Zawadi ya baba mkwe imenitokea puani!

Machale HAYAKUKUNDECHA MEKU!!!!!!!!!!!!!ilitakiwa ubadilishe deed of transfer aisee.BIASHARA KWISHNE.tujipange utafte kingine ujenge.KIFUATACHO ITV UNAKIJUA......?
 
mmmh! huyo baba mkwe kigeugeu...kama vip mwachie kiwanja chake afu muuzie hiyo nyumba
 
Sasa ndio umekuwa mwanaume, sio mbaya kumjengea mkweo nyumba.
Jipange, nunua eneo sehemu nyingine kisha jenga nyumba nyingine
Miaka kadhaa nyuma, nilimpata binti mmoja wa kunifaa kwenye maisha nikaamua kufunga naye ndoa. Tukio hili lilitokea takriban miaka kumi na mbili iliyopita nyuma.
Harusi yetu, haikuwa ndogo kwa wakati huo, mamia ya watu walihudhuria na zawadi kem kem tulipewa. Mojawapo ya zawadi ilikuwa ni kiwanja ambacho baba mkwe alituzawadia mbele ya hadhara.

Baada ya harusi, nilifanikiwa kujenga nyumba kubwa kwenye kiwanja hicho cha zawadi kwa ushirikiano na mke wangu. Baada ya nyumba kukamilika, sisi tulikuwa tunaendelea kuishi kwenye nyumba ambayo ilikuwa inalipiwa na shirika maeneo ya Oysterbay. Baba mkwe alistaafu na kuomba kukaa kwenye nyumba yetu kwa miezi michache wakati akimalizia ya kwake maeneo ya mbezi. Mimi na mke wangu bila hiyana, tukawakubalia wazee wetu wakae kwenye nyumba yetu kwa muda ma miaka 3 bure huku wakimalizia ujenzi wao.

Ndugu zangu, sasa yapata miaka 7 baba mkwe na mkewe hawataki kutoka kwenye nyumba yetu kwa kisingizio kuwa kiwanja ni chao na sisi tumejengwa kwenye kiwanja chao. Kinachoshangaza ni kuwa mpaka mikanda ya video ya harusi yetu nilishawahi kumuonyesha akitukabidhi hati za kiwanja kama zawadi, lakini mzee huyu katugeuka kabisa akishirikiana na baadhi ya watoto wake.

Kamtenga mke wangu-ambaye amekuwa karibu sana na mimi katika hili, na pia hataki hata kumuona na mimi kanizushia mambo kibao mabaya yasiyo ya kweli, naomba ushauri ndugu zangu nimtende nini mzee wangu maana na mimi nataka kuhamia kwenye hiyo nyumba na yeye hataki kutoka na nyumba yake keshamaliza! Hati ya kiwanja ninayo mimi maana alitukabidhi siku ya harusi.

Kosa langu ni nini, na nimfanyaje huyu mzee? Nimtoe kwa nguvu? Nahisi zawadi yake imenitokea puani!

***** Ombi hili la ushauri limetumwa na rafiki yangu mmoja toka Dodoma akiomba tumsaidie mawazo. Halina uhusiano na maisha yangu binafsi ***

Wenu

HorsePower
 
Fanya hili! wahusihe ndugu na jamaa wa karibu na mzee! waeleze the A,B,C na maamuzi ya nini kifanyike kama mzee ataendelea kukatalia kwenye nyumba hiyo yatokane na vikao vya kifamilia hakikisha hiyo resolution inafikiwa, maana you have a strong case and it is against mzee. una hati ya nyumba na una mkanda wa video! Ukisha pata baraka za vkao halali vya familia mpeleke mahakamani! Msikubali kuwa wanyonge kwa kisingizio cha baba mkwe, mama nae anasema baba! Mzee ananyumba yake ya kuishi na hiyo ni ushadi tosha kwamba ana taamaa ama anakufanyia jeuri
 
Poleni sana ndugu, Hebu piga magoti umwombe Mungu kama unaamini kwamba ndiye Muumba wa mbingu na nchi.
Naamini inawezekana kilainisha moyo wake kwa sala kabla hajaenda mahakamani. Pia usisahau kuwaita wazee wenye busara wa ukoo wake na wako.
 
Dah!mpe pole sana huyo rafiki yako,
Hivi wazee wengine mbona wanawalazimisha watu kupata dhambi kiasi hiki?
Hapo bila busara kutumika familia zitakuwa na uhasama mkubwa,
Namshauri amshukuru mungu na amwachie huyo mzee kila kitu afanye mpango ajenge kengine aishi na mkewe,
Alafu ataona nn mungu atafanya kwake na kwa huyo mzee.
 
