Zitto aenda kutibiwa Ujerumani

Zak Malang

JF-Expert Member
Dec 30, 2008
5,404
233
Zitto aenda kutibiwa Ujerumani

Mbunge wa Kigoma Kaskazini kwa tiketi ya Chadema, Zitto Kabwe, amekwenda Ujerumani kwa ajili ya matibabu baada ya kuzidiwa mwishoni mwa wiki akiwa bungeni mkoani Dodoma.

Akizungumza na Nipashe jana akiwa Uwanja wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere, Zitto alisema atakaa nchini Ujerumani akiangaliwa afya yake kwa muda wa wiki moja.

Alisema hayuko katika hali mbaya sana na kwamba anasumbuliwa na uchovu wa kawaida tu, hivyo anaenda kwa ajili ya uchunguzi zaidi wa afya yake.

“Naumwa kidogo tu, hapa niko Airport naenda Ujerumani leo… Siumwi saana.. Hii ni fatigue tu,” alisema Zitto pia ni Naibu Katibu Mkuu wa Chadema katika ujumbe wake kwa mwandishi wa habari hizi.

Zitto aliugua ghafla juzi jioni ikiwa ni muda mfupi baada ya Bunge kupitisha muswada wa Sheria ya Madini.

Zitto (34) alipelekwa kwenye zahanati ya Bunge baada ya mjadala wa muswada wa madini ambapo alichukuliwa vipimo na kuruhusiwa kuondoka.

Waliomshuhudia Zitto akitoka ndani ya ukumbi wa Bunge walisema kuwa walimsikia akilalamika kuwa anasikia maumivu ya kichwa.

Akiwa nje ya ukumbi, Zitto alisalimiana na baadhi ya wabunge lakini baada ya muda alionekana akipepesuka na aliomba msaada kwa waandishi waliokuwa jirani naye ambao walimpeleka kwenye zahanati ya Bunge ambako alitibiwa.

CHANZO: Nipashe
 
POLE SANA ZITTO...

Mungu unaemwamini na akujaaalie afya njema, haraka iwezekanavyo!

Lakini fatique tu ndo ukatibiwe Ujerumani!!...huh!
Ubunge raha bana, acheni watu wausake kwa udi na uvumba!
 
Zitto aenda kutibiwa Ujerumani

Mbunge wa Kigoma Kaskazini kwa tiketi ya Chadema, Zitto Kabwe.
Mbunge wa Kigoma Kaskazini kwa tiketi ya Chadema, Zitto Kabwe, amekwenda Ujerumani kwa ajili ya matibabu baada ya kuzidiwa mwishoni mwa wiki akiwa bungeni mkoani Dodoma.

Akizungumza na Nipashe jana akiwa Uwanja wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere, Zitto alisema atakaa nchini Ujerumani akiangaliwa afya yake kwa muda wa wiki moja.

Alisema hayuko katika hali mbaya sana na kwamba anasumbuliwa na uchovu wa kawaida tu, hivyo anaenda kwa ajili ya uchunguzi zaidi wa afya yake.

"Naumwa kidogo tu, hapa niko Airport naenda Ujerumani leo… Siumwi saana.. Hii ni fatigue tu," alisema Zitto pia ni Naibu Katibu Mkuu wa Chadema katika ujumbe wake kwa mwandishi wa habari hizi.

Zitto aliugua ghafla juzi jioni ikiwa ni muda mfupi baada ya Bunge kupitisha muswada wa Sheria ya Madini.

Zitto (34) alipelekwa kwenye zahanati ya Bunge baada ya mjadala wa muswada wa madini ambapo alichukuliwa vipimo na kuruhusiwa kuondoka.

Waliomshuhudia Zitto akitoka ndani ya ukumbi wa Bunge walisema kuwa walimsikia akilalamika kuwa anasikia maumivu ya kichwa.

Akiwa nje ya ukumbi, Zitto alisalimiana na baadhi ya wabunge lakini baada ya muda alionekana akipepesuka na aliomba msaada kwa waandishi waliokuwa jirani naye ambao walimpeleka kwenye zahanati ya Bunge ambako alitibiwa.




CHANZO: Nipashe



Huyu mwanasiasa, anayesemekana ni 'mtu wa watu' na even 'future presidential material' vipi? Fatigue kidogo tu inampeleka Ujerumani 'kuangaliwa' kwa wiki moja? nani analipia mchezo huu?

