Zijue nchi saba zenye Walokole wengi

Setfree

JF-Expert Member
Joined
Dec 25, 2024
Posts
5,527
Reaction score
7,121
Walokole hapa namaanisha watu wenye sifa zifuatazo: waliotubu dhambi zao na kumpokea Yesu awe Bwana na Mwokozi wao, waliobatizwa ubatizo wa maji mengi na kujazwa Roho Mtakatifu. Ibada zao zina shangwe ya kiroho, kunena kwa lugha, shuhuda za miujiza na uponyaji, na mahubiri/mafundisho yanayohimiza utakatifu.

Nchi zenye Walokole wengi kwa idadi ni hizi hapa:
Marekani(USA): Walokole takriban milioni 49
Brazil: Walokole ~milioni 34.
Nigeria: Walokole ~milioni 25
Philippines: Walokole ~milioni 22
India: Walokole ~milioni 18.4
South Africa: Walokole ~milioni 17.7
Zimbabwe: Walokole ~milioni 5.4

Idadi ya walokole duniani inakadiriwa kuwa karibu milioni 280. Idadi hii ni ndogo lakini inaonyesha ukweli wa maneno aliyosema Yesu katika Mathayo 7:14
"Bali mlango ni mwembamba, na njia imebana iendayo uzimani, nao waionao ni wachache."
====================
Kwa mujibu wa Ripoti za Gordon‑Conwell, idadi ya Wakristo wote duniani ni takriban bilioni 2.6. Idadi hii ni kubwa lakini inasikitisha kwa sababu wengi wao wana majina tu ya kikristo lakini hawayafanyi mapenzi ya Mungu. Yesu alisema:
"Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika Ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.” (Mathayo 7:21)
 
Je, wewe ni miongoni mwa Walokole wanaopita njia nyembamba au unapita njia pana?
"Ingieni kwa kupitia mlango ulio mwembamba; maana mlango ni mpana, na njia ni pana iendayo upotevuni, nao ni wengi waingiao kwa mlango huo." (Mathayo 7:13)
 
Huwezi kuwafahamu walokole wa kweli maana wapo kila dhehebu hadi RC. Hivyo hiyo sifa uliyotoa wewe ni ya madhehebu wanayojiita walokole. Maandiko yanasema "Bwana awajua walio wake"
 
Wanawahesabu vipi hao walokole maana imani hasa kama walokole ni kila mtu anayemwamini bwana kuwa mwokozi wa maisha yako basi wewe ni mlokole..
 
"ULOKOLE " kwahiyo wasio batizwa kwa maji mengi sio walokole? Ibada hazina shangwe, kunena kwa lugha wala shuhuda za miujiza sio walokole?
 
Huwezi kuwafahamu walokole wa kweli maana wapo kila dhehebu hadi RC. Hivyo hiyo sifa uliyotoa wewe ni ya madhehebu wanayojiita walokole. Maandiko yanasema "Bwana awajua walio wake"
NABII MTARAJIWA unaelewa maana ya neno "takriban?" au alama hii: " ~"?? Idadi iliyotajwa hapo sio idadi kamili.
By the way, huyo mlokole unayesema yupo RC, alibatizwa ubatizo wa maji mengi na Padre yupi?
 
Ukiiangalia hiyo list utabaini kwa kiasi kikubwa waliopelekewa hizi porojo ndio wako busy nazo kuliko waliozitunga na kuzikuza

Watu tuliotawaliwa na wakoloni tunakariba ya kuponda na kukosoa karibu kila kitu kilicholetwa na wazungu...... kasoro uongo wao tu Mungu, huu tunauamini kupitiliza
 
NABII MTARAJIWA unaelewa maana ya neno "takriban?" au alama hii: " ~"?? Idadi iliyotajwa hapo sio idadi kamili.
By the way, huyo mlokole unayesema yupo RC, alibatizwa ubatizo wa maji mengi na Padre yupi?
Achana na mambo ya Roman fata ya marekani we mama vipi ?

Kila mtu ajikane binafsi Baki na ulokole wako naye abaki na uroma wake!!
 
Hao ndo wataingia mbinguni mke wake na secretarybird

JE zile kabila kumi na mbili za Israel zilizoahidiwa mbingu ni zipi ?

Kwahiyo wachaga hatutaona ufalme wa Mungu? cc min -me
Kitendo cha kumfikiria mtu ataenda au haendi ni kujidanganya
Hujui Uhusiano wa mtu na Mungu kiundan
Cha msingi Omba uishi kwenye njia nzuri
Hata wanaotenda mema bado kuna makosa wanayafanya
 
Kitendo cha kumfikiria mtu ataenda au haendi ni kujidanganya
Hujui Uhusiano wa mtu na Mungu kiundan
Cha msingi Omba uishi kwenye njia nzuri
Hata wanaotenda mema bado kuna makosa wanayafanya
Ninyi walokole ndo mnajikuta special group la kwenda mbinguni ndo maana nimeuliza mmeshaokoka hamna madhambi
 
Naomba kujua walokole kwa English wanaitwaje!
 
Ninyi walokole ndo mnajikuta special group la kwenda mbinguni ndo maana nimeuliza mmeshaokoka hamna madhambi
wengi na sitaki Unafki
Na wengi wanaojifanya bado maovu yanafanyika
Huo ni Mtazamo wao
Na siwez kumsema mtu ataenda au haendi bali ni Kumsaidia awe kwenye njia Nzuri na kumuombea
Mungu atusaidie
Mungu anatumia njia nyingi kumsaidia Mtu afike mbinguni
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…