Ziito Kabwe ameongea ukweli mchungu

Ziito Kabwe ameongea ukweli mchungu

Nimesema hivi: Wananchi wa kawaida hali ni ile ile. Kwa wakubwa waliokuwa wanafaidi kuna baadhi hali zao ni mbaya. Ila hilo siyo tatizo la wananchi wa kawaida. Ni tatizo lao na familia zao.
Acha kuzingua basi,last tegime wananchi walikuwa wanalalamikia zaidi taasisi za haki na huduma kwamba pesa iko mbele lakini sio kwamba pesa haipatikani hapana this why mtu mmoja mmja walikuwa wana maendeleo kuliko saizi ambapo pesa ya kula tu ndio watu wanahangaika nayo,kumbuka wakibanwa wenye pesa maskini anazidi kuwa hoi ndio maana kilio ni kikubwa kuliko kipindi kilichopita
Mama muuza mboga na samaki mwenye kimeza tu aliniambia walikuwa wanaweza kuuza hadi 150,000 kwa siku lakini saizi ukipata 20,000 unaona ngekewa
Sasa mlishindwa nini kurekebisha yale mapungufu badala ya kuvuruga? Mafisadi na mahakama yao wako wapi ili kujustify hiyo ya kusema kulikuwa na wizi mkubwa? Haiingii akilini kila ngumbaru wa ccm saizi ndio mchumi
 
Kwann huwa mashambulia sana awamu iliyopita? Halafu Mara zote nikiuliza huo wizi umelingaishwa na wizi wa awamu zipi kwa data zipi ukaonekana ndo awamu ya wizi kuliko awamu zote huwa sipewi majibu ya kuridhisha.

Hakuna utawala usio na mapungufu. Utawala uliopita haukuwa wa ajabu saaana. Na uchumi pia haukushikiliwa na wezi kama mnavyosema' sema ulikuwa utawala wa kibepari na utawala wa kibepari lazima waibuke watu wanaoziona fursa na kuzitumia kwa njia yoyote hata za ujanja ujanja.

Mfano wa tofauti ya mfumo wa Ujamaa na ubepari: umefungua duka, ukaajiri mfanya biashara ambaye anajua biashara haswa, anakuletea faida ya milioni tatu kwa siku na yeye anakuibia milioni au umeajiri mwaminifu asiyeiba hata mia Ila anakuletea faida ya laki tano au milioni. Ungechagua yupi? Nchi yoyote ya kibepari wajanja wajanja lazima wawepo Ila maendeleo pia ni makubwa. China sijui waliwezaje kufanikiwa kupitia Ujamaa.
Nitapinganga na wewe kabisa. ''Ujanja ujanja'' uliyo kwenye nchi za kibebari siyo kuiba mali za umma bali ni ''ujanja ujanja'' wa kufanya kazi kwa bidii. Nenda USA basi ukaibe uone cha moto! Sisi huku kwetu watu walikuwa wanajichotea na hakuna wa kuonyesha concern ya aina yoyote sembuse kuchukuwa hatua. Kumbuka mimi huwa sisemi kuwa ufisadi umeisha awamu hii... la hasha. Bado upo sana tu. Lakini angalau kuna watu wanaoonyesha concern, kitu ambacho ni dalili nzuri kama kitakuwa mantained kwa kipindi kirefu. Bila kujua ugonjwa ni vigumu dr kutibu ugonjwa... hivyo hivyo bila kuwa na viongozi wanaojua matatizo yanayotukwamisha ni vigumu kuendelea. Na zaidi niseme hayo maisha magumu ya sasa hivi sipingi kama yapo ila ni LAZIMA yangekuwepo kwa rais yeyote mwenye nia ya kutibu ''ugonjwa wetu''. Hili siyo zoezi la miaka mitano na product ionekane...
 
