Zitto aahidiwa kupewa ulinzi na chama cha ACT

Zitto aahidiwa kupewa ulinzi na chama cha ACT

Chama Alliance for Change and Transparency mkoani Kigoma kimeahidi kumwekea Ulinzi Zitto Kabwe dhidi ya wabaya wake kisiasa. Pia ameombwa afute kesi ya CHADEMA ili aendelee na harakati za ACT
Source : Mtanzania, Nipashe...
My : Lililosemwa kuwa Zitto alishajiandalia chama na wasaliti wenzake kwa msaada wa CCM linazidi kujidhihirisha na kutimia.
Kumbe ACT ni chama cha ulinzi?
 
Ha ha haa ulinzi wa nini tena wakati alisema ana ulinzi wakutosha kuwa atakayemgusa kwao hatasalia hata panya.
 
Masikini Zitto, haya ni maandalizi ya kupotezwa na TISS ili waipakazie CHADEMA kesi yake.....he will go the Wangwe way
 
Kwani simiyu yetu ni mumeo?

Ndg mmehama mada!

Matusi hayajengi badala yake yanawabomoa na kuwaonesha jinsi mlivyo. Jitahidini kutumia lugha za kidiplomasia mkijikita kwenye ujenzi wa hoja. Suala la ZZK lisiwatenge na kuwafanya muwe maadui. Si ACT wala CDM hawawezi kwa sasa kuichukua Ikulu bado CCM ina nafasi kubwa sasa msipoteze muda mwingi kuchonga matusi.
 
Chama Alliance for Change and Transparency mkoani Kigoma kimeahidi kumwekea Ulinzi Zitto Kabwe dhidi ya wabaya wake kisiasa. Pia ameombwa afute kesi ya CHADEMA ili aendelee na harakati za ACT
Source : Mtanzania, Nipashe...
My : Lililosemwa kuwa Zitto alishajiandalia chama na wasaliti wenzake kwa msaada wa CCM linazidi kujidhihirisha na kutimia.
Kwa nini awekewe ulinzi na Alliance for Change and Transparency badala ya CHADEMA ama zito ameshakihama chama jumla?
 
sasa aende akawe mwenyekiti wa ACT milele, kuitoa kesi mahakamani hawezi, maana ndio jimbo lake.
 
Masikini Zitto, haya ni maandalizi ya kupotezwa na TISS ili waipakazie CHADEMA kesi yake.....he will go the Wangwe way


Absolutly Kamanda!! Either Zitto or Mchange will face the "way'!! Then Mnyika or Lisu will kept in custod...!!
 
kwa kuwa Think Tank ya ACT ndo huyo Mchange tutegemee kusikia vituko vingi mno kutoka katika chama hiki.
 
CHAMA cha Alliance Transparency For Change (ACT) Mkoa wa Kigoma, kimeahidi kumlinda na kumtetea Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Bw. Zitto Kabwe (CHADEMA), kutokana na changamoto zinazomkumba kupitia watu wachache wanaotaka kumwangusha kisiasa.

Mjumbe wa Kamati Kuu Taifa ya chama hicho, Bw. Jaffar Kasisiko, aliyasema hayo juzi katika mkutano wa hadhara uliofanyika Viwanja vya Cine Atlas, kwenye Manispaa ya Kigoma Ujiji.

Alisema chama hicho hakipo tayari kuyafumbia macho matatizo yanayomkuta Bw. Kabwe na kumshauri mbunge huyo aachane na CHADEMA badala yake ajiunge na ACT ili aweze kukusanya wanachama kuanzia ngazi ya kitongoji, vijiji, kata na wilaya.

Aliongeza kuwa, uongozi wa CHADEMA una hila ya kusambaza maneno kwa umma dhidi ya Bw. Kabwe ili kulinda masilahi yao binafsi badala ya kutetea haki za wanyonge.

"Kabwe asipoteze muda wa kulumbana na uongozi wa CHADEMA, huu ni wakati mwafaka kwake kufanya uamuzi makini wa kwenda kuifuta kesi dhidi ya chama chake mahakamani na kujiunga na ACT," alisema Mjumbe wa Halmashauri Kuu Taifa, Msafiri Wamalwa.

Katibu Mwenezi Wilaya ya Kigoma kutoka chama hicho, Anzoluni Kibela, alisema ACT imeandaa kadi kwa ajili ya Bw. Kabwe ambapo kuna wabunge 18 wapo tayari kujiunga na chama hicho kwenye uzinduzi rasmi ulipangwa kufanyika mwanzoni mwa Septemba mwaka huu.

Naye Kaimu Mwenyekiti wa chama hicho Taifa, Bw. Shaban Mambo, aliwasihi wananchi wamuunge mkono Bw. Kabwe atakapojiunga na chama hicho ili aboreshe hali ya usafiri wa reli ya kati kwa kuwaletea treni inayotumia umeme kwa gharama zake.

Baadhi ya wanachama wapya wa ACT akiwemo aliyekuwa Mweka Hazina wa CHADEMA Kigoma Ujiji, Bw. Hamidu Hamis na Katibu wa ACT wilayani humo, Bw. Haji Idd, walisema wamejiunga na chama hicho ili kuleta uwazi uwajibikaji.

CHANZO: Majira
 
Huyu jamaa ni bora akafundishe tu, kashajimaliza kisiasa!! hakujifunza vizuri namna CCM inavyowamalizaga wanasiasa wenye njaa njaa? amuulize baba yake mdogo DR. Kaburu

Akafundishe ana Ji Pi Ei? au ndo ukurupukaji tu kama wa Majina ya Pesa ya Uswisi kumbe hana jina hata moja......Awaulize TCU sifa za kufundisha.....
 
Jakaya mwenyewe anatembea na msururu wa magari kwaajili ya kutafuta umaarufu siyo kwaajili ya ulinzi. Hakuna mwenye muda wa kumdhuru Rais Kikwete, sasa ni nani atakayefikiria kumdhuru Zito? Zito ana nini cha pekee hata kuhitaji ulinzi? Labda kama aliwahi kudhulumu, basi hapo kweli utahitajika ulinzi, ingawa mimi naamini kuwa ulinzi wa kweli hutoka kwa Mungu.
 
Back
Top Bottom