Zanzibar kesho itapata uhuru wake

Zanzibar kesho itapata uhuru wake

Wewe mtoa MADA kama huna cha kusema bora utulie kaka,, hapa si sehemu ya kuporoja lete maneno yenye mashiko, ivi ni nani asiyejuwa kwamba Zanzibar ilipata uhuru wake tokea 64? Nani asiyejuwa kama Zanzibar iliungana na Tanganyika zote nchi 2 zikiwa huru? Nani asiyejuwa kama Nyerere alifanya hila akaiondoa na kuisambaratisha nchi ya Tanganyika kinyemela na kujificha kwenye Jamuhuri ya Muungano? Kwanini muna kichwa ngumu nyinyi Vichogo? kuweni wazalendo mudai nchi yenu ya Tanganyika kama vile wazanzibari wanavyopigania kupata nchi yao huru yenye mamlaka ambayo sasa yamemezwa na hilo gengi la Makada wa CCM, Kwa nini nyinyi samaki hamugeuki tu mukawa binadamu wa kawaida na akili timamu? daini nchi yenu Tanganyika mkataa kwao ni Mtumwa,
 
Kikwete aliapa kuilinda na kuitetea katiba ya JAMHURI YA MUUNGANO YA TANZANIA. Hamtaweza...
 
Hivi muda bado tu? Tuachane na hawa waunguja na wapemba???? Na 4.5% ya mapato muisahau
 
Kikwete aliapa kuilinda na kuitetea katiba ya JAMHURI YA MUUNGANO YA TANZANIA. Hamtaweza...

Serekali haina dini kiapo hakina mashiko,ufisadi aliuapia?
 
Written byAhmed Omar Khamis // 31/05/2013

Source: Mzalendo

Je unayo habari? Je umesahau? ni wazanzibari, wapenda nchi yao, wazalendo, wanaharakati, wana kindakindaki na wale wanaosema kwa yakini ya mioyo yao na kuthibitisha kwa vitendo vyao mapenzi makubwa ya nchi yao. Wale wanaoamini kwamba "vyovyote na iwe lakini Zanzibari ibaki huru yenye mamlaka yake kamili".

Umma huo utakusanyika kesho Jumamosi tarehe 01/06/2013 katika viwanja vya Demokrasia Kibanda Maiti. Uwanja wa Kibanda Maiti utageuka "Tahrir Square" ya Misri na kuudhihirishia ulimwengu kwamba wazanzibari kwa amani kabisa wanataka mamlaka kamili ya nchi yao tukufu.

Unamuogopa nani ewe mzanzibari? Ogopa nchi yako kuendelea kuwa chini ya ukoloni. Hapa ni Zanzibar kwanza, itikadi ni baadae. Viongozi mbali mbali wa vyama mbali mbali wazalendo wenye uchungu na nchi yao wanatarajiwa kuhudhuria.

Shime wazanzibari tujitokeze kwa wingi. Mambo yataanza saa 2:00 za asubuhi mpaka saa 12:00 jioni. Mgeni Rasmi ni Makamo wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad.

TUNATAKA NCHI YETU SASA TUMECHOKA TAFRANI

ZANZIBAR KWANZA!

My Take

Ni dhahiri kuwa Leo Zanzabar inafanya maamuzi wanayoamini ni makini kwa mustakabali wa nchi yao kwa kuitaka Zanzibar Huru yenye mamlaka kamili -Siku hii wameibatiza jina la "MAMLAKA DAY" 01/06/2013.

Sisi watu wa bara hatupaswi kuwabeza hata kidogo kwa wazanzibar kufikia maamuzi haya. Tulishaongea mara kadhaa kuwa kero za muungano zitatuliwe, viongozi wetu dhaifu wakapiga danadana jambo hili na kuendelea kuipeleka zanzibar nginjangija hadi sasa wazanzibar wamechoka na mwendo huu. I support them for what they are going to do this morning.

Hata kama Watanzania bara tunaona Zanzibar haina sababu za msingi kufanya maamuzi haya, mimi nadhan ni haki yao kabisa, Zanzibar lilikuwa taifa huru na Taifa kamili, hivyo linasauti kamili na halali katika kujiamulia mambo yake. Viongozi wetu wameshindwa kuweka fair playing ground hivyo tukubali tu maamuzi yao. Muungano sio lazma, waliingia kwa hiari yao na wanatoka kwa hiari yao.

Nadhan hii itakuwa ni ushahidi wa utendaji mbovu wa serikali ya ccm iliyopo madarakani kwa kushindwa kutatua kero za msingi za wananchi wake. Zanzibar ni nchi yao, Zanzibar ina watu wake ni vyema tukaheshimu maamuzi ya wanazanzibar.
 
