Zawadi ya baba mkwe imenitokea puani!

HorsePower

JF-Expert Member
Aug 22, 2008
3,612
2,566
Miaka kadhaa nyuma, nilimpata binti mmoja wa kunifaa kwenye maisha nikaamua kufunga naye ndoa. Tukio hili lilitokea takriban miaka kumi na mbili iliyopita nyuma.
Harusi yetu, haikuwa ndogo kwa wakati huo, mamia ya watu walihudhuria na zawadi kem kem tulipewa. Mojawapo ya zawadi ilikuwa ni kiwanja ambacho baba mkwe alituzawadia mbele ya hadhara.

Baada ya harusi, nilifanikiwa kujenga nyumba kubwa kwenye kiwanja hicho cha zawadi kwa ushirikiano na mke wangu. Baada ya nyumba kukamilika, sisi tulikuwa tunaendelea kuishi kwenye nyumba ambayo ilikuwa inalipiwa na shirika maeneo ya Oysterbay. Baba mkwe alistaafu na kuomba kukaa kwenye nyumba yetu kwa miezi michache wakati akimalizia ya kwake maeneo ya mbezi. Mimi na mke wangu bila hiyana, tukawakubalia wazee wetu wakae kwenye nyumba yetu kwa muda ma miaka 3 bure huku wakimalizia ujenzi wao.

Ndugu zangu, sasa yapata miaka 7 baba mkwe na mkewe hawataki kutoka kwenye nyumba yetu kwa kisingizio kuwa kiwanja ni chao na sisi tumejengwa kwenye kiwanja chao. Kinachoshangaza ni kuwa mpaka mikanda ya video ya harusi yetu nilishawahi kumuonyesha akitukabidhi hati za kiwanja kama zawadi, lakini mzee huyu katugeuka kabisa akishirikiana na baadhi ya watoto wake.

Kamtenga mke wangu-ambaye amekuwa karibu sana na mimi katika hili, na pia hataki hata kumuona na mimi kanizushia mambo kibao mabaya yasiyo ya kweli, naomba ushauri ndugu zangu nimtende nini mzee wangu maana na mimi nataka kuhamia kwenye hiyo nyumba na yeye hataki kutoka na nyumba yake keshamaliza! Hati ya kiwanja ninayo mimi maana alitukabidhi siku ya harusi.

Kosa langu ni nini, na nimfanyaje huyu mzee? Nimtoe kwa nguvu? Nahisi zawadi yake imenitokea puani!

***** Ombi hili la ushauri limetumwa na rafiki yangu mmoja toka Dodoma akiomba tumsaidie mawazo. Halina uhusiano na maisha yangu binafsi ***

Wenu

HorsePower
 
Unajua hakuna tensions mbaya kama za kifamilia....huwa hazina ukomo.....namuonea huruma''shemeji'' yetu kususwa na baba yake.....si kitu kizuri pamoja na wehu wa huyo mzee na familia yake........ni bora kurudisha hayo mahusiano japo kwa machalemachale kuliko kuendeleza bifu......akimtoa kwa mahakama itakuwa mbaya sana........am sorry....kujenga lilikuwa kosa kubwa....wengi yamewakuta ndio maana mimi niliuza cha Mikocheni nikanunua Bunju
 
Pole sana lakini hakuna cha kufanya zaidi ya kukubali matokeo.
Baba mke noma kakupiga tobo.
OTIS
 
hapo nahisi mahakama inahusika kumtoa huyo mzee

unalosema sawa lakini kumbuka kesi ni ya baba wa mkeo.........nafikiri ndugu wa karibu wanatakiwa kushirikishwa na kuweza kuliongea kifamilia hata itakapofikia kuwa la kisheria angalau ndugu wa pande zote watakuwa wanaelewa nini kinachoendelea na lawama za upande mmoja hazitakuwepo......mpe pole sana maana imemkalia vibaya sana

 
unalosema sawa lakini kumbuka kesi ni ya baba wa mkeo.........nafikiri ndugu wa karibu wanatakiwa kushirikishwa na kuweza kuliongea kifamilia hata itakapofikia kuwa la kisheria angalau ndugu wa pande zote watakuwa wanaelewa nini kinachoendelea na lawama za upande mmoja hazitakuwepo......mpe pole sana maana imemkalia vibaya sana


Hili nalo neno!
 
Lakini si ameshapewa hati ya kumiliki, ina maana yeye ndio mmiliki halali wa kiwanja kile. Aende tu mahakamani na hati miliki anayo.
 
Lakini si ameshapewa hati ya kumiliki, ina maana yeye ndio mmiliki halali wa kiwanja kile. Aende tu mahakamani na hati miliki anayo.

Nina hakika hakufanya transfer........angekuwa ameifanys huyo Mzee asingepata jeuri......mimi waliponikabidhi tu nikafanya transfer halafu nikapiga bei......hela niliyoipata nikanunu kiwanja na kujenga
 
Shirikisha ndugu wa pande zote mbili, nina imani miongoni mwao kuna wenye busara. Ikishindikana, mwambie Baba mkwe akulipe gharama ya nyumba ukiondoa kiwanja, ikishindikana mwachie kila kitu, kumbuka mali hutafufutwa kwa maana hiyo utapata nyingine. Kama ukimwondoa kwa nguvu ya mahakama, utajenga uadui wa kudumu baina yako na wewe.
 
ulivyofanya ulifanya poa kumsaidia makaz huy mzee ila da anavyofanya ni kama hakuna dili la kukudhurum hiy nyumba ashapanga kitambo ,so kama ni aje acha uoga mpeleke mahakaman ili kama anangangania nyumba akulipe, gharama za ujenzi wako umwachie nyumba na kiwanja chake au we unamuonea aibu
icon5.png
 
Hamia kwenye nyumba ya mzee. Kiukweli busara inahitajika, hawa wazee wanajua sana kuzusha na wanajamii watawasikiliza wao kwanza na kuwaona nyinyi matapeli.
 
Peleka mahakamani au alipe gharama za ujezi kwa thamani ya sasa. Ama utaula wa chuya....
 
apeleke tinga tinga abomoe abebe tofali zake awaachie kiwanja
......................................


seriously,
nyumba kitu gani? mwisho wa siku wote wataishia kaburini....

kama ana uwezo ajenge nyingine, akae na mkewe, apunguze mahusiano ya karibu na ndg wa mkewe maana hawana nia njema


na kama ni lazima sana kupata hiyo nyumba/jasho lake....

je hati aliibadilisha jina ipo kwenye jina lake na mkewe?
kama walibadilisha atafute wanasheria wajue nini cha kufanya kupata jasho lake ili hata wakiitwa watoto wao wabaki na nyumba
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom