Zikiwa zimebaki siku 50 Mwaka kuisha, hii ni tathmini ya matumizi yangu kwa mwaka 2020.

Nimependa #5 lakini nimesikitishwa na jinsi zilivyo pishana 5,6 na 7, kwamba starehe iko juu kuliko kujitoa kwako
 
Nimependa #5 lakini nimesikitishwa na jinsi zilivyo pishana 5,6 na 7, kwamba starehe iko juu kuliko kujitoa kwako
Hata hivyo mwaka huu nimefanya kupunguza hiyo #7 ilikuwa zaidi miaka ya nyuma. Mwakani nitaongeza hiyo #6 angalau ifike 3,500,000 kama nitaweza :p
 
roughly budget yako ya chakula ni tsh 7,000/= na starehe yako wastani kwa siku ni tsh. 3,000/= rekebisha hapa maisha ni mafupi sana kujibana kwa namna hii, utakaribisha magonjwa
 
roughly budget yako ya chakula ni tsh 7,000/= na starehe yako wastani kwa siku ni tsh. 3,000/= rekebisha hapa maisha ni mafupi sana kujibana kwa namna hii, utakaribisha magonjwa
Kuna targets nilijiwekea ambazo zililazimu nijinyime kidogo so far atleast 89% nimetimiza, panapo majaaliwa mwakani nitapunguza kujinyima
 
Mi natumia software ku track income and expenses, nilipoanza ilikuwa ni ngumu lakini sasa nimezoea, kila nikipata pesa na buget na kisha . Inanisaidia sana kujua wapi pesa inaenda. Mwaka huu matumizi makubwa yamekuwa kwenye ujenzi
Screenshot 2020-11-11 at 19.41.02.png
kurecord matumizi yake
 
Mi natumia software ku track income and expenses, nilipoanza ilikuwa ni ngumu lakini sasa nimezoea, kila nikipata pesa na buget na kisha . Inanisaidia sana kujua wapi pesa inaenda. Mwaka huu matumizi makubwa yamekuwa kwenye ujenziView attachment 1624337kurecord matumizi yake
Mkuu tupe link na sie tupakue
 
Mwaka 2020 ndiyo unaelekea mwishoni, huku zikiwa zimebaki siku 50 kuisha. Watanzania hatuna mazoea ya kuandaa bajeti zetu binafsi, lakini ni tool muhimu sana kwenye maisha yetu hasa unapotaka kuona maeneo ya kupunguza matumizi kama sio ya lazima

Hapa chini nimefanya tathmini ya matumizi ambayo nimefanya kwa mwaka mzima, inaweza isiwe exactly figures but i guess haitakuwa mbali sana na reality.

  1. Kodi ya pango, kwenye eneo hili hadi mwezi Septemba nilikuwa nimetumia 2,700,000
  2. Chakula, hadi kufikia Mwezi Oktoba nimetumia 2,100,000
  3. Gesi na Umeme hadi kufikia Mwezi Oktoba nilitumia 560,000
  4. Mavazi, hadi kufikia Mwezi Oktoba nimetumia 1,060,000
  5. Michango ya Harusi na Misiba hadi kufikia mwezi Oktoba nimetumia shilingi 650,000
  6. Starehe na kufurahi, hadi kufikia Oktoba nimetumia 800,000
  7. Sadaka na michango yake kwa pamoja imefikia 600,000 hadi Oktoba, 2020
  8. Kupiga taff home na ndugu hadi Oktoba nimetumia 1,000,000
  9. Mawasiliano, hadi mwezi Oktoba nimetumia 400,000
  10. Investments(Viwanja, Ujenzi, Mashamba) hadi Oktoba nimetumia 38,020,000
  11. Matumizi ya nyumbani 1,670,000
  12. Safari na Lodge hadi Mwezi Oktoba nimetumia 740,000
  13. Afya na matibabu nimetumia almost shilingi 940,000
  14. Bodi ya mikopo hadi kufikia Oktoba nimetumia 1,856,000
  15. Kulipia ada vijana, hadi Oktoba nimelipa 2,300,000
Hadi Oktoba nimetumia almost 55,396,000

Karibuni tupate experience zenu pia kwenye eneo hili, binafsi nimeona maeneo ambayo nahitaji kubana bajeti Mwaka ujao panapo Majaaliwa.

NB; Naomba tushare upande wa matumizi tu, upande wa Kipato ibaki ni SIRI ya mtu binafsi.
Bado umesahau kuhusu bank account umekopa bei gani? Matumizi makubwa sio kutusuhua katika maisha. Ni kuishi kwa ufahari mwisho wa siku ni stress
 
Back
Top Bottom