China baada ya kukuta wanatumia nguvu kubwa na maumivu makali ya ujamaa wakaachana rasmi na huo ujamaa,ikumbukwe vizuri china imeibuka kuwa taifa la uchumi unaopaa baada ya kufungua milango ya uwekezaji yaani liberalization na privatization na hata wawekezaji wakubwa china ni wageni ndio wakapata fursa ya kuiba na ku copy teknolojia za watu,hadi kesho china ni wajamaa kwenye siasa lakini sio kwenye uchumi.Hakuna nchi yoyote ya kijamaa imewahi endelea duniani hapa haipo
kweli boss
 
Acha kuzingua basi,last tegime wananchi walikuwa wanalalamikia zaidi taasisi za haki na huduma kwamba pesa iko mbele lakini sio kwamba pesa haipatikani hapana this why mtu mmoja mmja walikuwa wana maendeleo kuliko saizi ambapo pesa ya kula tu ndio watu wanahangaika nayo,kumbuka wakibanwa wenye pesa maskini anazidi kuwa hoi ndio maana kilio ni kikubwa kuliko kipindi kilichopita
Mama muuza mboga na samaki mwenye kimeza tu aliniambia walikuwa wanaweza kuuza hadi 150,000 kwa siku lakini saizi ukipata 20,000 unaona ngekewa
Sasa mlishindwa nini kurekebisha yale mapungufu badala ya kuvuruga? Mafisadi na mahakama yao wako wapi ili kujustify hiyo ya kusema kulikuwa na wizi mkubwa? Haiingii akilini kila ngumbaru wa ccm saizi ndio mchumi
Sizingui ila nachangia mawazo yangu! Ukiona unazinguka basi kaa pembeni waachie wasiozinguka! As simple as that! Sijui kiwango cha elimu yako lakini ni ajabu kutegemea nchi ilivyokuwa kwenye deep shit la ufisadi uongozi uweze kurebisha mambo kwa muda mfupi... Haya ni mawazo ya watu wavivu...
 
Mbona ndugu migebuka ameshindwa kutwambie kama tusipo muongezea Magufuli siku ikulu nani tumpe?
Atawale milele kwani hakuna mtanzania anayeweza kutawala ni Magu tu. Na hata akifa asiwekwe mtu mwingine ni yeye tu ndiyo mwenye uwezo wa kutawala. Akili ya mtanzania ndipo ilipoishia, hana uwezo wa kuwa mbunifu wala mtafiti ndiyo maana miaka 58 ya uhuru badala ya kwenda mbele tunarudi kinyume nyume
 
Zitto hana jipya ni opportunist kama walivyo wengine. Yeye ndiyo alieandaa mkutano na hao wafanyabiashara? Tulioangalia tulimsikia Rais akiwasisitizia kutoogopa na waseme yooote ili kama kutatua matatizo yatatuliwe. Zitto ni kati ya watu nisiowaamini na sitowaamini maisha.
Kwanini alikua anasema wasiogope?
 
KWANI AMETAJA KIPINDI CHA KIKWETE KTK HOJA YAKE? KWANI NI KIPINDI KIPI UCHUMI ULIWAHI KUWA MCHAFU KAMA AWAU HII?
Usitumie nguvu kumjibu kila mtu wengine wahurumie tuu km huyo wa hapo pichani ana hitaji huruma tuu
 
Mbona ndugu migebuka ameshindwa kutwambie kama tusipo muongezea Magufuli siku ikulu nani tumpe?
Inayofanya kampeni kwasasa nisisim wengene yatupasa tutumie akilizetu kwanini wao waanze kufanya kampeni sasa navyama vingine vikataliwe kufanyahivyo ukweli mchungu niwazi sisim imevurunda Sana tuwe makini
 
Unazingua banaaa!!
ukinawili = ukinawiri! By the way umesoma na kuelewa? Haya ngoja nijibu swali lako la ki-layman ambalo ni la ki-layman kweli kweli: Hata mimi nataka nifaidi uchumi kama utanawiri kwani hakuna mtu asiyependa maisha mazuri! Ila dukuduku langu bado liko pale pale: Uchumi wetu haukuwa mzuri hata wakati wa Kikwete. Inakuwaje Zitto anasema ''tuurejeshe'' ulikokuwa? Hakika atakuwa anazungumzia uchumi wake binafsi na siyo uchumi wa nchi!
 