Wewe mtoa MADA kama huna cha kusema bora utulie kaka,, hapa si sehemu ya kuporoja lete maneno yenye mashiko, ivi ni nani asiyejuwa kwamba Zanzibar ilipata uhuru wake tokea 64? Nani asiyejuwa kama Zanzibar iliungana na Tanganyika zote nchi 2 zikiwa huru? Nani asiyejuwa kama Nyerere alifanya hila akaiondoa na kuisambaratisha nchi ya Tanganyika kinyemela na kujificha kwenye Jamuhuri ya Muungano? Kwanini muna kichwa ngumu nyinyi Vichogo? kuweni wazalendo mudai nchi yenu ya Tanganyika kama vile wazanzibari wanavyopigania kupata nchi yao huru yenye mamlaka ambayo sasa yamemezwa na hilo gengi la Makada wa CCM, Kwa nini nyinyi samaki hamugeuki tu mukawa binadamu wa kawaida na akili timamu? daini nchi yenu Tanganyika mkataa kwao ni Mtumwa,
Kiongozi unaeleweka tu bila kututukana, si wabara wote tunaoona ni haki kuipeleka Zanzibar nginjanginja. Pia sio wabar wote tunaoona ni sahihi kwa serikali kufumbia macho utatuzi wa kero za muungano.

Hivyo unavyovurumisha maneno yasiyo na staha kwa wabara wote, unatuvunja sana moyo watu tunaoamini kuwa mpo sahihi kudai MAMLAKA kamili.
 
Unafiki gani? Hebu specify, kama huna unachokijua you dont have to post.

chilubi, unafiki wenu ni kuwa, tatizo ni CCM lakini mmevaa miwani ya mbao. Wapuuzi kweli ninyi
 
Last edited by a moderator:
Kumbe mnaitegemea zenj kuitoa ccm madarakani?

kuna mibunge ya CCM kama 50 hivi toka Zenj kama Mabumba haina faida wala mchango. 2015 bila wabunge wa Zenj the devils(ccm) will go down to the grave
 
Dahh!afadhali leo kuwa umekiri kumbe z'br sio nchi huru,kuna wenzako watanganyika hawataki kuiona z'br inatoka kwenye makucha ya mkoloni mweusi.

wanaokataa ni CCM tu! Ndo maana akina Kinana wameanza kumuwinda Lissu
 
Mnatulisha, yaani hizi point zenu mnachekesha nyie. Wapemba mnaotaka kuwafukuza wamekupeni Ajira Kkoo, wamekujengeeni mji, wamekufundisheni ustaarabu na usafi. Wapemba wanahela mjini wewe mwenyeo unawalilia wale. Msisahau kumuondoa na Bakhresa,mtazidi kujambajamba. Zanzibar tulikuwa tunaimport vitu from india na bei ilikuwa cheeeee kuliko tunavonunua bara, kisha mnasema mbatulisha. Mnauwezo wa kutulisha? Matumbo yenu yanawashinda apo mlipo. Mnatulisha nini hasa? Mnatupa bure? Gari ikitoka Zanzibar kuja dar ilipiwe ushuru dar kuja zanzibar hamudaiwi ushuru kisha eti mnatusaidia ah, mnavituko sana . Wakati wapemba ndio wanakusaidieni na hasa apo kkoo, angalau mnapata hela ya kula kwa siku vyenginevyo mngejaa barabarani mkiomba omba!

yaheee mbona unaongea pumbaaa! Acha uduanz chalii yangu wapemba wanawalisha kina nani?
 
Jamani kesho si ndio leo uhuru saa ngapi au tayari wameshapata.
 
chilubi, tupe updates baasi!! Sherehe za uhuru tayari? Waliberali wameshafika?
 
Last edited by a moderator:
Acha wagombane wao kwa wao wazanzibari sisi tunamsubiri Obama aje atupe maisha bora huku bara kama Magamba walivyo tuaminisha tunamsubiria baba Obama.
 
Wazanzibari wanashangaza sana, wanasema zanzibar ni nchi hapo hapo wanadai uhuru, sasa hiyo ni nchi gani isiyokuwa huru.
Kwanza hakuna haja ya muungano wa mkataba, muungano usiwepo kabisa kila nchi iwe kivyake.
Wazanzibar wanafikiri kujitenga ndiyo suruhisho la matatizo yao, ila ndiyo mwanzo wa matatizo zaidi ndani ya Zenji, wao kwa wao.
Na kama gas na mafuta vimepatikana Pemba Waunguja wana hali ngumu, kwa ujumla wapemba ni wabinafsi sana.
 
Back
Top Bottom