1. Watanzania tunadanganyika kwa urahisi sana! Na Zito yote anayoyafanya ni kwa kujua kwamba nchi hii inalo kundi kubwa la watu wanaomuamini kwamba ni mzalendo. Ni kwamba anajua hamsomi sana sana vichwa vya habari za magazeti na mnaamini moja kwa moja bila kufikiria zaidi na kufanya uchambuzi. Tatizo ni kubwa.
2. Watanzania tupende kusoma ili tuweze kujadili mambo kwa weledi. Zito aliyoyafanya kwenye Escrow ni kwa kutambua kwamba hatupendi kusoma. Kuthibitisha kutopenda kusoma kwetu, Mtanzania mmoja Bw. Salim Khatri, kwa kujitolea, alijihusisha kusoma taarifa zote yaani ile ya CAG na PAC amekuja na uchambuzi wa kina kuhusu hizo taarifa na akabainisha jinsi ZITO KABWE alivyo handisi taarifa ya PAC.
3. Huo uchambuzi wa kitaalam wa Bw. Khatri, uliwekwa wazi kwa Wahariri Wakuu wa vyombo vya habari nchini kwenye Semina ulioandaliwa na VIP Engineering & Marketing Ltd., kwa kushirikiana na Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF). Semina hiyo ya siku mbili ilifanyika kwenye hoteli ya Stella Maris mjini Bagamoyo, tarehe 3 - 4 Aprili, 2015.
4. Wakati wa Semina hiyo Bw. Khatri, akiwa patia wahariri wakuu fursa ya kuuliza maswali. Wahariri waliuliza maswali yao na kujibiwa. Hitimisho la Mada hiyo washiriki wote walikubali kwamba ZITO KABWE alihandisi taarifa yake kwa manufaa yake. Hii ni bila kujali taharuki aliyolisababishia taifa na kuhatarisha kuiangusha serikali.
5. Wiki moja baadaye, Zito katika hali ya kutahayari, bila kutafuta ukweli, akaamua kumshambulia binafsi Bw. James Rugemalira wa VIP. Baadhi ya magazeti yameandika uzushi wa Zito kwa kuhusisha waliyoyasema wahusika wa MWAPORC, kwani Wahariri wa magazeti hayo walikuwa wanazo taarifa za kina kuhusu mradi huo na wahusika wake. Wapo pia walioziandika habari za Zito kama kabisa hawana wajualo!
6. Juzi iliwekwa hapa JF taarifa ya uchunguzi ya Bw. Khatri, kutuonyesha UONGO wa taarifa ya PAC. Badala ya watu kuisoma kwa makini ili waichambue na kuikosoa, kwa kutojua wakatenda dhambi ya kukataa kusoma. Ninashindwa kuamini kwamba mtu ambaye hajasoma taarifa anavyoweza kusimama na kuikataa! Msemo wa Mao "no research no right to speak" hapa unakuwa na maana kubwa sana.
7. Watanzania wenzangu ninawasihi tuache uvivu wa kusoma. Hii ndiyo sababu kubwa ya kukimbilia kwenye umbea na kuhadaika kwa wepesi kwa watu aina ya Zito. Mkiisoma Kazi aliyoifanya Bw. Khatri, ninaamini mtaona jinsi wanasiasa wadanganyifu na wasaliti wa nchii wanavyo iangamiza nchi yetu na Zito akiwa ni mmoja wao.
8. Kazi ya Bw. Khatri, inadhihirisha kwamba Bunge linatumiwa na wanasiasa wabaya, walaghai, wazandiki na mafisadi kuihujumu nchi. Kazi ya Khatri, inaweza kuwa ndiyo mwanzo wa kukomesha huu uhuni ambao waheshimiwa wanatumia pesa zetu ili kuihujumu nchi.
9. Tusipokuwa makini, tujue kwamba tunajikaanga kwa mafuta yetu. Zito anatahayari badala ya UONGO wake alioufanya akiwa M/Kiti wa PAC kuhusu Ripoti Maalum ya Akaunti ya Tegeta Escrow kugundulika. MWAPORC haujawahi kuwa mradi wa Serikali kama alivyowaeleza Wahariri Wakuu kule Bagamoyo. Zito ana tapatapa za mwizi arobaini zimetimia. Wanasema, "you can fool some of the people all the time but you cannot fool all the people all the time". Watanzania, someni taarifa ya Bw. Khatri, kama kuikataa iwe ni kwa hoja na siyo milio kama niliyoisoma hapa JF.
Mungu Ibariki Tanzania!