Zitto aahidiwa kupewa ulinzi na chama cha ACT

Zitto aahidiwa kupewa ulinzi na chama cha ACT

Kama kuna mtu wa kumdhuru Zito, lazima itakuwa ni CCM, na siyo mtu mwingine yeyote. Maana kanuni za ujasusi zinafahamika, ukishatumika katika mipango ovu, ili kuwa na uhakika kuwa uovu huo hautawekwa wazi siku moja, wale waliotumika ni lazima wapotezwe. Hili Zito, Mchange, Juliana, wanastahili kulitambua.

Zito kweli ni kisiki cha mpingo.
 
Chama Alliance for Change and Transparency mkoani Kigoma kimeahidi kumwekea Ulinzi Zitto Kabwe dhidi ya wabaya wake kisiasa. Pia ameombwa afute kesi ya CHADEMA ili aendelee na harakati za ACT
Source : Mtanzania, Nipashe...
My : Lililosemwa kuwa Zitto alishajiandalia chama na wasaliti wenzake kwa msaada wa CCM linazidi kujidhihirisha na kutimia.
Yaani we bado unamuwaza Zitto tu.
 


"Kabwe asipoteze muda wa kulumbana na uongozi wa CHADEMA, huu ni wakati mwafaka kwake kufanya uamuzi makini wa kwenda kuifuta kesi dhidi ya chama chake mahakamani na kujiunga na ACT," alisema Mjumbe wa Halmashauri Kuu Taifa, Msafiri Wamalwa.

Mwenzenu anaangalia maslahi kwanza, kuna uwenyekiti wa PAC amuachie nani?, kuna kinuamgongo cha ubunge mamillion ya Shillingi amwachie nani?, mwenzenu yupo kifedha zaidi, kama mlikuwa hamjui basi litamueni hilo.
 
Mkuu, mbona umehamaki sana? Simiyu Yetu kakugusa penyewe nini? Rudia kusoma ulichoandika halafu ujione jinsi ulivyo mjinga
Kumbe hata lofa kama wewe anaweza kung'amua mjinga na asiye mjinga?
 
Naye Kaimu Mwenyekiti wa chama hicho Taifa, Bw. Shaban Mambo, aliwasihi wananchi wamuunge mkono Bw. Kabwe atakapojiunga na chama hicho ili aboreshe hali ya usafiri wa reli ya kati kwa kuwaletea treni inayotumia umeme kwa gharama zake.

Hahahah....siasa za Tanzania bana, hivi sijui huwa mnawezaje kuwaita watu wenye mawazo kama haya ni viongozi!!!
 
Basi jamaa ZZK amelamba bingo ndefu kutpka CCM km ana uwezo wa kujenga reli ya train za umeme toka Dar mpaka Kigoma....oh maskini Watanzania, bendera kufuata upepo
 
Yale yale ya kupewa ulinzi wa MARUHANI kama aliopewa mkulu na shehe yahaya! Teh teh teh teh
 
Ha ha haa ulinzi wa nini tena wakati alisema ana ulinzi wakutosha kuwa atakayemgusa kwao hatasalia hata panya.

teh teh! unafikiri Zitto ni rahis kukata kama tikitimaji! muulize Ben saa8, katembea sana na dum la lita 10 la su.m kumuwinda Zitto lakin kashindwa ameambulia kuumuka kifua ni mikono kama John Cena kutokana na mzigo mzito alokua akibeba kutwa nzima! Hata MAGAMBA wanajua, Zitto akitegeshewa ajali ya semi anaingia mwingine na Mkigoma wetu Zitto atakua wa kwanza kushuhudia ajali. Hahahahaaaaa! angetafutwa Lema kama anavyowindwa Zitto, yule mchaga tungekua tushamsahau kabsa.
 
Yaani unaweza kuona baadhi ya Wanasiasa walivyo IGNORANT! Huyu anayemtaka Zitto na wabunge wengine 8 waingie ACT September 2014 atawalipa mafao yao? Hakumbuki yaliyompata Mpendazoe 2010? Kwa mujibu wa Sheria ukijiondoa au kufukuzwa kwenye chama ulikopatia ubunge/udiwani na UBUNGE wako bye bye. Ndio maana Zitto na Rashi Hamad wako mahakamani. Waondoke kabla ya Bunge kuvunjwa alafu wakale wapi?
 
Hahahah....siasa za Tanzania bana, hivi sijui huwa mnawezaje kuwaita watu wenye mawazo kama haya ni viongozi!!!

Mkuu watu8 asante kwa msaada wako hapo kwenye red, maana nilikuwa nasoma kwa kuluka matuta. Nafikiri kila mtu akipaona hapo kwenye red lazima ashangae.
 
Last edited by a moderator:
kazi kweli kweli,mnafikiri kuanzisha chama ni kama kwenda kufungua akaunti banka unaambiwa njoo na wathamini wawili?
 
Naye Kaimu Mwenyekiti wa chama hicho Taifa, Bw. Shaban Mambo, aliwasihi wananchi wamuunge mkono Bw. Kabwe atakapojiunga na chama hicho ili aboreshe hali ya usafiri wa reli ya kati kwa kuwaletea treni inayotumia umeme kwa gharama zake. Hii hapa ndo imeniacha hoi
 
tukutane 2015...kelele za nini ?bado mapema mno..ACT kazeni buti sana sizani kama mtambulia mbunge hata mmoja
 
Zitto ajiunge tu rasmi na ACT yake sio kukiendesha kwa remote.
 
Mwisho wa kutumika kwa zzk, mchange na wasaliti wengine ni 2015, kama kuna kitu cha maana wameahidiwa wachukue mapema sidhani kama kuna rais atakae kubali huu upuuzi wa kusadikika unaoendeshwa sasa hivi na CCM uendelee, mwisho wa dhaifu kutawala ndio mwisho wa madhaifu tunayoyaona. Upuuzi umetawala kila sekta, mpaka polisi wameshindwa kufanya kazi na manasiasa uchwara? mwisho 2015 wachukue chao mapemaaa.
 
Back
Top Bottom