Duh! Kazi kweli kweli, huyo mzee ana uchu wa mali, mstaafu, nyumba amemaliza kujenga, ni nini kama si ukorofi? Akutanishe ndugu wa pande zote mbili (wenye busara) waongee kifamilia juu ya jambo hilo, na ikibidi babamkwe arudishe gharama za ujenzi wa hiyo nyumba, la akikataa, aende mahakamani vithibitisho vyote sianavyo? Kujenga ni kazi jamani hata ningekuwa mimi nisingekubali
 
Ndugu yangu pole sana kwa masaibu yaliyokukuta nakushauri utulie kama unao ushaidi wa video ya harusi na ninaamimini kuwa kuna mashuhuda wengi waliokuwepo siku ya harusi wakati ukipewa kiwanja hicho wewe nenda manispaa halafu ardhi na uanze taratibu za kubadili umiliki wa kiwanja hicho kutoka kwa baba mkwe kwenda kwako na mkeo yeye akileta pingamizi toa ushahidi wa video ulio nao. ukishapata hati miliki wewe mwache akae amalize siku zake kwa amani.

ukiona kwamba hutaweza kusubiri mpaka amalize siku zake shauriana na mkeo akikubali muende bank mkachukue mkopo na hiyo nyumba iwe ndiyo collateral mpate fedha mkajenge nyumba sehemu nyingine. pia nashauri usiitegemee tena nyumba hiyo kwa namna yoyote ile maana hata ukiipata kwa kufuata sheria za mahakama ukimwachia mwanao kama urithi bado itamletea matatizo makubwa sana na wajomba zake.

wakwe ni watu wa ajabu sana mimi nimeoa moshi na na naishi DSM shemeji zangu wanaishi kwangu na hata wakwe zangu wenyewe kuna wakati huwa wanakuja kwangu kupumzika au matibabu na baadaye wanaondoka wakati fulani nilikuwa nafikia ukweni ninapokuwa moshi kwani mimi bado nilikuwa sijajenga nyumba moshi kumbe jambo hili likawa haliwafurahishi hata kidogo. wakawa wanalalamika kimya kimya habari hizi ziliponifikia mimi nikatania mbona na wao wakija dar wanafikia kwangu? siku ya siku ndugu yangu nilipewa live nilifika jioni wao walikuwa hawapo nikapaki gari langu nikaingia kwenye room ya mke wangu nikalala wao waliporudi walikuta gari wakafikiri nimetoka nitarudi kumbe nilishalala asubuhi nimeamka nasalimia wanaitikia kwa unyonge na swali juu hivi ulipopaki hili gari hapa bila ruhusa ungeamka ukalikosa ungemuuliza nani? nikajibu kwa upole si ningeanza na wenye mji ambao ndio ninyi mpaka tujue limeenda wapi? uanze na sisi kwani tumekuita hapa? kwa upole niliwaambia basi kwa kuwa aliyenikaribisha huku yupo hapa mke wangu naomba niwaachie na siku mkiniona tena huku kwenu katoeni taarifa polisi - mke wangu aikataa kubaki na tukaondoka mpaka leo huwa naeda huko kamakuna shida ya lazima sana . kifupi tuu ni kwamba usije ukafikiri kwamba ukweni huwa wanafurahi sana wanapoona wewe umepata mke na bado unaaendelea kuneemeka through wao - tafakari na uchukue tahadhari sana ndugu yangu
 
mmh kweli zawad imemtokea puan.
unahitajika uamuz wa busara hapo, la sivyo utatokea mfarakano mmoja balaa.
kama vp amuachie 2 inakuwa kamjengea mkwewe lol, maana kwenda kumshtak au kumtoa hapo kinguvu sio ishuu.
tafakar chukua ha2a madhubutii.
 
hapo pagumu..kama we kauzu mpeleke mahakamani kama unamwonea huruma peleka kesi kwa wazee wenzake wawasaidie...au alipe gharama ulizotumia kujenga nyumba
 
Duu mkuu pole sana.Hata mimi yalikuta,nilipewa kiwanja na babamkwe baada ya harusi kwa kuwa tulikuwa ughaibuni tulimtumia baba mkwe kianzio cha kuanza kujenga,lakini baada muda nilikuja likizo nikamuuliza baba mkwe akanionyeshe kiwanja maana nilikuwa sijakiona ndipo akaniambia amekiuza kwani alipata dharura,nilinyong'onyea kwani hata zile hela nilizotuma kwa maana hiyo hazipo pia.
Sijawahi uliza kitu chochote since,nilichofanya nilimtarifu mwanae yaliyotokea.

Mimi nakushauri kwamba kama unauwezo wa kujenga nyumba nyingine jenga achana na hiyo kwani mkeo utamwacha kwenye wakati mgumu kama utaamua kuchukuka hatua yoyote ile.ILa kama hali ni ngumu basi dai haki yako liwalo na liwe
 
Lakini si ameshapewa hati ya kumiliki, ina maana yeye ndio mmiliki halali wa kiwanja kile. Aende tu mahakamani na hati miliki anayo.
Je alikumbuka kuibadili jina baada ya kupewa? USHAURI WA BURE: Akubali kuwa imekula kwake! na ajipange upya ili kuepuka madhara zaidi.
 
Lakini si ameshapewa hati ya kumiliki, ina maana yeye ndio mmiliki halali wa kiwanja kile. Aende tu mahakamani na hati miliki anayo.
Kama hati imeandikwa kwa jina la yule mzee na haikubadilishwa kuwa na majina ya watoto, hata kwenda mahakani ni kazi bure. Kimsingi washirikishwe ndugu ili swala hili liishe kifamilia. Vinginevyo huyu mzee alipiga hesabu mapema. Hakutoa zawadi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom