Zawadi ya baba mkwe imenitokea puani!

Jukwaa la sheria ungepata msaada zaidi, sielewi kwa nini umeprefer kuileta MMU, au kwa kuwa kisa kilianzia kwenye sherehe ya ndoa?
 
Unajua hakuna tensions mbaya kama za kifamilia....huwa hazina ukomo.....namuonea huruma''shemeji'' yetu kususwa na baba yake.....si kitu kizuri pamoja na wehu wa huyo mzee na familia yake........ni bora kurudisha hayo mahusiano japo kwa machalemachale kuliko kuendeleza bifu......akimtoa kwa mahakama itakuwa mbaya sana........am sorry....kujenga lilikuwa kosa kubwa....wengi yamewakuta ndio maana mimi niliuza cha Mikocheni nikanunua Bunju

Duh! What an eye opener that is? Thanks Comrade!
 
miaka kadhaa nyuma, nilimpata binti mmoja wa kunifaa kwenye maisha nikaamua kufunga naye ndoa. Tukio hili lilitokea takriban miaka kumi na mbili iliyopita nyuma.
Harusi yetu, haikuwa ndogo kwa wakati huo, mamia ya watu walihudhuria na zawadi kem kem tulipewa. Mojawapo ya zawadi ilikuwa ni kiwanja ambacho baba mkwe alituzawadia mbele ya hadhara.

Baada ya harusi, nilifanikiwa kujenga nyumba kubwa kwenye kiwanja hicho cha zawadi kwa ushirikiano na mke wangu. Baada ya nyumba kukamilika, sisi tulikuwa tunaendelea kuishi kwenye nyumba ambayo ilikuwa inalipiwa na shirika maeneo ya oysterbay. Baba mkwe alistaafu na kuomba kukaa kwenye nyumba yetu kwa miezi michache wakati akimalizia ya kwake maeneo ya mbezi. Mimi na mke wangu bila hiyana, tukawakubalia wazee wetu wakae kwenye nyumba yetu kwa muda ma miaka 3 bure huku wakimalizia ujenzi wao.

Ndugu zangu, sasa yapata miaka 7 baba mkwe na mkewe hawataki kutoka kwenye nyumba yetu kwa kisingizio kuwa kiwanja ni chao na sisi tumejengwa kwenye kiwanja chao. Kinachoshangaza ni kuwa mpaka mikanda ya video ya harusi yetu nilishawahi kumuonyesha akitukabidhi hati za kiwanja kama zawadi, lakini mzee huyu katugeuka kabisa akishirikiana na baadhi ya watoto wake.

Kamtenga mke wangu-ambaye amekuwa karibu sana na mimi katika hili, na pia hataki hata kumuona na mimi kanizushia mambo kibao mabaya yasiyo ya kweli, naomba ushauri ndugu zangu nimtende nini mzee wangu maana na mimi nataka kuhamia kwenye hiyo nyumba na yeye hataki kutoka na nyumba yake keshamaliza! Hati ya kiwanja ninayo mimi maana alitukabidhi siku ya harusi.

Kosa langu ni nini, na nimfanyaje huyu mzee? Nimtoe kwa nguvu? Nahisi zawadi yake imenitokea puani!

***** ombi hili la ushauri limetumwa na rafiki yangu mmoja toka dodoma akiomba tumsaidie mawazo. Halina uhusiano na maisha yangu binafsi ***

wenu

horsepower

nenda mahakamni maana mkwewe kawa mkora!! Unless usamehe tu na wewe umpe zawadi!!
 
Msaidie kumalizzia nyumba yake then msaidie kuhama,au mlazimishe kuhama kwa kuhamia hapo kwake wewe na familia yako....!

Watu wengine wanatoa zawadi kwenye harusi kutafuta umaarufu tu,nao waonekane wazazi bora.
 
Mkuu pole! Msikilize mkeo mkubaliane mnafanyaje maana hukusema mkeo analichukuliaje hili na pia mkumbuke kuna radhi ya baba yake
 
Hapo imekula kwa mshkaji, akubali tu yaishe kwamba ni sehemu ya mahari. Kwani kuna ubaya gani kuwajemgea wakwe zako nyumba? Hata akienda mahakamani bado itakula kwake, mzee huyo ni mzoefu atakuwa keshajiandaa. Ushahidi wa video ya harusi utatupiliwa mbali maana hiyo hati itakuwa haisomeki kwenye video, na mzee anaweza kusema siyo hiyo aliyokupa, na kwamba ile shamba aliyokupa uliikataa au akatunga uongo mwingine wowote.
 
hapo pagumu..kama we kauzu mpeleke mahakamani kama unamwonea huruma peleka kesi kwa wazee wenzake wawasaidie...au alipe gharama ulizotumia kujenga nyumba

Unamaanisha nini kusema kama wewe ni kauzu peleka mahakamani?
 
Hapo imekula kwa mshkaji, akubali tu yaishe kwamba ni sehemu ya mahari. Kwani kuna ubaya gani kuwajemgea wakwe zako nyumba? Hata akienda mahakamani bado itakula kwake, mzee huyo ni mzoefu atakuwa keshajiandaa. Ushahidi wa video ya harusi utatupiliwa mbali maana hiyo hati itakuwa haisomeki kwenye video, na mzee anaweza kusema siyo hiyo aliyokupa, na kwamba ile shamba aliyokupa uliikataa au akatunga uongo mwingine wowote.


Sheria za nchi gani hiyo? Kakwambia hati anayo, sasa itkulaje kwake na uongo gani utakaotungwa na baba mkwe ili kufuta hati?
 
Sheria za nchi gani hiyo? Kakwambia hati anayo, sasa itkulaje kwake na uongo gani utakaotungwa na baba mkwe ili kufuta hati?
Hati ina jina la baba mkwe, na hakuna ushahidi wa kumwezesha kufanya transfer, zaidi ya hiyo video ya harusi. Kwa sababu ukitaka kufanya transfer ya hati lazima kuwe na ushahidi mfano mkataba wa mauziano, hati ya mirathi, tamko la donation nk (zote kutoka mmiliki wa awali pamoja na picha zake), sasa hapo kama tayari kuna bifu la kiwango hiki bado huoni imekula kwake?
 
huyo mzee ni mwizi, hy jamaa afanye mpango apate hati ya nyumba yenye jina lake dhen akachukue mkopo wa kutosha benk hlf asilipe
 
Sikuhizi ukipewa zawadi ya vitu visivyo hamishika kwenye sherehe angalia mtu anaye kupa asije akawa amepiga maja a.k.a pombe huwa ahidi yy bali nipombe ndiyo huwa inamuongoza kesho yake hujutia.
 
Hati ina jina la baba mkwe, na hakuna ushahidi wa kumwezesha kufanya transfer, zaidi ya hiyo video ya harusi. Kwa sababu ukitaka kufanya transfer ya hati lazima kuwe na ushahidi mfano mkataba wa mauziano, hati ya mirathi, tamko la donation nk (zote kutoka mmiliki wa awali pamoja na picha zake), sasa hapo kama tayari kuna bifu la kiwango hiki bado huoni imekula kwake?

Kakwambia hakufanya transfer au hati ipo kwenye jina la baba mkwe, au wewe ndio assumptions zako?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom