Zimbabwe kununua Korosho za Tanzania

Zimbabwe kununua Korosho za Tanzania

esther mashiker

JF-Expert Member
Joined
May 29, 2018
Posts
616
Reaction score
555
1114168

Baada ya Zimbabwe kuonyesha nia ya kununua mahindi na mazao mengine kiasi cha 800,000 kutoka Tanzania, taifa hilo la Kusini mwa Afrika linafikiria pia kuanza kununua mazao mengine kama korosho.

Ujumbe kutoka Serikali ya Zimbabwe utawasili nchini kuanzia siku ya Jumanne ya Tarehe 3 Juni na unatajiwa kuwa nchini mpaka tarehe 7 ya Mwezi Juni.

“Ujumbe huo unakuja kwa ajili ya kuangalia na kujiridhisha kuhusu mambo ya msingi kama ubora wa chakula na mambo mengine ya awali,” Waziri wa Kilimo Japhet Hasunga ameyasima hayo jana wakati wa kikao cha dharura na wakurugenzi wa taasisi na idara mbalimbali za Wizara ya Kilimo.

“Zimbabwe imefikiria pia kuanza kununua mazao mengine kama korosho kwa kuwa imeona fursa ya kupata mazao yenye ubora na kwa bei nzuri ipo Tanzania. Baadae mazao mengine ya mbegu za mafuta, jamii ya mikunde, mboga na matunda yataanza kununuliwa na taifa hilo,” aliongeza Waziri Hasunga.

Kikao hicho kilikuwa na lengo la kuanza kutekeleza agizo la Rais Magufuli la kuiuzia nchi ya Zimbabwe mahindi na mazao mengine kiasi cha Tani 800,000.
 
Zimbabwe wanunue korosho wazipeleke wapi?kweli tunamawaziri wapuuzi kweli ambao hawajui hata wafanye nini.
Yaani muda wote wanakaa ofsini kujadili ZIM watanunua korosho kweli hii serikali iko mbioni kuanguka tena bila kusukumwa.
 
Pole pole leo kasema tutagawana korosho zetu endapo hazitauzika...... Naomba Zimbabwe washindwe heri tupewe kg mbili zetu kila mmoja
 
Back
Top Bottom