mzee kuanzia sasa wasikilize wapinzani ndio wanaosema ukweli sasa mnavyowafanyia kule bungeni na nje si sawa nadhani sasa unaweza badilika baada ya kuelewa umuhimu wa bunge live na kukubali kukosolewa
Kwelikweli kabisa
 
Nitapinganga na wewe kabisa. ''Ujanja ujanja'' uliyo kwenye nchi za kibebari siyo kuiba mali za umma bali ni ''ujanja ujanja'' wa kufanya kazi kwa bidii. Nenda USA basi ukaibe uone cha moto! Sisi huku kwetu watu walikuwa wanajichotea na hakuna wa kuonyesha concern ya aina yoyote sembuse kuchukuwa hatua. Kumbuka mimi huwa sisemi kuwa ufisadi umeisha awamu hii... la hasha. Bado upo sana tu. Lakini angalau kuna watu wanaoonyesha concern, kitu ambacho ni dalili nzuri kama kitakuwa mantained kwa kipindi kirefu. Bila kujua ugonjwa ni vigumu dr kutibu ugonjwa... hivyo hivyo bila kuwa na viongozi wanaojua matatizo yanayotukwamisha ni vigumu kuendelea. Na zaidi niseme hayo maisha magumu ya sasa hivi sipingi kama yapo ila ni LAZIMA yangekuwepo kwa rais yeyote mwenye nia ya kutibu ''ugonjwa wetu''. Hili siyo zoezi la miaka mitano na product ionekane...
Mkuu' hii concern yako nimeshakujibu. Hakuna utawala usio na mapungufu. Na ishu ya wizi mtu yoyote mwenye akili hawezi sema utawala huu wizi ni mkubwa bila data au kulinganisha na awamu iliyo na wizi kidogo. Kuhusu kujali mbona awamu iliyopita ndo tulishuhudia kusakamwa kwa wezi mpaka waziri mkuu kujiuzulu? Wapinzani na waandishi wa habari waliachwa waichunguze serikali watakavyo halafu waikosoe na kuichamba wawezavyo. Unadhani ulifahamuje kuwa kuna wizi kama si raisi wako kuruhusu wewe ufahamu? Sema raisi aliyepita alikuwa baba wa wote hilo ndo kosa lake, alikuwa baba wa wazalendo, baba wa wezi, wafanya biashara, waandishi wa habari na hata adhabu alizitoa kwa hali hiyo hiyo ya ubaba, hili lilikuwa ni kosa ndio Ila kosa sahihi. (sijui kama utanielewa ninaposema kosa sahihi) pamoja na mapungufu Tuwe na heshima kwa kiongozi aliyepita.

Unapokuwa na ubinadamu ukaita wapinzani ikulu kushiriki Chai na watoe mapendekezo wewe unakuwa dhaifu, hufai kuongoza nchi maana unacheka cheka. wapinzani ndo waliamini hili katka awamu iliyopita. Mpaka leo sijawaelewa wanataka nn. Wapo kama watoto wa kambo wenye kulalamika kila wakati.
 
Na tena wakiambiwa biashara zinafungwa, wao wanasema kuna mpya zinafunguliwa na Bungeni wanapiga makofi.

Msiwaamini hawa watu.Hii ni siasa tu.
Magifuli alimtuma mkuu wa wilaya ya hai akaharibu mashamba ya mfanyabiashara Mbowe, ili awe masikni, Je? niwafanyabiashara wangapi? serikali hii imewahujumu, ukiondoa wale wa korosho
 
Zito Kabwe njoo na ngonjera zako za bandari ya bagamoyo.

Mnahongwa pesa mtetee ujinga na ufisadi
Wewe utasemaje kama utawala ulikufanya upate pesa yakununua mtoto chupa utajuwa uchumi kweli
 
Serikali imewahujumu makusudi wafanyabiashsra , kutumia PCB, DPP, DCI, TISS, TRA na polisi,

kila MTU aliona ya MO, Manji, Zacharia, Mbowe, Korosho,
Baada ya hujuma eti endo wanaleta maigizo ikulu

Nadhani tuandike katiba ambayo itaulinda uchumi, wafanyabiasha dhidi ya tofauti na maslahi ya wana siasa
 
Back
Top Bottom