Hivi hizi hospitali za 'walalaho' ambao inasemekana wanampenda na kumtetea hazina hadhi kabisa kuchunguza kuumwa kwake kidogo?i

Vipi akika kuwa president?
 
Ni mdogo mno inabidi acheki hiyo afya kwa kina aanze tiba mapema,tusipoutumia ujana.umaarufu na pesa zetu kwa busara hakika hatutafika!.pole sana kabwe.
 
keshafika umri wa kutibiwa! mmh .....afrika hasa maisha yetu ni mafupi
 
Tunamwombea M/mungu amsaidie apate nafuu haraka, taifa bado linamuhitaji.
Miaka 3 iliyopita kulikuwa na mjadala mrefu hapa ukumbini na wengi wetu yalituletea wasiwasi, tutaendelea kufuatilia hali ya siha yako.

Ugua pole Mh. Zitto!
 
Kwa maoni yangu, safari ya Ujerumani ilikuwa imepangwa kabla. Haiwezekani mtu ajisikie vibaya Alhamisi, atibiwe zahanati a Bunge, Ijumaa aje Dar, Jumamosi huyoo Ujerumani.
Taratibu za kutibiwa nje ya nchi ni ndefu unless it is real emergence. Mhe. Zitto hakuwa na dharura ya kuhivyo kukimbizwa hospitalini Ujerumani, ila kwa vile safari ilikuwepo, na amejisikia uchovu, akaamua ngoja tuu akachunguzwe huko huko.

Kitu ambacho lazima tukubali, kwenye masuala ya tiba, Mjerumani ni mwisho!. Sisi tunawakumbatia Wahindi kwa kupeleka wagonjwa wetu India, sio kwa sababu ya ubora wa tiba, ni kwa sababu ya cheap service na bakhshis kubwa kubwa kila anayewapeleka biashara.
 
Kwa maoni yangu, safari ya Ujerumani ilikuwa imepangwa kabla. Haiwezekani mtu ajisikie vibaya Alhamisi, atibiwe zahanati a Bunge, Ijumaa aje Dar, Jumamosi huyoo Ujerumani.
Taratibu za kutibiwa nje ya nchi ni ndefu unless it is real emergence. Mhe. Zitto hakuwa na dharura ya kuhivyo kukimbizwa hospitalini Ujerumani, ila kwa vile safari ilikuwepo, na amejisikia uchovu, akaamua ngoja tuu akachunguzwe huko huko.

Kitu ambacho lazima tukubali, kwenye masuala ya tiba, Mjerumani ni mwisho!. Sisi tunawakumbatia Wahindi kwa kupeleka wagonjwa wetu India, sio kwa sababu ya ubora wa tiba, ni kwa sababu ya cheap service na bakhshis kubwa kubwa kila anayewapeleka biashara.

Mkuu Pasco, Unachosema kwa kiasi kikubwa kina mantiki. Naamini mwandishi wa hiyo habari ama Zitto mwenyewe ameamua kuipotosha. Binafsi siamini kama mtu anaweza kwenda nje ya nchi kwa fatigue tu!
 
Tunamwombea M/mungu amsaidie apate nafuu haraka, taifa bado linamuhitaji.
Miaka 3 iliyopita kulikuwa na mjadala mrefu hapa ukumbini na wengi wetu yalituletea wasiwasi, tutaendelea kufuatilia hali ya siha yako.

Ugua pole Mh. Zitto!


Mkuu,

Unataka kuunganisha hali ya Afya ya ndugu zitto na mjadala uliyohusu uhusiano wake na Amina Chifupa...mkuu sitaki kushawishika kuamini kwamba umeamua kujikita katika mijadala inayoelekea kujenga hisia potofu

Kwenye Hoja sasa,

Ndugu Zitto,Get well soon

Hata hivyo kweli Taifa limedidimia kiafya namna hii kiasi kwamba hata Fatigue inakua issue ya Germany?Anyway,hata baba wa Taifa letu aliyewatimua waingereza na kuongoza malengo mapana ya kulikuza taifa hili kiuchumi na kijamii alienda kuchekiwa St.Thomas,Uk

 
Zitto aenda kutibiwa Ujerumani

Mbunge wa Kigoma Kaskazini kwa tiketi ya Chadema, Zitto Kabwe.
Mbunge wa Kigoma Kaskazini kwa tiketi ya Chadema, Zitto Kabwe, amekwenda Ujerumani kwa ajili ya matibabu baada ya kuzidiwa mwishoni mwa wiki akiwa bungeni mkoani Dodoma.

