Zitto aenda kutibiwa Ujerumani

Mkuu Kero,

Unaweza kusoma hiyo post yako kwa sauti kubwa hapo ulipo na kama kuna watu jirani?

Huu udaku sijui una umri wa miaka mingapi
 
Broda Ben, naona kama umeanza vizuri sana mpangilio wa hoja zako, lakini hapo kwenye red hapajatulia! Mzee JKN alienda kutibiwa broda, si kuchekiwa!...huoni ugonjwa wake ukawa serious hadi kumnyoosha?


Asante Broda PJ,

Alipoaga nchini aliaga kuwa anaenda kufanyiwa checkup lakini......
 
Huyo jamaa naye kizunguzungu, ukimuangalia amebakiza kichwa tu na mdomo wa kuzungumza, anaishi na stress nyingi sana huyo bwana mdogo, anakunywa sana pombe na demu wake yule, yaani kiufupi ni kama amepoteza muelekeo, Pale mara nyingi Zoungh garden yaani anajidhalilisha, wewe kijana mdogo mijipombe isiyo ya lazima yanini yarabi?
Ameo ka sister do sasa kanampeleka hakuna hata maadili kamebakia jina tu ni katotorial asistant pale UD japo kwa ufinyu wa walimu nako kanaitwa lecturer.
Kijana mwenzetu hajapata mke mwema!!
Taabu kabisa sasa afya mgogoro mara misuada hiyo.
Shwine kabisa kabisa

Makubwa sasa! Una maana kuwa ameka***** miw***?
 
Kwa maoni yangu, safari ya Ujerumani ilikuwa imepangwa kabla. Haiwezekani mtu ajisikie vibaya Alhamisi, atibiwe zahanati a Bunge, Ijumaa aje Dar, Jumamosi huyoo Ujerumani.
Taratibu za kutibiwa nje ya nchi ni ndefu unless it is real emergence. Mhe. Zitto hakuwa na dharura ya kuhivyo kukimbizwa hospitalini Ujerumani, ila kwa vile safari ilikuwepo, na amejisikia uchovu, akaamua ngoja tuu akachunguzwe huko huko.

Kitu ambacho lazima tukubali, kwenye masuala ya tiba, Mjerumani ni mwisho!. Sisi tunawakumbatia Wahindi kwa kupeleka wagonjwa wetu India, sio kwa sababu ya ubora wa tiba, ni kwa sababu ya cheap service na bakhshis kubwa kubwa kila anayewapeleka biashara.

Huyo Zitto ni mwanafunzi ujerumani kwahiyo kwa vyovyote ana haki ya matibabu bure kama sehemu ya scholarship yake.

Atakuwa anakwenda kuonana na walimu wake na pia kuangalia afya, ukweli ndio huo.
 
Lakini huwezi kuficha? kama anaenda kuangalia afya yake si aende kimyakimya, hata kama anatibiwa bure huko kwa sababu ni mwanafunzi, lakini kuaga watu na kusema unaenda kutibiwa kunaleta picha ya tofauti!

Kwa level yetu ya maendeleo, kiongozi yeyote should avoid using those languages! ina maana leo wagonjwa wote mahospitalini wawe na wasiwas na mad!ktari wao! Akiwa rais itakuwaje? unless taarifa ya uongo, kama ya ukweli personally naona ni KOSA KUBWA! kwa kiongozi
 
Wagalatia mmezidi kwa kulalama.
Kila ndege hutua mti aupendao, mambo mengine ni kuingilia uhuru wa mtu husika. Mbona watu wengi tu m-mesoma nje ya nchi kwani hamkuona kuwa kuna vyuo ndani ya nchi ambavyo mgesoma?

Ipo siku nayo yaja kwamba Zitto atamuwa kufanya utalii ktk mbunga ya kilimanjaro, na wagalatia mtahoji kwanini aende kilimanjaro wakati huko kwao kigoma ipo mbuga ya gombe ambayo angetembelea angeonesha uzalendo kwa wananchi wa ma-gharibi.

