Rungwe88
JF-Expert Member
- Jul 12, 2013
- 307
- 610
Mataifa mbalimbali duniani kama Marekani, Umoja wa Ulaya, Ghana, Africa Kusini, Australia, Kenya n.k wameonesha kusikitishwa na vitendo haramu kama ubakaji, utekaji, mauaji, ufiraji, kesi haramu za kisiasa, uvunjwaji mkubwa wa haki za kidemokrasia n.k vilivyofanywa na utawala uliopo nchini Tanzania ukiongozwa na samia.
Hivyo kwa wakati tofauti Mataifa mbalimbali duniani yameonesha kusikitishwa kwa vitendo hivyo na kutoa nyaraka mbalimbali kulaani vitendo hivyo zidi ya raia watanzania.
Kwa upande mwingine mataifa hayo yamekubaliana kwamba kuandamana ni sehemu ya haki za msingi za kiraia kuonesha hisia, mawazo, kupinga maovu n.k kwenda utawala husika.
Kwa maana hiyo mataifa mbalimbali duniani yameonesha kuunga mkono maandamano yaliyofanywa na watanzania kuanzia tarehe 29 oct na hata katiba ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 inaainisha kwamba maandamano ni moja ya haki ya msingi ya mwananchi.
Mtanzania hiyo ndio fursa adhimu uliyopata kuikomboa kutoka kwa hao mafisadi, waporaji, watekaji, wauaji n.k
Hivyo unatakiwa kuandamana kwa amani popote pale ulipo ukiungana wa watanzania wenzako nchini kote pia tukumbuke kwamba madhara ya utawala huu haramu uliopo unaoongozwa na samia kama utekaji, mauaji, ufisadi, huduma mbovu za jamii n.k tunapata watanzania wote bila kujali mkoa uliopo, dini, kabila lako n.k maana yake tuwe na maandamano ya amani bila kubaguana kidini, kikabila, mkoa n.k
Mikoa yote unganeni kuikomboa nchi yetu, mataifa mbalimbali duniani Sasa macho yao yote yapo Tanzania na wakiona nia ya dhati kwa kuonesha Umoja wa kukataa utawala huu haramu nao watatumia maandamano hayo ya tarehe 9/12 kama kete muhimu ya kuondoa utawala huu haramu.
Tunaipongeza mikoa kama Dar es salaam, Mbeya, Arusha, Mwanza, Shinyanga, Songwe, Mara, Geita, Dodoma, Kilimanjaro, Ruvuma, Iringa n.k kwa kuwa viongozi Bora katika maandamano ya tarehe 29 oct na mwamko wa tarehe 9/12 uwe mkubwa zaidi.
Wito kwa mikoa kama Tanga, Lindi, Mtwara, Morogoro, Singida, Tabora, Kigoma, Kagera, Katavi n.k unganeni na watanzania wenzenu kuikomboa nchi yetu nzuri sababu matatizo yanayoletwa na utawala huu haramu tunapata sote bila kubagua mikoa tuliopo.
Zifuatazo ndio documents zilizotoka kimataifa kukubali maandamano yanayopangwa kufanywa tarehe 9/12.
Karibuni tukomboe nchi yetu kwa uhuru wa mara ya pili
Hivyo kwa wakati tofauti Mataifa mbalimbali duniani yameonesha kusikitishwa kwa vitendo hivyo na kutoa nyaraka mbalimbali kulaani vitendo hivyo zidi ya raia watanzania.
Kwa upande mwingine mataifa hayo yamekubaliana kwamba kuandamana ni sehemu ya haki za msingi za kiraia kuonesha hisia, mawazo, kupinga maovu n.k kwenda utawala husika.
Kwa maana hiyo mataifa mbalimbali duniani yameonesha kuunga mkono maandamano yaliyofanywa na watanzania kuanzia tarehe 29 oct na hata katiba ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 inaainisha kwamba maandamano ni moja ya haki ya msingi ya mwananchi.
Mtanzania hiyo ndio fursa adhimu uliyopata kuikomboa kutoka kwa hao mafisadi, waporaji, watekaji, wauaji n.k
Hivyo unatakiwa kuandamana kwa amani popote pale ulipo ukiungana wa watanzania wenzako nchini kote pia tukumbuke kwamba madhara ya utawala huu haramu uliopo unaoongozwa na samia kama utekaji, mauaji, ufisadi, huduma mbovu za jamii n.k tunapata watanzania wote bila kujali mkoa uliopo, dini, kabila lako n.k maana yake tuwe na maandamano ya amani bila kubaguana kidini, kikabila, mkoa n.k
Mikoa yote unganeni kuikomboa nchi yetu, mataifa mbalimbali duniani Sasa macho yao yote yapo Tanzania na wakiona nia ya dhati kwa kuonesha Umoja wa kukataa utawala huu haramu nao watatumia maandamano hayo ya tarehe 9/12 kama kete muhimu ya kuondoa utawala huu haramu.
Tunaipongeza mikoa kama Dar es salaam, Mbeya, Arusha, Mwanza, Shinyanga, Songwe, Mara, Geita, Dodoma, Kilimanjaro, Ruvuma, Iringa n.k kwa kuwa viongozi Bora katika maandamano ya tarehe 29 oct na mwamko wa tarehe 9/12 uwe mkubwa zaidi.
Wito kwa mikoa kama Tanga, Lindi, Mtwara, Morogoro, Singida, Tabora, Kigoma, Kagera, Katavi n.k unganeni na watanzania wenzenu kuikomboa nchi yetu nzuri sababu matatizo yanayoletwa na utawala huu haramu tunapata sote bila kubagua mikoa tuliopo.
Zifuatazo ndio documents zilizotoka kimataifa kukubali maandamano yanayopangwa kufanywa tarehe 9/12.
Karibuni tukomboe nchi yetu kwa uhuru wa mara ya pili