Akizungumza na Nipashe jana akiwa Uwanja wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere, Zitto alisema atakaa nchini Ujerumani akiangaliwa afya yake kwa muda wa wiki moja.

Alisema hayuko katika hali mbaya sana na kwamba anasumbuliwa na uchovu wa kawaida tu, hivyo anaenda kwa ajili ya uchunguzi zaidi wa afya yake.

“Naumwa kidogo tu, hapa niko Airport naenda Ujerumani leo… Siumwi saana.. Hii ni fatigue tu,” alisema Zitto pia ni Naibu Katibu Mkuu wa Chadema katika ujumbe wake kwa mwandishi wa habari hizi.

Zitto aliugua ghafla juzi jioni ikiwa ni muda mfupi baada ya Bunge kupitisha muswada wa Sheria ya Madini.

Zitto (34) alipelekwa kwenye zahanati ya Bunge baada ya mjadala wa muswada wa madini ambapo alichukuliwa vipimo na kuruhusiwa kuondoka.

Waliomshuhudia Zitto akitoka ndani ya ukumbi wa Bunge walisema kuwa walimsikia akilalamika kuwa anasikia maumivu ya kichwa.

Akiwa nje ya ukumbi, Zitto alisalimiana na baadhi ya wabunge lakini baada ya muda alionekana akipepesuka na aliomba msaada kwa waandishi waliokuwa jirani naye ambao walimpeleka kwenye zahanati ya Bunge ambako alitibiwa.




CHANZO: Nipashe

Wakuu U-TURN Imegeuka kuwa vituko tupu http://u-turn-umbea.blogspot.com/
 
fisadi original hiyo ya umbea hujaifungua wewe lakini!....maana umeijua haraka.

watu wakiwa hawakupendi tanzania tabu kweli kweli ......mpaka wanaiga blog yako na ku copy picha zooooote! mmh


hivi bunge limemaliza kikao? au zitto kenda kupumzika fatigue wakati bunge linaendelea?
 
Mkuu,

Unataka kuunganisha hali ya Afya ya ndugu zitto na mjadala uliyohusu uhusiano wake na Amina Chifupa...mkuu sitaki kushawishika kuamini kwamba umeamua kujikita katika mijadala inayoelekea kujenga hisia potofu

Kwenye Hoja sasa,

Ndugu Zitto,Get well soon

Hata hivyo kweli Taifa limedidimia kiafya namna hii kiasi kwamba hata Fatigue inakua issue ya Germany?Anyway,hata baba wa Taifa letu aliyewatimua waingereza na kuongoza malengo mapana ya kulikuza taifa hili kiuchumi na kijamii alienda kuchekiwa St.Thomas,Uk
Broda Ben, naona kama umeanza vizuri sana mpangilio wa hoja zako, lakini hapo kwenye red hapajatulia! Mzee JKN alienda kutibiwa broda, si kuchekiwa!...huoni ugonjwa wake ukawa serious hadi kumnyoosha?
 
Ugua pole Zito mengine tutaulizana ukisharudi ukiwa mzima. Mungu akulinde na kukutia nguvu.
 
Huyo jamaa naye kizunguzungu, ukimuangalia amebakiza kichwa tu na mdomo wa kuzungumza, anaishi na stress nyingi sana huyo bwana mdogo, anakunywa sana pombe na demu wake yule, yaani kiufupi ni kama amepoteza muelekeo, Pale mara nyingi Zoungh garden yaani anajidhalilisha, wewe kijana mdogo mijipombe isiyo ya lazima yanini yarabi?
Ameo ka sister do sasa kanampeleka hakuna hata maadili kamebakia jina tu ni katotorial asistant pale UD japo kwa ufinyu wa walimu nako kanaitwa lecturer.
Kijana mwenzetu hajapata mke mwema!!
Taabu kabisa sasa afya mgogoro mara misuada hiyo.
Shwine kabisa kabisa
 
Huyu Bwana alikuwa anasoma Masters kinyemela!Sasa hiyo trip ya Germany,may be ni kupeleka Phd proposal.Niliandika sana kuhusu elimu ya huyu Bwana na hicho chuo chake,lakini hapa JF watu walinipinga sana!
Eti unaenda kutibiwa Germany na kupumzika!Oh my God.
Unaweza kudanganya nyani ,sio watu wenye akili
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom