Zitto amlipua Rugemarila wa Escrow

Zitto amlipua Rugemarila wa Escrow

Mtu anaeibua madhambi kama haya bado tu mnasema ni mfuasi wa CCM? Ni mwendawazimu pekee ndiye atawaza hivyo.

Safi sana Zitto. Huu ndio uzalendo.

wanajitoaga akili tu,wanashindwa kujua Zitto anapendwa na Taifa zima si kwa sababu ya chama,Bali uzalendo wake
 
Wangepewa Wachina au Wazungu hiyo Tender ingelalamikiwa?...
kwani kuna aliyelalamika hapa tumeuliza utaratibu wa kupata zabuni, sio kugawiana kama pipi matokeo yake mzigo ukitoka watu wanaambiwa wakafungue akaunti Mkombozi na stanbic.
 
Zitto amesema Rugemarila amepewa zabuni hiyo yenye thamani ya shilingi trilioni 54 bila kufuata taratibu za zabuni ikiwa ni pamoja na zabuni hiyo kutangazwa.

Duuuh project ya TZS 54 trillion? Hii figure mbona ni kubwa sana. Wengine tumezoea kuziona figure za namna hii kwenye project za NASA huko.

ZZK awe na uhakika na hili pasipo shaka maana ninavyomfahamu Mzee Sitta na kufyatuka kwake akiipata weakness moja tu kwako anaweza kukujeruhi vibaya.
 
Mtu anaeibua madhambi kama haya bado tu mnasema ni mfuasi wa CCM? Ni mwendawazimu pekee ndiye atawaza hivyo.

Safi sana Zitto. Huu ndio uzalendo.

mwakyembe alivyomuangusha el, karamagi na wenzale alikua nld? filikunjombe tlp?
 
Tuache siasa kwenye maendeleo, kama hawa Jamaa wameandika proposal zao , wakashirikiana na serikali wakaenda world bank kwani kuna mtu katukataza sisi kwenda TIC kuchukua projects ambazo zipo na wewe utafute uwekezaji , Huyu mzee anajua kutumia fursa si Wa kulaumiwa hapa kwa kweli jambo la kulaumu ni mfumo wetu na si rugemalira , manake hawa watakuja tu wengine .
 
usilaumu watendaji, kosa ni letu, kuwaachia wapuuzi wachache wafanye wanachotaka

Yaani umenena mkuu...na kosa letu kubwa tunabaki tumejiinamia na kusema..Mungu atawalaani...na iko siku yao. Sisi wote tunajukumu la kuifanya hiyo siku iwe leo/sasa...
 
tsz 54 trillion!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!.......
 
Alie waloga waTanzania kafa, na mganga kafa
 
..kila mtanzania nchi hii amekua mpiga dili...yani nchi imegeuzwa "banana republic" na watanzania wenyewe....Utashangaa kila mtu anakemea jambo ambalo kwake anaona lina maslahi.....kama halina maslahi kwake na family yake basi halikemewi....ndipo TZ ilipofikia sasa....Hata huyu Zitto analiongelea hili kwa sababu tu za maslahi yake kisiasa...maana kama alikuwa kweli ana uchungu wa jambo hili anajua wapi pa kulisemea.....Hizi ni dili tu kuelekea uchaguzi mkuu....

..Taifa hili litabadilika pale tu tutakapoacha kutawaliwa na viongozi walafi na wanafiki.....
 
Na ndio sababu Kulwa akabeba lumbesa zenye mabilioni na kwenda kugawa ndani ya Ikulu kwa akina Gurumo, watendaji wengine ndani ya Ikulu ikiwemo familia ya Doto kwa kujua fika Doto hatatia neno kwa mabilioni hayo kugawiwa ndani ya Ikulu.

Rugemalira na rahisi wa Danganyika ni kulwa na doto!!!
 
Mimi nawalaumu upinzani hawa jamaa kwakweli we might as well stick to single party politics hakuna chochote wanachofanya au kufuatilia kwenye maswala ya maendeleo kazi yao ni kuropoka tu kwa vile vilivyopo lakini mambo ya kufuatilia what is cooking serikarini muda huo awana kabisa.

Kwa sasa siasa zetu lazima jamaa wajue miradi ya serikari na jinsi inavyokuwa financed na kama inatija kwa walipa kodi sio sababu za uchumi tu kama the sales man would have pitched but value yenyewe ya mrdi; aiwezakani tufanywe wajinga kiasi hiki yaani mtu yule yule kwa namna ile ile ambapo ana hela anapewa tender bila ya kuwa na shillingi.

Halafu ndio akatafute mwekezaji sasa ni kigezo kimetumika si ndio haya mengi anayataka pia kwenye vitalu vya gesi, serikari mkopo aijali watakao pewa wawekezaji utakuwa na masharti gani awajui kama jamaa wanaweza maliza mradi ontime kwa sababu awana hiyo experience na majukumu ya malipo yatakuwaje after the grace period kama bandari aijaanza kazi (to name few risks).

Yaani same thing as IPTL in terms of its early phases na wakati ata hiyo escrow aijapowa my god seriously yaani huku ni kufanywa taifa la wapu.mbavu kupindukia.
 
wanajitoaga akili tu,wanashindwa kujua Zitto anapendwa na Taifa zima si kwa sababu ya chama,Bali uzalendo wake

wewe ndo unaempenda usitulishe maneno.sisi tunajua hiyo ni kiki tu ya kutaka kuungwa mkono katika harakati zake kisiasa.
 
Haya ndio yanayotakiwa kwa wapinzani lkn watu hawayataki wataka malumbano tu
 
Back
Top Bottom