Zanzibar strikes again !

Zanzibar strikes again !

Haya kuna ile hadithi ya punda aliyetaka kwenda njia mbili,akaishia kufa.Sasa sijui hawa wenzetu wanataka nini?Wakija bara serikali mbili,wakiondoka serikali tatu.Mh!:shock:😕

Miaka 47 sasa hawatoa Mchango kugharamia Muungano , kumbe pesa wanayo? Kama pesa ipo Mbona hawalipi mishahara watumishi wao?hata posho Zimewashinda? Kila kitu Tanganyika ndio analipia ! Pesa za zenji wamehifadhi kwa ajili ya kununulia dhana za kivita kisha wazitumie kudai Uhuru wa kujitenga.
 
Kumbe Zenji ni wajanja saana wao wanabania pesa Yao kwa na kutumia za Tanganyika zao wanatunza kwa ajili ya kununulia Bunduki ili baadae waje kuzitumia kudai Nchi Yao ! Tanganyika sasa amekuwa buzi anachunwa pasipo kujielewa .
 
Uzuri/ubaya wa haya yote wanayasemea wakiwa Mchambawima, lakini wakifika Dodoma wanaufyata. Hizo kelele za Mchambawima ambazo hata mwangi wake haufika Chumbe, hazitunyimi usingizi.
 
Ni hatari sana Zanzibar ni nchi lakini wananchi wake sio raia ni wakaazi tu, Kuna haja Zanzibar kufanya Mapinduzi makubwa sana kujivua kutoka kwa watanganyika kwa nguvu zote ata kama hawatak. Ni aibu miaka 50 toka uhuru wazanzibar siyo raia ndani ya nchi yao
Keissy aliwaambi nji nyeupee, jhakuna aliyetoka mjengo! Ungewauliza waikuwa wanasubiri nini, na je walihitaji nguvu za kutoka mjengoni kuelekea bandarini.
 
Wazanzibar ni wazuri sana wa kuongea. Badala ya kununua silaha tungependa wasema, ulinzi na usalama si jambo la muungano. Hapo tungewaelewa. Halafu silaha hazinunuliwi na wabunge, ni dalili za kubweka tu. Lini ulisikia ndani ya bunge la JMT wakitangaza vifaa vyao. Hapa hamuoni kuna kubweka tu siku ipite.

Kuhusu Uraia, hili ni zuri sana. Kwanza wanatakiwa wamwambie Seif na wenzake waliokuja Karimjee kurudisha viyambulisho vya NIDA. Halafu watengeneze vyao. Hilo halina shida.

Hata huko nyuma walikuwa na passport, sijui walitupa wapi.
Hakuna aliyewashia bunduki, walizutupa baharini wenyewe.
Waje KIUTA wachapishe mpya, kila la heri.
 
Zanzibar inawatu wenye msimamo na wanajitambua..
 
Wizara hiyo ina wafanyakazi hewa wanaochukua mishahara tu na wasiijuwa kazi zao, wengi sana
 
Baada ya Kuufyata sasa afyetuka baada ya kuzomewa
Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) imeshauriwa kuwa na uraia kwa watu wake pamoja na kuvipa hadhi vikosi vyake maalumu ili viweze kumiliki silaha za kivita chini ya mfumo wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

wakati umefika kwa vikosi vya SMZ kupewa hadhi ya kumiliki silaha za kivita badala ya kumiliki silaha za kawaida kama ilivyo sasa kwa mujibu wa sheria.
ni wakati mwafaka na unaofaa kwa SMZ kununua silaha kama mizinga, vifaru, helikopta za kivita na boti za kijeshi pamoja na silaha nzito kama RPG.

“Huwezi kuwa na nchi bila ya kuwa na raia.” Alitaka Wazanzibari kupewa uraia wao katika mfumo wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na kusema ni jambo la kushangaza Wazanzibari kuitwa wakazi na si raia.
hatua ambayo itaipa hadhi nchi na kutambulika kitaifa na kimataifa.
Mkuu Mwiba, asante kwa hii!.

Maadam hayo ni maoni tuu ya Wawakilishi, yataendelea kubaki ni maoni tuu!.

Maadamu wamezungumzia kwa mujibu wa sheria!, nashauri anzeni na sheria kwanza ndipo utekelezaji ufuate!.

Kwa mujibu wa sheria, Jeshi ni la JMT!, hao wa huko Zanzibar ni vikosi tuu kama migambo au Ultlmate security, mwisho wa uwezo wao kisheria ni kumili silaka ndogo za kujilinda na sio silaha za vita!. Kama mnataka kuvibadili vikosi vigeuke jeshi, anzeni na kuibadili sheria kuwa Zanzibar nayo iwe na jeshi lake!.

Vivyo hivyo kwenye uraia, uraia bi wa Nchi, JMT!, huko Zanzibar ni ukaazi tuu!. Maadam Mwakilishi katamka vizuri, "huwezi kuwa na nchi bila kuywa na raia!", Zanzibar sio nchi, ni sehemu ya JMT hivyo haiwezi kuwa na raia wake!, raia wote ni wa JMT!, ili Zanzibar iweze kuwa na raia wake, inabisi kwanza iwe nchi!m ndipo ipate raia lakini sivyo kama ilivyo sasa ni "nchi jina tuu!" lakini sii nchi lolote!, sii nchi chochote!, ila kama shida yenu ni jina tuu!, then naiwe!, kitambulisho cha ukaazi wa Zanzibar kiitwe "Kitambulisho cha Raia Wa Nchi ya Zanzibar!", kama tulivyokupeni bendera si mnapeperusha!, na wimbo wa taifa si mnapiga!, kujiita raia wa Zanzibar ruksa, ila vifaru, RPG, mizinga ya kujiandaa kupigana vita na nani?.

Enyi waume mnaomiliki silaha!, inapotokea mkeo nae anaomba na yeye amiliki silaha! na nyite mlale nazo chini ya mito kuna usalama kweli hapo?!.

Mke kazi yake ni kula bure, kulala bure, kuvishwa, kupendezeshwa, umeme bure!, mishahara bure na asilimia 4.5 % ya misaada yote bure na nimesikia sasa ajira ni asilimia 21!%, Mungu akupe nini tena!.

Hongereni!.

Pasco
 
Baada ya Kuufyata sasa afyetuka baada ya kuzomewa


Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) imeshauriwa kuwa na uraia kwa watu wake pamoja na kuvipa hadhi vikosi vyake maalumu ili viweze kumiliki silaha za kivita chini ya mfumo wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.


Ushauri huo ulitolewa jana na baadhi ya wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wakati wakichangia makadirio na matumizi ya Wizara ya Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Vikosi Maalumu iliyowasilishwa na Waziri wake, Haji Omar Kheir, Chukwani mjini Unguja jana.


Akichangia bajeti hiyo, Mwakilishi wa Koani, Mussa Ali Hassan alisema wakati umefika kwa vikosi vya SMZ kupewa hadhi ya kumiliki silaha za kivita badala ya kumiliki silaha za kawaida kama ilivyo sasa kwa mujibu wa sheria.
Hassan alisema kuna vikosi vya SMZ ambavyo havina tofauti na askari wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), ambavyo vilishiriki kupambana na majeshi ya Idd Amini yalipovamia Tanzania mwaka 1978.
Alisema ni wakati mwafaka na unaofaa kwa SMZ kununua silaha kama mizinga, vifaru, helikopta za kivita na boti za kijeshi pamoja na silaha nzito kama RPG.


Wajumbe wengine, Amina Idd Mabrouk (Viti Maalumu), Jaku Hashim Ayoub(Muyuni), Raha Suleiman (Viti Maalumu), waliitaka Serikali kuangalia masilahi ya askari wa vikosi vya SMZ ikiwamo kuwapatia vitendea kazi pamoja na kuwajengea makazi bora.


Wawakilishi hao kwa nyakati tofauti walidai kuwa nyumba nyingi za makazi ya askari ni chakavu na hazistahili kukaliwa na askari ambao wanalinda nchi huku wananchi na viongozi wakiishi kwenye makazi bora.


Pia waliitaka SMZ kutambua umuhimu wa kuwalipa posho na marupurupu stahiki kwa muda wa kazi wa ziada askari wa vikosi vya SMZ pamoja na kuwaingiza katika Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF).


Akizungumzia uraia, Mwakilishi wa Chambani, Mohamed Mbwana Hamad alisema: “Huwezi kuwa na nchi bila ya kuwa na raia.” Alitaka Wazanzibari kupewa uraia wao katika mfumo wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na kusema ni jambo la kushangaza Wazanzibari kuitwa wakazi na si raia.


