Exaud Mamuya
JF-Expert Member
- Jul 26, 2011
- 403
- 242
Yaani swala hili halijakukera wewe tu Ila Watanzania wote hata wale wasio wanachama wa Chadema. Napenda nichukue fursa hii kukupongeza sana kamanda Zitto kwa kuvunja ukimya na kuamua kuweka kila kitu wazi juu ya fununu zilizokuwepo juu ya kugombea nafasi ya kuwa kiongozi mkuu wa Taifa letu Tanzania, yaani nafasi ya Urais. Hongera sana brother kwa hatua uliyoifikia maana wasiokitakia mema chama chetu walitegemea ndo itakuwa mwanzo wa mpasuko wa chama na kufarakana kwa viongozi wakuu wa chama. Narudia Tena Hongera sana kwa kufanya maamuzi magumu na yenye tija kwa chama na Taifa kwa ujumla wake.