Mimi nafikiri wengi wetu tunajihadi kujadili kwa kutumia kumbukumbu za nyuma na vizasasi binafsi, nafrikiri ingebidi kuwa na kisasi kwa maada iliyo mbele yako
 
Wagalatia mmezidi kwa kulalama.
Kila ndege hutua mti aupendao, mambo mengine ni kuingilia uhuru wa mtu husika. Mbona watu wengi tu m-mesoma nje ya nchi kwani hamkuona kuwa kuna vyuo ndani ya nchi ambavyo mgesoma?

Ipo siku nayo yaja kwamba Zitto atamuwa kufanya utalii ktk mbunga ya kilimanjaro, na wagalatia mtahoji kwanini aende kilimanjaro wakati huko kwao kigoma ipo mbuga ya gombe ambayo angetembelea angeonesha uzalendo kwa wananchi wa ma-gharibi.

Mimi nafikiri wengi wetu tunajihadi kujadili kwa kutumia kumbukumbu za nyuma na vizasasi binafsi, nafrikiri ingebidi kuwa na kisasi kwa maada iliyo mbele yako

Ndugu .... umenza kusoma hii thread katikati? Naomba urudie tena ...ni kwa nini Zitto (amesema?) anaenda (kutibiwa?) Ujerumani! Ni kwa sababu ndogo tu... ya uchovu! Sasa hapo ndipo maswali yanapoanzia! Kwa upande mwingine mimi sioni tatizo kubwa kwa yeye kuamua kwenda popote ila inabidi anapoongea na waandishi (kama inavyoonekana anapendelea-- hata kwa vitu visivyo na umuhimu) achague maneno yakuzungumza.....
 
Ndugu .... umenza kusoma hii thread katikati? Naomba urudie tena ...ni kwa nini Zitto (amesema?) anaenda (kutibiwa?) Ujerumani! Ni kwa sababu ndogo tu... ya uchovu! Sasa hapo ndipo maswali yanapoanzia! Kwa upande mwingine mimi sioni tatizo kubwa kwa yeye kuamua kwenda popote ila inabidi anapoongea na waandishi (kama inavyoonekana anapendelea-- hata kwa vitu visivyo na umuhimu) achague maneno yakuzungumza.....

Mkuu
Nimeisoma tangu mwanzo, hizo lugha za uchovu yawezekana ni lugha za kidiplomasia, mara ngapi umesikia mtu fulani maarufu ila yupo hoi lakini wanaporipoti wanasema hali yake imetengemaa.?

Cha kujiuliza zaidi je huo uchovu ndo ulimwewesesha mpaka dispesari?
Mimi nafikiri watanzania tumekuwa na mentality ya kijima iliyopitwa na wakati, kwamba eti kutumia cha kwatu hata kama ni kibovu kupitiliza basi ndo utaonekana mzalendo, muungwana na mtu wa watu.

Hii ni sawa na wanavijiji kule vijijini kwetu , ukienda kuwatembelea watakulazimisha ulale kwenye ngozi hata kama kitanda kizuri na godoro zuri vinapatikana, eti kwa kulala kwenye ngozi ndo kipimo chao kuwa wewe ni mtu wa watu.Kifupi hii tabia imepitwa na wakati ni tabia ya kijima zaidi nifikilivyo.Dunia ya leo inamtaka mtu kutumia na kujiamulia mambo yake bila kuingilia mipaka ya mwenzake.
 
Kama ilivyo ada kwa muungwana yeyote...namtakia afya njema Mh. Zitto, na Mungu amjaalie awe nuheri wa afya mapema iwezekanavyo arudi kwenye kwenye kulitumikia taifa.....baada ya hayo....

Hivi si juzi juzi tu Muhimbili walituonesha wodi za kisasa kabisa na Mh. Rais alipewa maelezo ya kutosha ya namna hata mgonjwa mahututi anavyoweza kupatiwa matibabu ya kimsingi akapota hapa hapa kwetu???....kama jibu ni ndio sas kuna uhitaji gani wa kufungashana mpaka ughaibuni kwa matibabu??????

