Ziito Kabwe ameongea ukweli mchungu

Ziito Kabwe ameongea ukweli mchungu

Zitto Kabwe:
Wakati Biashara zinafungwa mawaziri walikuwa wanasema kuwa wanaofunga ni WAPIGA DILI. Leo nimeshangaa kuona eti Rais anashangaa kwanini Biashara zinafungwa. Eti na maagizo yanatoka kuwa TRA isifunge Biashara za Watu sababu za Kodi. Biashara zaidi ya 200K zimeshafungwa!

Ziito Kabwe:
Leo siku nzima nimefuatilia Mkutano wa Rais Magufuli na Wafanyabiashara kutoka nchi nzima. Nawapongeza Wafanyabiashara waliojitoa bila woga kueleza hali halisi. Yote yaliyosemwa tumekuwa tukiyasema Bungeni na Nje ya Bunge. Fikra zangu kuwa tunahitaji Uongozi mpya zimeimarika

Zitto Kabwe:
Ninawasihi Watanzania kuwa tusipumbazwe na haya ‘mateke ya punda anayekata Roho’. Serikali ya CCM ya awamu ya 5 chini ya Rais Magufuli haipaswi kuongezewa hata siku moja Ikulu. Njia ya uhakika kurejesha Uchumi wetu kwenye Reli sahihi ni kufanya MABADILIKO.

Zitto Kbwe:
Baada ya mkutano ule wa Rais Magufuli na Wafanyabiashara nimetazama makadirio ya makusanyo ya Kodi za Wafanyakazi nchini kwa Bajeti ya 2019/2020 na nimekuta makadirio yameshuka kwa zaidi ya TZS 500 Bilioni. Hii maana yake ni kuwa ajira rasmi zimeshuka sana

Chanzo:Ukurasa wake wa twitter.

My take:
Ipo siku tutakuja kuelewa ukweli huu wakati tukiwa tumechelewa.

CCM ni wajanja sana tumieni akili watanzania(hapa kuna siasa inaendelea).

Kushughulikia watu wachache kwa faida ya chama na kiongozi wao kwao si tatizo.

Maandalizi ya 2020 yanaendelea.

Biashara zaidi ya 200 k
hyo ina maanisha nini ?
200 K
 
Eti nini Zitto anasema? Anasema ''Njia ya uhakika kurejesha Uchumi wetu kwenye Reli sahihi ni kufanya MABADILIKO''. Hivi jamani uchumi wetu ulishakuwa kwenye reli sahihi ili tuurejeshe? Anakumbuka kipindi cha Kikwete alichokuwa anafaidi ndiyo anakiita ''uchumi ulikuwa kwenye reli sahihi''. Huu ni upumbavu na ubinafsi wa hali ya juu. Wanasiasa wa aina hii walaaniwe kwani wanajifikiria wao tu! Kweli kile kipindi cha Kikwete ambacho kila mtu alikuwa anaachiwa kuiba na kufanya hujuma atakavyo ndiyo anasema tulikuwa kwenye reli sahihi?
Mkuu kwan hujui kua Sasa hivi uchumi unakua kwa 4% wakati zamani ilikua 7% acha kujifanya nyumbu
 
Ya wizi si ya kwangu ila ni ya awamu iliyopita (japo hata sasa bado wizi upo lakini angalau kuna watu wanaoonyesha concern). Nchi ilikuwa inachezewa na waliokuwa wanafaidi ni wachache, Zitto akiwa mmoja wapo. Ndugu zangu, jamaa, majirani na wananchi wa kijijini kule nitokako hawaoni tofauti kati ya uchumi wa sasa na uchumi uliopita!
Sio kweli,hali imezidi kuw mbaya zaidi!
 
Ukweli ni kuwa Mh. Rais amefanya makosa mengi sana kwenye uchumi, demokrasia na haki za binadamu.

Tunachoshukuru ni kuwa na yeye ameanza kuyatambua makosa aliyoyafanya lakini kwa bahati mbaya damage iliyofanyika ni kubwa, na ni vigumu sana kuyaondoa madhara yake hata kwa miaka kumi. Leo Tamzania imeingizwa kwenye kundi la risk countries for foreign investments.

Makosa yaliyofanyika katika awamu hii yanatukumbusha umuhimu wa katiba mpya ambayo haimpi mtu mmoja mamlaka ya kufanya chochote anachokitaka bila ya kushirikiana na taasisi nyingine.

