Kibunango
Platinum Member
- Aug 29, 2006
- 8,531
- 2,490
Unaweza kuangalia tatizo hili kupitia kwenye mfumo wa uundwaji wa Halmashauri zetu na uwajibikaji wake....so kazi ya mbunge/diwani ni kuwabana,na kama amefanya hivyo na bado hamna kilichofanyika nani alaumiwe ? Hapo ndo tunapishana mtazamo na zembwela yeye anatupa lawama kwa mbunge/diwani wakati si kazi yake. Tukienda mbali zaidi hiki ndo chanzo cha rushwa,mfuko wa jimbo na serikali kutojali kauli za wabunge maana inajua haitawajibishwa kwa makosa yake bali mbunge ndo atawajibishwa kwa kosa ambalo kimsingi ni la serikali...
Shughuli za Halmashauri zinafanywa kupitia vikao vyake. Kwa mfano mkutano mkuu wa Halmashauri, katibu wake huwa ni Mkurugenzi wa Halmashauri. Vikao vya kawaida vya Halmashauri hizo katibu wake huwa ni Mkuu wa Idara. Mkurugenzi wa Halmashauri ni cheo cha kuteuliwa na Rais... Aidha kwa wakuu wa idara nao wanateuliwa toka serikalini. Hapa ndio walakin unapoanzia.
Hivyo basi labda tuanzie hapa na kuona je kuna wakurugenzi wenye kudharau maelekezo ya madiwani wao kwa sababu tu ni wateuliwa wa Rais, na kwa namna moja ama nyingine hawawajibiki moja kwa moja kwa Madiwani?
Je kimefanyika nini ili kuona kuwa Mkurugenzi wa Halmashauri anachaguliwa na Madiwani, ili aweze kuwajibika moja kwa moja kwa Madiwani hao na sio venginevyo?