Zanzibar: Rais Samia kuwa Mgeni rasmi Maazimisho ya Maisha ya Maalim Seif Sharif Hamad. Kwa siku mbili

figganigga

JF-Expert Member
Oct 17, 2010
25,474
54,801
cover_150613323_893092191444948_8062762209227983204_n.jpg

Rais Samia atakuwa Mgeni rasmi katika maazisho ya Hayati Maalim Seif Hamad Shalif Mjini Zanzibar.

Maazimisho yatafanyika Golden Tulip Airport Hotel Zanzibar kuanzi tarehe 05 hadi 06 Novemba 2021 siku ya Ijumaa na Jumamosi.

Je, rais Samia ni rais wa Wote?

Maalim Seif alifariki dunia saa tano asubuhi 17.02.2021 akiwa katika Taasisi ya Magonjwa ya Moyo ya Jakaya Kikwete iliyopo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) alikokuwa amelazwa kwa takribani wiki mbili.

Maalim Seif alifariki dunia akiwa ametumikia wadhifa wa makamu wa kwanza wa rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa chini ya siku 100 - akiwa sehemu ya Serikali ya Umoja wa Kitaifa iliyoundwa baada ya Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar wa mwaka 2020.

Kabla ya kifo chake, katika hatua isiyo ya kawaida, chama chake cha ACT Wazalendo kilitoa taarifa kwa vyombo vya habari iliyoeleza kwamba Maalim na baadhi ya wasaidizi wake na watu ndani ya familia yake walipata maambukizi ya ugonjwa wa korona.

Maalim Seif Sharif Hamad, mbali na kuwa Makamu wa kwanza wa Rais visiwani Zanzibar pia alikuwa mwenyekiti wa chama cha kisiasa cha ACT Wazalendo na gwiji katika maswala ya kutetea demokrasia nchini Tanzania.

Zaidi, soma; TANZIA - Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad afariki dunia
 
Kweli siasa siyo uadui lakini kwanini Mwendazake alitaka kumuuwa kijana wa watu. Yani risasi 16

Nae mama kampa kesi ya ugaidi Mbowe wa watu ambae hata mataifa ya nje wameshindwa kujua ugaidi wa Mbowe
SSH atajichoresha tu.Labda kama "anataka" dunia ione Tanzania ni "mfano fake" wa "kuigilizwa"!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom