi ya pro-Chadema watakuwa wamechukizwa na hili.
 
Hii ni aibu kubwa sana kwa Mahakama Zetu.
 
Zitto alivyo na siasa za bila kumtukana MTU
Wala kumvunjia heshima mtu

Alipaswa kumpa ushauri huo lema
Ili afanye siasa za akili na sio kutafuta kick kwa matusi
Acha ujinga mtochini, ebu tuambie matusi aliyotukana? Mh Zitto amesema tuko nyuma ya Lema kwa ajili ya kutafuta haki.
 
Mie natamani lema akae huko walau mwaka mmoja tu
Huyu kazidisha upuuzi
Ndio akili yako, kutamani wenzako wafe ili ufurahi, ujue na wewe yatakupata kabla jua halijachwea. Lakini kwa kuwa unawaju wanaomuweka ndani ongea nao, wamuweke huo mwaka ambao wewe na familia yako mtufutahi.
 
Ili kuendeleza solidarity kwelikweli na Ruyagwa atukane tukane viongozi wa nchi ili wakaungane gerezani. Lissu alitukana tukana, lkn amenyooshwa sasa ni mtu safi sana
 
Hongeta Zitto kwa ulichofanya, msife moyo katika kusimamia yale yaliyo kweli na kumweka mtanzania huru.
 
Tunazungumzia suala la haki za binadamu kama vile halituhusu, siku yakitufika na sisi ndipo tutakapoona umuhimu wa watu km lema, kama mnabisha tusubiri... Lkn tukumbushane wakati mikutano ya wanasiasa inazuiwa kinyume na katiba, Zitto aliwaambia waandishi wa habari. wakubwa wakitumaliza nyinyi mtafuata wakacheka, île sheria ya habari wakubwa wakiamua hata kesho watafunga vyombo vyote vya habari wanavyovichukia kwa mujibu wa sheria, ndugu zangu Uwovu tuupingeni ili usije ukaturudi
 
Back
Top Bottom