Pili kwa kitendo cha kila itokeapo kiongozi kuugua anakimbizwa nnje ya nnchi ni wazi viongozi wetu ki vitendo wanakubali kuwa hospitali wanazo watengenezea wa Tanzania ni za kiwango duni....na kama ni hivyo basi hawastahili kukalia viti vya bunge kwani watakuwa wameshafeli kile tunachotazamia toka kwao yaani kutupatia maisha bora zikiwemo hospitali bora...

Tatu Mh. Zitto ameptwa na maumivu ya kichwa kutokana na uchovu kapelekwa ughaibuni vipi kuhusu watanzania wa kawaida ka mie mvuja jasho ambao kila siku tunarudi kwenye vijinyumba vyetu tukiwa na maumivu ya mgongo,viuno, vichwa, miguu,shingo, vipanda uso n.k. kutokana na shulba za kubeaba zege, jembe, kugonga kokoto, kusukuma mkokoteni n.k...fungu letu la kutupeleka ughaibuni kwa matibabu likwapi????

Mi naamini huu uwe mfano kwa mh. Ziito pindi atakaporudi,awahimize wenzake pale mjengoni Dodoma zile hela za nyongeza za mishahara yao na mashangingi zipelekwe kwenye mfuko maalumu wa kuboresha hospitali zetu ili ikitokea MBUNGE AKAPTA MAUMIVU YA KIUNGULIA AU TUMBO LA KUHARA KUSIWE NA HAJA YA KUPELEKANA INDIA KWA MATIBABU!!!!!!!

Sayonara!!!!!!!
 
Kama ilivyo ada kwa muungwana yeyote...namtakia afya njema Mh. Zitto, na Mungu amjaalie awe nuheri wa afya mapema iwezekanavyo arudi kwenye kwenye kulitumikia taifa.....baada ya hayo....

Hivi si juzi juzi tu Muhimbili walituonesha wodi za kisasa kabisa na Mh. Rais alipewa maelezo ya kutosha ya namna hata mgonjwa mahututi anavyoweza kupatiwa matibabu ya kimsingi akapota hapa hapa kwetu???....kama jibu ni ndio sas kuna uhitaji gani wa kufungashana mpaka ughaibuni kwa matibabu??????

Pili kwa kitendo cha kila itokeapo kiongozi kuugua anakimbizwa nnje ya nnchi ni wazi viongozi wetu ki vitendo wanakubali kuwa hospitali wanazo watengenezea wa Tanzania ni za kiwango duni....na kama ni hivyo basi hawastahili kukalia viti vya bunge kwani watakuwa wameshafeli kile tunachotazamia toka kwao yaani kutupatia maisha bora zikiwemo hospitali bora...

Tatu Mh. Zitto ameptwa na maumivu ya kichwa kutokana na uchovu kapelekwa ughaibuni vipi kuhusu watanzania wa kawaida ka mie mvuja jasho ambao kila siku tunarudi kwenye vijinyumba vyetu tukiwa na maumivu ya mgongo,viuno, vichwa, miguu,shingo, vipanda uso n.k. kutokana na shulba za kubeaba zege, jembe, kugonga kokoto, kusukuma mkokoteni n.k...fungu letu la kutupeleka ughaibuni kwa matibabu likwapi????

Mi naamini huu uwe mfano kwa mh. Ziito pindi atakaporudi,awahimize wenzake pale mjengoni Dodoma zile hela za nyongeza za mishahara yao na mashangingi zipelekwe kwenye mfuko maalumu wa kuboresha hospitali zetu ili ikitokea MBUNGE AKAPTA MAUMIVU YA KIUNGULIA AU TUMBO LA KUHARA KUSIWE NA HAJA YA KUPELEKANA INDIA KWA MATIBABU!!!!!!!

Sayonara!!!!!!!

