Zanzibar Yanusurika Kupinduliwa Mara 14!

Zanzibar Yanusurika Kupinduliwa Mara 14!

Buchanan

JF-Expert Member
Joined
May 19, 2009
Posts
13,192
Reaction score
1,976
SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) ilinusurika majaribio 14 ya kupinduliwa, likiwamo lililosababisha kifo cha muasisi wa Mapinduzi, Sheikh Abeid Amaan Karume, Aprili 7, 1972.

Kwa mujibu wa wazee waliokuwapo wakati wa kuasisiwa kwa Muungano, majaribio hayo yalishindikana na mmoja wa wazee hao, aliyewahi kuwa Katibu wa Kwanza wa Jumuiya ya Vijana ya Chama cha Afro Shiraz, Baraka Mohamed Shamte alisema kama si Muungano, baadhi ya majaribio hayo yangefanikiwa na kungeendelea kutokea mapinduzi zaidi ya mara sita.


“ Kama isingekuwa Muungano, tungepinduana zaidi ya mara sita,” alisema Shamte ambaye pia ni mtoto wa marehemu Muhammad Shamte, aliyekuwa Waziri Mkuu wa Serikali ya Zanzibar iliyopinduliwa.


Alifafanua kuwa wafuasi wa utawala uliopinduliwa uliokuwa chini ya Sultan ambao walikuwa ndani na nje ya Zanzibar, ndio waliofanya majaribio hayo 14 katika kipindi kifupi cha kati ya mwaka 1964 na 1972.

Kwa habari zaidi soma HabariLeo.
 
Sultani alivikalia visiwa vya Zanzibar kwa karne moja, angekubali kunyang'anywa tonge mdomoni hivi hivi?
 
Wakereketwa wa mambo ya Muungano mmeishia wapi?
 
Wanaotaka kuvunjika kwa muungano ni kwa ajili ya kuidhoofisha Zanzibar zaidi! wanajua kabisa kuwa wakiiondoa Zanzibar ni rahisi kuweassert their influence. Lakini siyo influence ya hivi hivi tu ni influence ya utawala. Kwa sababu baada ya kujiondoa guess kitafuata nini.. zitatokea sauti Zanzibar zitakazohoji uhalali wa serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa sababu .. iliondoa "serikali halali ya Sultani".. na wao watataka waiondoe hiyo (ndiyo sababu ya hayao majaribio anayoyazungumzia shamte) ili kurejesha serikali halali iliyoko Uingereza na Oman. Na kwa mara ya kwanza, mtasikia kwa sauti Oman na kina Jamsheed na uzao wake wakianza tena kudai Zanzibar yao..!! yakitokea mapinduzi mengine guess watu watakimbilia wapi? ... Bara! kwa ndugu zao!!! halafu sisi tufanya nini.. watu wa bara watasema "tutawaacha wauane wenyewe kwa wenyewe" right!!!! Tusingeungana kwa haraka vile historia ya Zanzibar ingekuwa ni ya migogoro mikubwa ya kisiasa yenye msingi wa kinasaba kuliko tunavyofikiria..
 
siyo magumu kiasi hicho..

Kama siyo magumu kiasi hicho nini kifanyike basi ili watu (wengi) wa pande zote mbili za Muungano waridhike na muunganiko wao? Maanake some of us have had it up to here with this stupid muungano....
 
siyo magumu kiasi hicho..

Ni magumu ndio maana mpaka leo pamoja na tume 45 zilizokwishaundwa hakuna la maana lililofanyika ni blah blah tu na kupoteza fehda pamoja na muda kwa kuunda tume.kamati zisizokuwa na kichwa wala miguuu...Hii ngoma nzito..
 
Kama siyo magumu kiasi hicho nini kifanyike basi ili watu (wengi) wa pande zote mbili za Muungano waridhike na muunganiko wao? Maanake some of us have had it up to here with this stupid muungano....

Ondoa magugu na kuacha mahindi yakiendelea kustawi, sio kung'oa mahindi pamoja na magugu!
 
Kama siyo magumu kiasi hicho nini kifanyike basi ili watu (wengi) wa pande zote mbili za Muungano waridhike na muunganiko wao? Maanake some of us have had it up to here with this stupid muungano....

soma mojawapo ya makala zangu kesho uone mambo ya kuanzia.. it all start with leadership!! Hatuna viongozi wenye uwezo wa kukabili matatizo na kuyatatua.. wanaogopa kukwaza watu, kuudhi, au kukasirisha watu. We need leaders who are willing and able to offend and defend!
 
soma mojawapo ya makala zangu kesho uone mambo ya kuanzia.. it all start with leadership!! Hatuna viongozi wenye uwezo wa kukabili matatizo na kuyatatua.. wanaogopa kukwaza watu, kuudhi, au kukasirisha watu. We need leaders who are willing and able to offend and defend!
Nitaipitia makala hiyo kesho!
 
wacheni kuzungumza msiyo yajuwa, kwani kabla ya kunganisha hiyo ASP na TANU tulikuwa tunaishi vipi ? mbona hamkuwa na sauti ya kuingilia mamuzi yaliyokuwa yanafanywa wakati ule?na wenywe wazanzibari wanamuliana kwa upendo wa ugu wao wa damu na huruma, fita zote zilianza baada mwaka 1977mara tu baada ya kunganishwa vyama viwili hivi nakumbuka kama leo nikiwa kijana mdogo wa paunia pale Amani Mzee Thabit Kombo alitokwa na machozi kama mtoto kwa kujuwa kuwa tumeruka mapote na tumejingiza ndani ya kinyesi tena changuruwe ,angalau kingekuwa cha ngombe kinatumika kwa mbole ,hatma yake leo ndio hii unakuta watu akina mwanakijiji wamekuwa wao ndio wasemaji wakubwa na wajuwaji wa maswali ya watu wa zanzibar na nini wanataka kataika maisha yao ,leo tumekuwa utu wetu umeondoshwa tumelazimishwa tuishi masiha ya ulahai ambayo hayakuwa ndani ya tamduni zetu imefika hadi leo huwezi kumkaribisha mgeni aliyepotea hata gilasi ya maji ,wacheni nyie wazanzibar hawakuzoweya vya kunyoga .

Hivi Kambarage alitaka kupinduliwa mara ngapi ?
 
wacheni kuzungumza msiyo yajuwa kwani kabla ya kunganisha hiyo ASP na TANU tulikuwa tunaishi vipi ? mbona hamkuwa na sauti ya kuingilia mamuzi yaliyokuwa yanafanywa wakati ule wenywe wazanzibar wanamulianakwa upendo wa ugu wao wa damu fita zote zilianza baada mwaka 1977mara tu baada yakunganishwa vyama viwili hivi nakumbuka kama leo nikiwa kijana mdogo wa paunia pale Amani Mzee Thabit Kombo alitokwa na machozi kwa kujuwa kuwa tumeruka mapote na tumejingiza ndani ya kinyesi tena changuruwe hatima yake ndio hii unakuta watu akina mwanakijiji wamekuwa wao ndio wasemaji wakubwa na wajuwaji wa maswali ya watu wa zanzibar na nini wanataka kataika maisha yao leo tumekuwa utu wetu umeondoshwa tumelazimishwa tuishi masiha ya ulahai ambayo hayakuwa ndani ya tamduni zite inefika leo huwezi kumkaribisha mgeni aliyepotea hata gilasi ya maji ,wacheni nyie wazanzibar hawakuzoweya vya kunyoga .

Hivi Kambarage alitaka kupinduliwa mara ngapi ?

Mkuu usisahau this is the home of great thinkers, just don't please!
 
Back
Top Bottom