One thing really boggles my mind. Inawezekanaje makosa haya makubwa na ya kisera kufanyika chini ya chama kikongwe, chenye misingi bora kabisa, uzoefu wa miaka mingi na sera zinazoeleweka? Something is terribly wrong somewhere. Uchambuzi wa kina unahitajika kupata ufumbuzi endelevu. Kwa uzoefu tuliopata katika miaka hii minne nadhani hata ile rasimu ya Warioba haitoshi!
 
Binafsi simkubali kabisa huyu bwana na ni bora tu muda wake uishe aondoke madarakani na ikiwezekana aondoke yeye na CCM yake yote waje watu wengine watuongoze.

One battle at a time! Avoiding fighting on many fronts; it is counterproductive.
 
Wia ini ze raiti traki.

Hamjajua tu jinsi watumishi wanamhujumu huyu Pogba Kwa kuwakandamiza haki zao.Wapo kimya kama wameridhika vile

Wakati mwingine siyo kunyamaza bali hakuna kazi ya kufanya!
 
Mkuu' hii concern yako nimeshakujibu. Hakuna utawala usio na mapungufu. Na ishu ya wizi mtu yoyote mwenye akili hawezi sema utawala huu wizi ni mkubwa bila data au kulinganisha na awamu iliyo na wizi kidogo. Kuhusu kujali mbona awamu iliyopita ndo tulishuhudia kusakamwa kwa wezi mpaka waziri mkuu kujiuzulu? Wapinzani na waandishi wa habari waliachwa waichunguze serikali watakavyo halafu waikosoe na kuichamba wawezavyo. Unadhani ulifahamuje kuwa kuna wizi kama si raisi wako kuruhusu wewe ufahamu? Sema raisi aliyepita alikuwa baba wa wote hilo ndo kosa lake, alikuwa baba wa wazalendo, baba wa wezi, wafanya biashara, waandishi wa habari na hata adhabu alizitoa kwa hali hiyo hiyo ya ubaba, hili lilikuwa ni kosa ndio Ila kosa sahihi. (sijui kama utanielewa ninaposema kosa sahihi) pamoja na mapungufu Tuwe na heshima kwa kiongozi aliyepita.

Unapokuwa na ubinadamu ukaita wapinzani ikulu kushiriki Chai na watoe mapendekezo wewe unakuwa dhaifu, hufai kuongoza nchi maana unacheka cheka. wapinzani ndo waliamini hili katka awamu iliyopita. Mpaka leo sijawaelewa wanataka nn. Wapo kama watoto wa kambo wenye kulalamika kila wakati.
Data unazozitaka huwezi kuzipata kwa sababu wezi hawaweki data wanapoiba. Vinginevyo bado nasimamia msimamo wangu. Kikwete hakuwa kiongozi mzuri hata kidogo. Kwangu mimi ni bora utawala huu mara kumi kuliko uliopita. Kuhusu wapinzani, kama walivyo viongozi wengi wa siasa Afrika, wanajali matumbo yao tu! Hawana wanachosimamia ukiondoa wachache sana!
 
Data unazozitaka huwezi kuzipata kwa sababu wezi hawaweki data wanapoiba. Vinginevyo bado nasimamia msimamo wangu. Kikwete hakuwa kiongozi mzuri hata kidogo. Kwangu mimi ni bora utawala huu mara kumi kuliko uliopita. Kuhusu wapinzani, kama walivyo viongozi wengi wa siasa Afrika, wanajali matumbo yao tu! Hawana wanachosimamia ukiondoa wachache sana!
Utawala huu ni wa ccm na uliopita ni wa ccm. Angalia vizuri utagundua kuwa utawala ni wa ccm, unafata ilani ya ccm. Hakuna tofauti. Maendeleo ni yale yale ya ccm, mapungufu ni yale yale ya ccm, ubora ni ule ule wa ccm, udhaifu ni ule ule wa ccm. Angalia vizuri utagundua viongozi ni wale wale wa ccm. Uwezekano ni kuwa Ccm itatawala sana kwa sababu ya uwezo wake mkubwa wa kukuaminisha wewe mtawaliwa kuwa sasa unaongozwa na watu tofauti. Waliompa kiongozi aliyepita uongozi chamani ndo Waliompa huyu wa sasa. Ubora na udhaifu wa hao watu ni ule ule. Tamaduni na taratibu zao ni zile zile. Sema mwonekano wa nje ni tofauti, ccm ya kikwete ni tofauti na ya mkapa ya mkapa tofauti na mwinyi kimwonekano wa kisiasa si kimtindo na muundo wa utendaji. Ccm ni Ile Ile, watu wale wale, watendaji wale wale wanarithishana.