Kwanini uone hospitali tu kwamba ndo kipimo cha uzalendo na uache mambo mengine kama shule?
 
aibuuuuuuuuuuuuuuuu...........hatuna wanasiasa....wizi mtupu
 
Ugua pole Zito mengine tutaulizana ukisharudi ukiwa mzima. Mungu akulinde na kukutia nguvu.
Walalahoi hawawezi zuia hiyo safari yake, lakini kama ni kweli hiyo safari ipo na kuaaanalipiwa na pesa ya walala hoi sioni kwa nini asiishie huko huko maana si kweli kua anatetea maslahi ya walalahoi. Kuulizana baadaye kuhusu ufisasi ktk TZ hii wala hua hamna ufanisi wowote.
 
Mkuu
Nimeisoma tangu mwanzo, hizo lugha za uchovu yawezekana ni lugha za kidiplomasia, mara ngapi umesikia mtu fulani maarufu ila yupo hoi lakini wanaporipoti wanasema hali yake imetengemaa.?

Cha kujiuliza zaidi je huo uchovu ndo ulimwewesesha mpaka dispesari?
Mimi nafikiri watanzania tumekuwa na mentality ya kijima iliyopitwa na wakati, kwamba eti kutumia cha kwatu hata kama ni kibovu kupitiliza basi ndo utaonekana mzalendo, muungwana na mtu wa watu.

Hii ni sawa na wanavijiji kule vijijini kwetu , ukienda kuwatembelea watakulazimisha ulale kwenye ngozi hata kama kitanda kizuri na godoro zuri vinapatikana, eti kwa kulala kwenye ngozi ndo kipimo chao kuwa wewe ni mtu wa watu.Kifupi hii tabia imepitwa na wakati ni tabia ya kijima zaidi nifikilivyo.Dunia ya leo inamtaka mtu kutumia na kujiamulia mambo yake bila kuingilia mipaka ya mwenzake.

Wengi tunadhani analipiwa na pesa ya umma kama sivyo si angesema tu, la sivyo ana uhuru wa kwenda kokote kwa kujigharimia.
 
Kwa umri wake Zitto na mafanikio aliyopata kimaisha mbwembwe hizi na nyinginezo haziepukiki. Binafsi nahusudu sana baadhi ya michango yake Bungeni. Anazidi tu kupoteza mguso wake kwa jamii ya Watanzania wa kawaida. Hatibiwi pamoja nao, hali nao, hakai na kuongea nao na hivyo hatajua matatizo na shida zao za kila siku.
 
Sioni tatizo kwa Zitto kwenda anakohisi anaweza kupata huduma stahili hasa ukizingatia mazingira ya sasa ambapo umezembea mwananyamla unapelekwa zahanati ya Bunge. Lakini pia tujiulize kwa nini anaenda Ujerumani kama vile wewe umetoka Dar unaenda Mtwara, na si pengine? Amejisikia vibaya leo kesho kaamua akachunguzwe huko. I understand that visa could not be a problem but flight and his personal plans can help us. Ila huenda hakuzungumza hivyo..... tusubiri upande wa pili kama mjadala huu unatija, otherwise haya ndo maisha kwenye ulimwengu huu wetu, haina haja kujadili wakati kila kitu kipo wazi.
 
siasa za tanzania haziwezi kufanana na nchi za nje .....hatujafika huko jamani! waacheni kina zitto wajitangaze wanaenda kutibiwa kipele Marekani pia, uelewa wa wananchi unawaruhusu kufanya hivyo.

wabunge tanzania wana watoto out of wedlock ......hakuna tatizo ( ingekuwa ulaya, angepata tabu kuwa mbunge au kuendelea na ubunge wake ( kama amepata akiwa mbunge)


wabunge wengi sana wana nyumba ndogo.....................but wananchi hatujali.

wabunge wengi ni mafisadi even.....................na wananchi hawajali wanawachagua hao kwa hao

sioni sababu ya kupiga kelele hili, la mtu kutumia pesa zake kwenda hospitali ujerumani........hakutomnyima kura.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom