Zembwela acha upotoshaji...!

Zembwela acha upotoshaji...!

...yes anaweza kufanya hayo lakini asipotoshe jamii kwa uelewa wake mdogo ktk jambo husika,na huu ndo ugomvi wangu na zembwe...

asante sana. Kwa upeo wako mkubwa, nini dhumuni la kuwa na diwani au mbunge? Kazi zao katika jamii ni nini?
 
...yes anaweza kufanya hayo lakini asipotoshe jamii kwa uelewa wake mdogo ktk jambo husika,na huu ndo ugomvi wangu na zembwe...

unaizungumziaje huu mfano wa maranguoriginal? Je! Wananchi wa upande wa pili wasihoji kwa diwani wao?

madiwani lazima waulizwe kwa mfano nipo hapa mbezi beach lakini upande wa juu maeneo kama unakuja five star hall ni diwani wa chadema hakuna maendelo kwake miundo mbinu yake ni mibovu. upande wa chini ni diwani wa ccm kuna miundo mbinu mizuri sana,madiwani wengi wa chadema na wabunge wao hawajafanya kitu kabisa tangu wawe madarakani
 
Mleta mada atakuwa ni moja ya madiwani walioshindwa kuwaletea maendeleo wananchi.

...hahahaaa dah ! mkuu,do i sound like a politician..?no way man,dogo zembwe amepotosha jamii kuhusu haya mambo kwa muda mrefu. Na jambo kama hilo lisiposemewa litaleta tatizo kwa taifa maana watu wengi hawaumizi vichwa kudigest mambo muhimu kama haya...
 
unaizungumziaje huu mfano wa maranguoriginal? Je! Wananchi wa upande wa pili wasihoji kwa diwani wao?

...kila kiongozi wa umma anawajibika kutoa ufafanuzi wa hoja na mambo aliyotumwa na wananchi. Concern yangu ni kuwa tuwawajibishe kwa vigezo na si kwakuwa yeye ni mbunge/diwani. Mfano ulioleta kwanini majimbo ya upinzani tu ndo yatelekezwe ?unadhani ni hujuma ya ccm au madiwani wazembe ?huwezi kupata jibu la haraka kama ambavyo ungemuuliza zembwela angesema timua madiwani wote ndo wazembe. Kumbe hao wa ccm wamekwapua mihela ya epa na wakaja kuitumia....
 
asante sana. Kwa upeo wako mkubwa, nini dhumuni la kuwa na diwani au mbunge? Kazi zao katika jamii ni nini?

...kwa kifupi ni sauti ya wananchi wa jimbo na kutunga sheria. Lakini msingi wa madi yangu ni je ni sahihi kwa mbunge/diwani kubeba lawama kwa kila jambo ambalo halijatimia kama alivyoahidi...?
 
...kwa kifupi ni sauti ya wananchi wa jimbo na kutunga sheria. Lakini msingi wa madi yangu ni je ni sahihi kwa mbunge/diwani kubeba lawama kwa kila jambo ambalo halijatimia kama alivyoahidi...?

inaweza ikawa ndiyo. Kama kuna tatizo ambalo linatakiwa kufanyia kazi kwa uharaka na mbunge amekaa kimya kwa nini asilalamikiwe? Na je hiyo uliyoiita sauti ya wananchi imesimama badala ya nini?
 
Acha kupanic huo Mfano nimeutoa kuoonesha kuwa Zembwela yuko sawa na Kazi ya mbunge ni kuhishinikiza serikali kuahakikisha maendeleo yana patikana na hakishindwa yeye ndiye wa kwanza kupewa lawama!

Mnyika Swala la maji limemshinda na bahati mbaya hawezi kurudi bungeni Tena!

Hivi Mnyika au Mbunge anapokea kodi? Serikali ndiyo yenye wajibu wa kuhakikisha maji, barabara, huduma za afya, elimu, umeme na huduma zote za jamii zinatufikia watanzania. Mbunge kazi yake kubwa ni kuishinikiza , kuisimamia serikali na si jukumu la mbunge kuleta maendeleo ya jimbo. Na jukumu letu wananchi ni kumsaidia mbunge kutekeleza ahadi zake kwa kuilazimisha utekelezaji wa ahadi zake. Je wewe , mim na yeyei tumetekeleza wajibu wetu? Au tunawasubiria Wabunge tu?
 
Acha kupanic huo Mfano nimeutoa kuoonesha kuwa Zembwela yuko sawa na Kazi ya mbunge ni kuhishinikiza serikali kuahakikisha maendeleo yana patikana na hakishindwa yeye ndiye wa kwanza kupewa lawama!

Mnyika Swala la maji limemshinda na bahati mbaya hawezi kurudi bungeni Tena!


Serikali kutambua matatizo au mahitaji ya wananchi kupitia Wabunge na Madiwani ni jambo moja,utekelezaji ni jambo lingine.Hakuna Diwani au Mbunge atakaeweza kuilazimisha Serikali impe pesa au itoe pesa kwa ajili ya mahitaji ya jimbo fulani sasa unaposema Zemb
ela yupo sahihi ni kwa hoja gani?.Juzi nilishuhudia Waziri akiwahimiza wananchi wasivichague vyama vya upinzani kwa sababu havipo Serikalini hivyo haviwezi kuwaletea wananchi maendeleo ,kauli kama hizi nnaona ndio zinawapoteza wananchi walio wengi ambao hushangilia tu na sio kupima kauli na kuzitafakari.Zembwela hayupo sahihi ni mropokaji na ukipiga simu katika kipindi chake na akakuona umem’bana kwa hoja huwa anaongea sana na kutokukupa nafasi na hukukatia simu juu kwa juu.Mimi hilo nimewahi kukumbana nalo na nimemdharau sana.
 
inaweza ikawa ndiyo. Kama kuna tatizo ambalo linatakiwa kufanyia kazi kwa uharaka na mbunge amekaa kimya kwa nini asilalamikiwe? Na je hiyo uliyoiita sauti ya wananchi imesimama badala ya nini?

...msingi wa mada ni je ni sahihi kushusha lawama kwa hawa viongozi kwa kila jambo.?sikusema wasiwajibike...
 
Yaani unapoteza muda Kumsikiliza huyo mtangazaji kanjanja., huyo jamaa simskkilizagi hata siku Moja., yaani huyo na kibonde wote sawa tu.eti mtangazaji anaanzisha story, anaeleezea., anatoa conclusion.
 
Back
Top Bottom