Kama sipo sahihi jiulize awamu hii kiongozi yupi kawajibishwa kwa sababu ya wizi awamu iliopita unaoupigia kelele? Wezi si huwa wanashtakiwa na kuadhibiwa? Hakuna viongozi kwa udhaifu wao na uzembe walisababisha hao Wezi waiibie nchi? Wamewajibishwa? Point ni moja tu ccm ni Ile Ile na ina madhaifu yake Ila awamu zote zinajitahidi kadri ziwezavyo kuongoza nchi.

Akili ya ccm ni kubwa ndo maana ipo madarakani. Hao wanaosema wanategemea polisi na jeshi mm nawaambia kuwafanya polisi na jeshi kuwa upande wako pia ni matumizi ya akili. Siku upinzani ukiizidi akili ccm watakuwa madarakani. Acha kuiponda awamu iliyopita.
 
Eti nini Zitto anasema? Anasema ''Njia ya uhakika kurejesha Uchumi wetu kwenye Reli sahihi ni kufanya MABADILIKO''. Hivi jamani uchumi wetu ulishakuwa kwenye reli sahihi ili tuurejeshe? Anakumbuka kipindi cha Kikwete alichokuwa anafaidi ndiyo anakiita ''uchumi ulikuwa kwenye reli sahihi''. Huu ni upumbavu na ubinafsi wa hali ya juu. Wanasiasa wa aina hii walaaniwe kwani wanajifikiria wao tu! Kweli kile kipindi cha Kikwete ambacho kila mtu alikuwa anaachiwa kuiba na kufanya hujuma atakavyo ndiyo anasema tulikuwa kwenye reli sahihi?

Ishara mojawapo ya hali mbaya tuliyonayo sasa ni ongezeko kubwa mitandaoni la watu waliopewa kazi ya kushambulia hoja za wachangiaji zinazoonekana kutokuwa na mtazamo wa kusifia watawala wa sasa. Na kwa vile uwezo wao wa kushambulia hizo hoja ni madogo huishia kutoa kejeli tu matusi. Hata hivyo busara ya kawaida inataka kuangalia mtu wa kumshambulia. Mbilikimo kwa mbilikimo would make a good march. Zitto is a giant; not hoodlum! Hali haikuwa nzuri sana awamu ya 4 lakini angalau watu walikwenda kulala wakijua kesho itakuwaje. Uchumi ulikuwa unaongezeka kwa 7% badala ya 4% ya sasa; mzunguko wa fedha mtaani ulikuwa mkubwa na sekta binafsi ambayo ndiyo injini ya uchumi haikuwa inapigwa vita waziwazi. TIC ilikuwa inasajili miradi mipya ya uwekezaji karibu 1000 kwa mwaka tofauti na sasa ambapo inasemekana ni kama 200! Ajira zilikuwepo kila mwaka na watumishi wa serikali walipata nyongeza zao za kisheria za kila mwaka na kupandishwa madaraja. Tukirudi hapo tulipokuwa awamu ya nne siyo haba. Kisiasa, mtu mmoja amesema tumerudi nyuma miaka 50! Hata wakoloni waliotutawala wanatushangaa.
 
Magifuli alimtuma mkuu wa wilaya ya hai akaharibu mashamba ya mfanyabiashara Mbowe, ili awe masikni, Je? niwafanyabiashara wangapi? serikali hii imewahujumu, ukiondoa wale wa korosho
Ndio maana huwa simkubali Magu hata siku moja.
 
Utawala huu ni wa ccm na uliopita ni wa ccm. Angalia vizuri utagundua kuwa utawala ni wa ccm, unafata ilani ya ccm. Hakuna tofauti. Maendeleo ni yale yale ya ccm, mapungufu ni yale yale ya ccm, ubora ni ule ule wa ccm, udhaifu ni ule ule wa ccm. Angalia vizuri utagundua viongozi ni wale wale wa ccm. Uwezekano ni kuwa Ccm itatawala sana kwa sababu ya uwezo wake mkubwa wa kukuaminisha wewe mtawaliwa kuwa sasa unaongozwa na watu tofauti. Waliompa kiongozi aliyepita uongozi chamani ndo Waliompa huyu wa sasa. Ubora na udhaifu wa hao watu ni ule ule. Tamaduni na taratibu zao ni zile zile. Sema mwonekano wa nje ni tofauti, ccm ya kikwete ni tofauti na ya mkapa ya mkapa tofauti na mwinyi kimwonekano wa kisiasa si kimtindo na muundo wa utendaji. Ccm ni Ile Ile, watu wale wale, watendaji wale wale wanarithishana.

