chase amante
JF-Expert Member
- Feb 24, 2018
- 5,652
- 2,146
ACT -2020
BIASHARA ndio njia pekee ya kukufanya ulinde na kuongeza mtaji wako. Mara nyingi Kufunga Biashara sio kulinda mtaji bali kuupunguza kupitia matumizi.
Wengi hawafungi bali wanabadili na wapo wachache wanaohamisha biashara zao.
Dhana ya wapiga deal ni sahihi kwa zaidi ya 50%..
Hakuna mfanyabiadhara mwaminifu..
Wenyewe wamekiri kutoa rushwa japo wanasababu..
Rais amekuja na ushahid wa makampuni 17000 ya kitapeli.
Wako wenye mauzo bilion wao huonyesha milion 20.
Wako kina Kaluwa wazee wa ganji la bilion 4
Hawa wakifunga kwa nini tusiseme ni wapiga deal
Mkuu ndipo lilipo tatizo basi. Woga! Mmoja akipotea tukijitokeza kwa malaki kuulizia yuko wapi kesho hatapotea tena mwingine. Unafanya kosa kubwa kufikiri atakuja kuingia kiongozi atakayebadili mfumo bila kusimamiwa na watu. Wakati wa Kikwete mnayemsifia na kusema alijali demokrasia mbona kina Dr Ulimboka walifanyiziwa. Tatizo kubwa ni kuwa wale wanaopenya na kushika nafasi za juu wengi wao wana malengo mengine. Mara nyingi mfumo haurusu mtu mwenye nia njema kushika uongozi. Mara nyingi ni wale wabaya tu japo kuna exceptions mara chache.
Zitto hana jipya ni opportunist kama walivyo wengine. Yeye ndiyo alieandaa mkutano na hao wafanyabiashara? Tulioangalia tulimsikia Rais akiwasisitizia kutoogopa na waseme yooote ili kama kutatua matatizo yatatuliwe. Zitto ni kati ya watu nisiowaamini na sitowaamini maisha.
Bora hata Kingwendu Aisee. At least yeye atasikiliza watuMbona ndugu migebuka ameshindwa kutwambie kama tusipo muongezea Magufuli siku ikulu nani tumpe?
Na ndio hapo tujue kuwa rais huyu ni wa hovyo kuwahi kutokea....huwezi kuharibu vyote kwa pamojaUkweli ni kuwa Mh. Rais amefanya makosa mengi sana kwenye uchumi, demokrasia na haki za binadamu.
Tunachoshukuru ni kuwa na yeye ameanza kuyatambua makosa aliyoyafanya lakini kwa bahati mbaya damage iliyofanyika ni kubwa, na ni vigumu sana kuyaondoa madhara yake hata kwa miaka kumi. Leo Tamzania imeingizwa kwenye kundi la risk countries for foreign investments.
Makosa yaliyofanyika katika awamu hii yanatukumbusha umuhimu wa katiba mpya ambayo haimpi mtu mmoja mamlaka ya kufanya chochote anachokitaka bila ya kushirikiana na taasisi nyingine.
Watanzania tumerogwa, siyo bure!
Zito Kabwe atahongwa na nani kutetea Bandari ya Bagamoyo? Haiingii kwenye kikao chochote cha maamuzi. Wanaoingia ni MAKADA WA CCM, ambao ndiyo wameingia mikataba yote ya hovyo tangia awamu ya pili.
Kwa hiyo kama yupo wa kumhonga Zito Kabwe, basi ni wale MAKADA WA CCM, walioingia makubaliano ya kifisadi kuhusu Bandari ya Bagamoyo.
Ukweli mchungu ndiyo huu: CCM NI JANGA LA KITAIFA.
Wanaoitetea wote ni WASALITI Wa Taifa letu!
Engine ya Chama Ni Kamati Kuu na Secretariat zake. Waliopo huko Kama si vikongwe waliojichokea, ni vijana waliojizeekea kabla ya umri. Akina Pole Pole. Hawa wanachojuwa Ni kutengeneza propaganda uchwara ili bora liende.One thing really boggles my mind. Inawezekanaje makosa haya makubwa na ya kisera kufanyika chini ya chama kikongwe, chenye misingi bora kabisa, uzoefu wa miaka mingi na sera zinazoeleweka? Something is terribly wrong somewhere. Uchambuzi wa kina unahitajika kupata ufumbuzi endelevu. Kwa uzoefu tuliopata katika miaka hii minne nadhani hata ile rasimu ya Warioba haitoshi!
Nani kaomba poo..Sasa kama ni wapiga dili kinachowauma ni nini? Acheni wafunge na wasepe na nyie mkae na hao wachache ambao siyo wapiga dili, inashangaza kuona mnataka kukaa chini na wapiga dili muombe poo