Ziko wapi ajira 40,000 alizotuahidi Rais Samia?

Ziko wapi ajira 40,000 alizotuahidi Rais Samia?

Honorable GPA

Senior Member
Joined
Mar 31, 2019
Posts
149
Reaction score
223
Nakumbuka siku ya mei mosi mwaka huu, mheshimiwa Rais alituhaidi kwamba serikali yake inatarajia kutoa ajira za kudumu 40000 kwa vijana mwaka huu.

Hata bajeti iliyopitishwa na bunge kwa mwaka wa fedha 2021/2022 ambayo utekelezaji wake umeanza mwezi wa saba pia inazungumzia hicho kitu.

Japokuwa utekelezaji wake umeanza lakini hadi sasa hakuna dalili wala mtu hata mmoja ambaye amekwisha ajiriwa.

Je, hizi ajiriwa tulizoahidiwa na mheshimiwa Rais wetu ni lini zitaanza kutoka?

Maana isije ikawa kama ajira 5000 za ualimu alizoahidi hayati magufuri baadaye zikatokomea kusiko julikana hadi wa leo hazijulikani zilipo
 
Mkuu fanya kazi hata za kitaani , iwe kibarua, kupiga kokoto, kuchoma viepe , boda nk limradi malengo yakamilike!

Ukisubiri ajira elfu 40 kwa nchi inayogharamikia kesi za kubambikia na kutengeneza masanamu kwa gharama kubwa, utakumbuka shuka kumekucha, mvi zmejaa kichwan hauna kila kitu!

Nchii hii inaendeshwa kwa propaganda, usiamin kila kitu ,

UTANIKUMBUKA
 
Utasubiri sana mrembo uza hata nyanya tu hapo kitaa
 
Nafikiri zipo kwenye hatua na mchakato wa kuombewa vibali. Baada ya hapo zitatangazwa. Mwaka wa fedha ndio umeanza.

Tatizo watu wengi ni wabinafsi sana siku hizi, wao na watoto zao wameajiriwa serikalini lakini wanahimiza vijana wajiajiri.

Wengine wamekuwa wanafiki na kuwahadaa vijana kuwa waliacha kazi serikalini kwa kuona hakuna maslahi na kuamua kufanya shughuli binafsi kumbe ni wabunge na mawaziri, wengine wamepata teuzi ni maDAS, maRAS, DEDs, RCs, DCs.

Ipo siku vijana watachoka na kuamua kuwashikisha adabu. Tatizo kubwa kwa sasa ni ajira kwa vijana. Serikali iangazie hapo.
 
Walichoweza so far Madaktari wetu wa Uchumi ni kubuni mbinu ya kupunguza ajira ya Vibanda vya M pesa.

Nadhani hilo kwa 'Dokta' limekuwa rahisi kama kumsukuma Mlevi.....maana ni kuagiza tu "kateni hizi mtuletee tusishindwe kulipia Watoto FEZA ya school fees"..
 
ccm bila kupewa changamoto ya kuondolewa madarakani nchi hii haitakaa ipate maendeleo na tutaendelea kutawaliwa na marais wanaopuyanga kwa maneno yao.
 
Nakumbuka siku ya mei mosi mwaka huu, mheshimiwa Rais alituhaidi kwamba serikali yake inatarajia kutoa ajira za kudumu 40000 kwa vijana mwaka huu

Hata bajeti iliyopitishwa na bunge kwa mwaka wa fedha 2021/2022 ambayo utekelezaji wake umeanza mwezi wa saba pia inazungumzia hicho kitu.

Japokuwa utekelezaji wake umeanza lakini hadi sasa hakuna dalili wala mtu hata mmoja ambaye amekwisha ajiriwa.

Je, hizi ajiriwa tulizoahidiwa na mheshimiwa Rais wetu ni lini zitaanza kutoka?

Maana isije ikawa kama ajira 5000 za ualimu alizoahidi hayati magufuri baadaye zikatokomea kusiko julikana hadi wa leo hazijulikani zilipo
Tuliza mshono

Mwaka wa fedha ndio umeanza

ajira sio kama kutype JF
 
Tuliza mshono

Mwaka wa fedha ndio umeanza

ajira sio kama kutype JF

Na ule utapeli wa waziri Mkuu mzee wa ripoti za moto taarifa ndani ya siku 7, kuhusu treni ya SGR kuanza kazi mwezi huu wa 8 kipande cha Dar-Moro unaanza lini? Au bado wanatengeneza epsode za kesi za ugaidi?
 
Back
Top Bottom