Kama sipo sahihi jiulize awamu hii kiongozi yupi kawajibishwa kwa sababu ya wizi awamu iliopita unaoupigia kelele? Wezi si huwa wanashtakiwa na kuadhibiwa? Hakuna viongozi kwa udhaifu wao na uzembe walisababisha hao Wezi waiibie nchi? Wamewajibishwa? Point ni moja tu ccm ni Ile Ile na ina madhaifu yake Ila awamu zote zinajitahidi kadri ziwezavyo kuongoza nchi.

Akili ya ccm ni kubwa ndo maana ipo madarakani. Hao wanaosema wanategemea polisi na jeshi mm nawaambia kuwafanya polisi na jeshi kuwa upande wako pia ni matumizi ya akili. Siku upinzani ukiizidi akili ccm watakuwa madarakani. Acha kuiponda awamu iliyopita.
Umeandika ukweli ambao mimi wala sina shaka nao. Na ndipo ilipo shida kubwa, i.e. kila utawala unaingia na madoido na mapungufu yake. Ukiondoka anayefuatia nae anaingia na yake. Shida kubwa mimi sidhani kama ni CCM. Naomba usinielewe vibaya siyo kuwa nasema ni nzuri. Ila shida kubwa ni sisi wananchi wa Tanzania. Hatutaki na tuu waoga mno kuwasimamia viongozi wetu. Kiongozi anafanya madudu lakini sisi tunakaa kimya na kuchekelea kama tunaangalia movie nzuri. Si wasomi si wakulima. Nikupe mfano: Makonda ameshafanya na kutenda mambo mabaya sana ambayo yanakiuka kanuni za uongozi lakini jiji lenye ''wajanja'' kama Dar wanakubali kuswagwa kama ng'ombe! Kwa nini tunashindwa kumwonyesha aliyemteua kuwa huyu mtu hatufai? Unajua nchi ikiwa na wanachi wanaojielewa inaweza kuwa na viongozi wazuri sana hata kama inataliwa na chama kimoja kwa muda mrefu kama CCM? La muhimu ni wananchi kukemea kila uovu unaofanywa bila kujali vyama.
 
Zito Kabwe njoo na ngonjera zako za bandari ya bagamoyo.

Mnahongwa pesa mtetee ujinga na ufisadi

Jikite kwenye mada, wapiga dili wameisha? Kibwagizo chali kama kile cha hapa kazi tu
 
Ishara mojawapo ya hali mbaya tuliyonayo sasa ni ongezeko kubwa mitandaoni la watu waliopewa kazi ya kushambulia hoja za wachangiaji zinazoonekana kutokuwa na mtazamo wa kusifia watawala wa sasa. Na kwa vile uwezo wao wa kushambulia hizo hoja ni madogo huishia kutoa kejeli tu matusi. Hata hivyo busara ya kawaida inataka kuangalia mtu wa kumshambulia. Mbilikimo kwa mbilikimo would make a good march. Zitto is a giant; not hoodlum! Hali haikuwa nzuri sana awamu ya 4 lakini angalau watu walikwenda kulala wakijua kesho itakuwaje. Uchumi ulikuwa unaongezeka kwa 7% badala ya 4% ya sasa; mzunguko wa fedha mtaani ulikuwa mkubwa na sekta binafsi ambayo ndiyo injini ya uchumi haikuwa inapigwa vita waziwazi. TIC ilikuwa inasajili miradi mipya ya uwekezaji karibu 1000 kwa mwaka tofauti na sasa ambapo inasemekana ni kama 200! Ajira zilikuwepo kila mwaka na watumishi wa serikali walipata nyongeza zao za kisheria za kila mwaka na kupandishwa madaraja. Tukirudi hapo tulipokuwa awamu ya nne siyo haba.
Hilo la kusema mtu ninayemjua in and out kama Zitto kuwa ni ''giant'' wa siasa limefanya nicheke lakini baadae nikasikitika sana kwani kuna mawili. Kama wewe siyo Zitto in disguise basi nakuhurumia sana kwani hujawajua wanasiasa wewe.
 
Umeandika ukweli ambao mimi wala sina shaka nao. Na ndipo ilipo shida kubwa, i.e. kila utawala unaingia na madoido na mapungufu yake. Ukiondoka anayefuatia nae anaingia na yake. Shida kubwa mimi sidhani kama ni CCM. Naomba usinielewe vibaya siyo kuwa nasema ni nzuri. Ila shida kubwa ni sisi wananchi wa Tanzania. Hatutaki na tuu waoga mno kuwasimamia viongozi wetu. Kiongozi anafanya madudu lakini sisi tunakaa kimya na kuchekelea kama tunaangalia movie nzuri. Si wasomi si wakulima. Nikupe mfano: Makonda ameshafanya na kutenda mambo mabaya sana ambayo yanakiuka kanuni za uongozi lakini jiji lenye ''wajanja'' kama Dar wanakubali kuswagwa kama ng'ombe! Kwa nini tunashindwa kumwonyesha aliyemteua kuwa huyu mtu hatufai? Unajua nchi ikiwa na wanachi wanaojielewa inaweza kuwa na viongozi wazuri sana hata kama inataliwa na chama kimoja kwa muda mrefu kama CCM? La muhimu ni wananchi kukemea kila uovu unaofanywa bila kujali vyama.


Tatizo ni mfumo si watu , kwani hakuna waliojitokeza kuchunguza ili kutoa taarifa kwa umma , mwisho wao ulikuwa wapi ?? Ndio ukaona watu wanaogopa au utamalizikia kuwa Gaidi au kutupwa COCO Beach kwenye mfuko uliopigwa marufuku wa Plastiki
 
Umeandika ukweli ambao mimi wala sina shaka nao. Na ndipo ilipo shida kubwa, i.e. kila utawala unaingia na madoido na mapungufu yake. Ukiondoka anayefuatia nae anaingia na yake. Shida kubwa mimi sidhani kama ni CCM. Naomba usinielewe vibaya siyo kuwa nasema ni nzuri. Ila shida kubwa ni sisi wananchi wa Tanzania. Hatutaki na tuu waoga mno kuwasimamia viongozi wetu. Kiongozi anafanya madudu lakini sisi tunakaa kimya na kuchekelea kama tunaangalia movie nzuri. Si wasomi si wakulima. Nikupe mfano: Makonda ameshafanya na kutenda mambo mabaya sana ambayo yanakiuka kanuni za uongozi lakini jiji lenye ''wajanja'' kama Dar wanakubali kuswagwa kama ng'ombe! Kwa nini tunashindwa kumwonyesha aliyemteua kuwa huyu mtu hatufai? Unajua nchi ikiwa na wanachi wanaojielewa inaweza kuwa na viongozi wazuri sana hata kama inataliwa na chama kimoja kwa muda mrefu kama CCM? La muhimu ni wananchi kukemea kila uovu unaofanywa bila kujali vyama.
Upo sahihi. Ukiwa huru kiitikadi utaona mapungufu mengi.
 
Nchi yetu bado kuna adui ujinga anaendelea kutamalaki.

Kunawatu hawaelewi hata maana ya ajira rasmi wao wanachojua ni kula ,kuvaa na kulala tu. Yaliyosalia hayawahusu.

Asilimia kubwa ya wapiga kura hawana smartphones hivyo hizi Mada za kina Zitto wala haziwafikii .
 
Tatizo ni mfumo si watu , kwani hakuna waliojitokeza kuchunguza ili kutoa taarifa kwa umma , mwisho wao ulikuwa wapi ?? Ndio ukaona watu wanaogopa au utamalizikia kuwa Gaidi au kutupwa COCO Beach kwenye mfuko uliopigwa marufuku wa Plastiki
Mkuu ndipo lilipo tatizo basi. Woga! Mmoja akipotea tukijitokeza kwa malaki kuulizia yuko wapi kesho hatapotea tena mwingine. Unafanya kosa kubwa kufikiri atakuja kuingia kiongozi atakayebadili mfumo bila kusimamiwa na watu. Wakati wa Kikwete mnayemsifia na kusema alijali demokrasia mbona kina Dr Ulimboka walifanyiziwa. Tatizo kubwa ni kuwa wale wanaopenya na kushika nafasi za juu wengi wao wana malengo mengine. Mara nyingi mfumo haurusu mtu mwenye nia njema kushika uongozi. Mara nyingi ni wale wabaya tu japo kuna exceptions mara chache.
 
Back
Top Bottom