Zimbabwe kununua Korosho za Tanzania

Zimbabwe kununua Korosho za Tanzania

KOROSHO+PIC.jpg
Waziri wa Viwanda na Biashara, Joseph Kakunda akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma leo. Picha na Ericky Boniphace

https://www.mwananchi.co.tz › ...
Kampuni sita zasaini mkataba wa awali kununua korosho nchini Tanzania ...

16 May 2019 · Serikali imesaini mkataba wa awali na kampuni sita ya kununua korosho kati ya zilizoomba kununua
Leo 01.06. 2019
Hapo ina maana kuwa habari ya kampuni sita zilizotia saini hivi karibuni nazo zimeshindwana na serikali kiasi ya kutafuta soko Zimbabwe la korosho?
 
Kuna uzi ukisoma kuna hatari kubwa ya kupatwa na maradhi ya upunguani.Ewe mola tulinde waja wako
 
Hii nchi imekufa kifo cha mende yaani watu wanawaza kusifia nyayo za mkulu hata kufikiria no!
Vuta subira kidogo mkuu, hakuna haja ya kuwa na haraka kulaumu.

Kama hayo yaliyoandikwa hapo juu yatakuwa ya kweli, basi sote tutashukuru bila kujali nani kayaleta na nchi yetu ikafaidika kwa matokeo hayo. Kama ni sifa, basi, kwa nini tuwanyime sifa wanapofanya mazuri ya kuneemesha nchi yetu. Lakini hata tukisifu, hatuwezi kamwe kusahau mabaya waliyotenda na wanaendelea kulifanyia taifa.

Mimi sijui kwa nini Zimbabwe watake sana kununua korosho ya Tanzania wakati huu; au ni kwa vile wametembelewa?
Hata sijui uzoefu wa Zimbabwe na zao la Korosho. Wana viwanda vya kubangua korosho? Zimbabwe kuna soko kubwa la korosho, au wananunua kuuza nje kama wale Wakenya!

Siku hizi hata mawaziri kuamini wanachosema imekuwa tabu tupu! Acha tusubiri.
 
Mmh hao wazimbabwe wanunue korosho? Mmh kwao petrol kwa lita wanauziwa elfu 7 tsh wana shida mpaka huko chini maana hata toilet paper hawana! Halafu kwani mazao kutoka south africa mmembiwa yana bei kubwa kuliko ya tz? Au mahindi ya zambia yana bei kunwa kuzidi yetu?
 
View attachment 1114168
Baada ya Zimbabwe kuonyesha nia ya kununua mahindi na mazao mengine kiasi cha 800,000 kutoka Tanzania, taifa hilo la Kusini mwa Afrika linafikiria pia kuanza kununua mazao mengine kama korosho.

Ujumbe kutoka Serikali ya Zimbabwe utawasili nchini kuanzia siku ya Jumanne ya Tarehe 3 Juni na unatajiwa kuwa nchini mpaka tarehe 7 ya Mwezi Juni.

“Ujumbe huo unakuja kwa ajili ya kuangalia na kujiridhisha kuhusu mambo ya msingi kama ubora wa chakula na mambo mengine ya awali,” Waziri wa Kilimo Japhet Hasunga ameyasima hayo jana wakati wa kikao cha dharura na wakurugenzi wa taasisi na idara mbalimbali za Wizara ya Kilimo.

“Zimbabwe imefikiria pia kuanza kununua mazao mengine kama korosho kwa kuwa imeona fursa ya kupata mazao yenye ubora na kwa bei nzuri ipo Tanzania. Baadae mazao mengine ya mbegu za mafuta, jamii ya mikunde, mboga na matunda yataanza kununuliwa na taifa hilo,” aliongeza Waziri Hasunga.

Kikao hicho kilikuwa na lengo la kuanza kutekeleza agizo la Rais Magufuli la kuiuzia nchi ya Zimbabwe mahindi na mazao mengine kiasi cha Tani 800,000.
Uongo at wirk
 
Hii nch ina bwebwe. Yan kukaa kikao tu et inakuja na conclusion.
 
Tuache masihara mtu hana uwezo wa kupata mahindi kwa ajili ya mlo apate uwezo wa kununua korosho?
Kilo ya korosho na mahindi kipi bei ya chini ?
 
Haya ni madhara ya nchi kuwa mikononi mwa watu wasiojitambua.
 
ni vyema kufanya biashara na nchi zenye rika letu, tunaweza kuwa na uhuru wa kuongea biashara na mazingira rafiki ya kibiashara, Zimbabwe tuwauzie Korosho Sembe mchele Ngano ya Bakhresa, mbaazi maharagwe Vitenge khanga samaki na bidhaa zozote rafiki. Tuangalie uwezekano wa CRDB EXIM bank kwenda kufungua matawi Zimbabwe na Namibia, ndege zetu ziweze kwenda Zimbabwe na Namibia, wanafunzi wa huko waje kusoma vyuo vikuu vyetu. Huu ni mwanzo mzuri wa kufungua fursa za kibiashara baina ya nchi za Africa.
Mkuu nakubaliana na unachokiongea mazao ya chakula hasa Mahindi,Mchele,mbaazi mihogo ,maharage na mengineyo kweli wanauhitaji mkubwa lakini kwa korosho mzee narudia tena kusema hizo ni kauli za kisiasa.

Serikali yetu imekwama wapi wazipeleke korosho ndiyo maana hawaishi komedi.
 
Sasa hao Zimbabwe wana viwanda vya kubangua hizo korosho?? Au ni madalali??
 
Kwa nini tusiwe na viwanda wenyewe?? Eti tuwauzie Zimbabwe...dah.!
 
Ndio na mimi najiuliza. Itakuwa yaleyale ya Kenya.!
Zimbabwe wanunue korosho wazipeleke wapi?kweli tunamawaziri wapuuzi kweli ambao hawajui hata wafanye nini.
Yaani muda wote wanakaa ofsini kujadili ZIM watanunua korosho kweli hii serikali iko mbioni kuanguka tena bila kusukumwa.
 
Hawa watu wamejidadavua vizuri sana.
Yaani haya majitu ni matakataka ya kiwango cha lami

Kuna watu wanatakiwa kuwa viongozi na kuna watu wanatakiwa kuongozwa milele daima

Sasa hii mikolomije ni ya kuswaga tu kama ng'ombe
 
Back
Top Bottom