Alisema Wazanzibari wote wanatakiwa kupewa hadhi ya uraia na wageni ndiyo wanaostahili kuwa na vitambulisho vya ukaazi kama ilivyokuwa miaka ya nyuma, hatua ambayo itaipa hadhi nchi na kutambulika kitaifa na kimataifa.
Watanunua na nini hiyo mixinga wakati tunawalipia mishahara ya wafanyakazi SMZ na kuwalipia umeme!
Tatizo Wazenj hawajijui kuwa wameolewa ndani ya muungano mapembe ya kumtishia nani?
 
Hata Asha Bakari akiwa Zanzibar anadai uhuru wa Zanzibar, ila akiwa Dodoma, ujasiri wote unaisha!
 
Keissy aliwaambi nji nyeupee, jhakuna aliyetoka mjengo! Ungewauliza waikuwa wanasubiri nini, na je walihitaji nguvu za kutoka mjengoni kuelekea bandarini.

Kutoka bungeni na kielekea bandarini bado wazanzibar hawajajitoa kwenye himaya ya Tanganyika, kujitoa ni kuvunja muungano huu wa kidhalim ambapo Kessy na Lukuvi walienda makanisani wakasema haiwezekani Zanzibar kupatiwa mamlaka yao, kwa lugha nyengine Tanganyika hawataki Zanzibar iwe huru. Tanganyika ndio kikwazo hamtaki kutuacha munatungangania.
 
Pasco unasemaje? mwanamke inabidi atunzwe.. huyu mke tumemchoka.. tumempa yote lakini bado anataka apewe na silaha.. mdau mmoja kasema ako ka bil 700 kanampa kibri..
 
Last edited by a moderator:
Kutoka bungeni na kielekea bandarini bado wazanzibar hawajajitoa kwenye himaya ya Tanganyika, kujitoa ni kuvunja muungano huu wa kidhalim ambapo Kessy na Lukuvi walienda makanisani wakasema haiwezekani Zanzibar kupatiwa mamlaka yao, kwa lugha nyengine Tanganyika hawataki Zanzibar iwe huru. Tanganyika ndio kikwazo hamtaki kutuacha munatungangania.

mbona mnafurahia kung'ang'aniwa.. mnapenda sana umeme wa bwelele.. tulia mpate vya bure..ila msilalame hiyo ndio impact ya vya bwelele..
 
Kutoka bungeni na kielekea bandarini bado wazanzibar hawajajitoa kwenye himaya ya Tanganyika, kujitoa ni kuvunja muungano huu wa kidhalim ambapo Kessy na Lukuvi walienda makanisani wakasema haiwezekani Zanzibar kupatiwa mamlaka yao, kwa lugha nyengine Tanganyika hawataki Zanzibar iwe huru. Tanganyika ndio kikwazo hamtaki kutuacha munatungangania.

hehehe wazenjy bwana kwa kuongea tu hamjambo
 
Ng'ombe tumempa mashudu kwa muda mlefu sana, wacha tumkamue maziwa.. japo ng'ombe mwenyewe kakonda kabaki mifupa mitupu lakini lazima maziwa tuyakamue na yatoke tena yakutosha..
 
mbona mnafurahia kung'ang'aniwa.. mnapenda sana umeme wa bwelele.. tulia mpate vya bure..ila msilalame hiyo ndio impact ya vya bwelele..

Zanzibar ndio nchi pekee ulimwenguni inayonunua umeme ghali kutoka Tanga ambapo huduma hiyo ata nchi za Kenya na nyengine za jirani tungeipata kwa unafuu mara 2 zaidi.,
 
Ni hatari sana Zanzibar ni nchi lakini wananchi wake sio raia ni wakaazi tu, Kuna haja Zanzibar kufanya Mapinduzi makubwa sana kujivua kutoka kwa watanganyika kwa nguvu zote ata kama hawatak. Ni aibu miaka 50 toka uhuru wazanzibar siyo raia ndani ya nchi yao

Mkuu zanzibar haijafikisha miaka hamsin ya uhuru bali zanzibar ilikua huru kwa miez mitatu tu. Yaan january to april 1964 kisha ikarud kutawaliwa mpaka leo hii
 
Back
Top Bottom