Zanzibar iungwe na Bara kwa Daraja - Wazo Jipya

kwani daraja linaondoa ulazima wa bandari?

Haiondoi ulazima lakini inaweza kupunguza hitaji na kazi zake.

Katika tathmini ya traffic ya mizigo itakoyopita kwenye daraja, uwepo wa bandari yenye kufanya kazi hiyo tayari, ni factor kubwa ya kuzingatiwa.

Uwepo wa daraja utaathiri vipi bandari na uwepo wa bandari utaathiri vipi daraja ni details ambazo haziwezi kupuuzwa kuzingatiwa
 
Wakati mwingine inabidi kujiuliza kama tunajiamini tunaweza au tunasubiri wengine waamue tunaweza.. NSSF na wadau wengine kama mko serious kwa hili you have my support....
Tumeanza na daraja la Kigamboni kuunganisha pande mbili za jiji la Dar es Salaam. Soon tutahamia ujenzi wa daraja la Bara na Visiwani
 
Kabla hatujafikiria kuwaunganisha wabara na wazanzibari, tuwafikirie kwanza Wakerewe na Wamafya
 
Kwanini wasijenge tube iwe inapita train kama ile ya uk to france,maana daraja kwa umbali huo bahari ikichafuka mawimbi si yataleta balaa kwa watumiaji?
 
Je, Rais Magufulu kutokana na maono yake ya "Tanzania Inayoweza" anaelekea kufikiria kitu kikubwa kama hiki? Kuna watu wanaweza kuunga mkono wazo kama hili? Ni nini kitakuwa kizuizi kikubwa cha kifikra kufikiria, kupanga na kutekeleza mradi mkubwa kama huu?
 
Project hii kwa nchi kama Tanzania haiwezekani na wala haina tija. Tuendeleekutumia usafiri wa tija kama ferry, meli, boti na ndege toka Tanganyika kwenda Unguja na kurudi.

Tutazame daraja refu liliotumia miaka tisa kumalizika (2008 -2018 )

Mega project! Taking a ride on world's longest sea bridge, which, linking Hong Kong, Zhuhai and Macao, is yet to be formally opened to traffic.



Source : NewChina TV
 
Bagamoyo, usiangalie kwa miaka kumi ijayo; ni lazima uangalie miaka 100 ijayo. Na kila daraja linaweza kuangaliwa tija yake - kuanzia ujenzi n.k Lakini, pia ni muhimu kujaribu kujibu swali la kwanini tuunganishe; kutakuwa na faida gani kuunganisha kwa daraja...
 
Bila ya shaka utakuwa umesikia leo taarifa ya lile daraja refu zaidi kupita bahari limefunguliwa huko China leo. Daraja hilo liitwalo Daraja la Qingdao Jiazhou lina urefu wa kilometa 42 (sawa na umbali wa mbio za marathoni) kama mile 26 hivi. Daraja hilil la China la kisasa kama picha zinavyoonesha limejengwa kwa gharama ya dola bilioni 1.5 (karibu na shilingi za Kitanzania Trilioni 2 na ushee). Daraja hili lilianza kujengwa mwaka 2006 na limekamilika mwaka 2011 kama ilivyotarajiwa.

e51fd62d93389c0ef10e6a706700fb3f.jpg


2011-06-30T113121Z_01_PEK07_RTRIDSP_3_CHINA.jpg









(Picha zote na AP na Reuters)

Tunajifunza Nini?

a. Bahari si kikazo cha kuunganisha sehehu mbili za nchi moja.
b. Gharama ya kujenga daraja kama hili kuunganisha Tanzania moja ziko ndani ya uwezo wetu na ninaweza kuargue kuwa tunaweza kufanya kwa fedha zetu wenyewe japo utaalamu na wataalamu tunaweza kuwashirikisha rafiki zetu wa China - tukiwapa BAES!
c. Gharama ya dola bilioni 1.5 ni sawa na fedha zilipotea katika ufisadi kwa mwaka mmoja uliopita tu. Tukichanganya fedha zilizopotea kwa miaka kumi iliyopita tungeweza kabisa kuunganisha Zanzibar mara tatu - kutokea Tanga kwenda Pemba, kutoka Dar (au Bagamoyo-the closest points to the mainland from Unguja?) na Pemba na Unguja! - by the Way kwa miaka kumi iliyopita ufisadi umegharimu zaidi ya bilioni 10 (dola!!)
d. Kwenye kile kinachoitwa Mpango wa Maendeleo ambao uko tayari kutumia shilingi trilioni 42 hakuna mpango wa kuthubutu kama huu.
e. Tunapoelekea miaka 50 ya Uhuru hakuna kitu kitakachoonesha Muungano wetu kuwa umehimiri vishindo na matatizo kama kuzinduliwa kwa daraja la Muungano (Union Bridge) japo sehemu yake mwaka 2014 huku likikamilika 2015.
f. Naamini ujenzi wa daraja/madaraja ya kuunganisha Zanzibar na Bara utasaidia sana katika kuleta maendeleo visiwani na kuusogeza ule udugu wa damu kati yetu karibu zaidi kwani kwa mara ya kwanza bahari itaondolewa kama alama ya kutengana kwetu, watu wa Zanzibar na bara wataweza kwenda nchini mwao wakati wowote na mahali popote bila kutishiwa sana na masuala ya usalama kama ilivyo sasa.
g. Bara nako kutanufaika sana na kufunguliwa kwa njia hii mpya.


Maswali ya Kutafakari:
Je kuna uongozi wowote ndani ya CCM wenye mawazo ya namna hii au mwitikio wa kwanza 'hatuwezi?
Je, Rais Kikwete anaweza kuja na mpango kama huu madhubuti wakati daraja la kuunganisha Kigamboni na Kivukoni tu pale limeshindikana hadi hivi sasa licha ya kuwa katika mipango kwa muda mrefu?
Je, yawezekana wazo hili haliwezi kuletwa, kutetewa wala kusimamiwa na viongozi wetu wa sasa - kwani hawana uwezo wa kulisimamia kama Nyerere alivyosimamia kujengwa kwa reli ya Uhuru (of course lazima nirushe dongo kidogo tu!)?
Je, yawezekana Chama cha Mapinduzi kimepoteza kabisa uwezo wake wa kuthubutu mambo makubwa na sasa kimeamua kufanya mambo madogo kama "mabarabara ya juu kwa juu"?
Je, tusubiri uongozi mpya ambao utakuwa tayari kuliunganisha taifa letu.

Jambo pekee ambalo tuna uhakika nalo kwa kuangalia China ni kuwa inawezekana kuunganisha kwa daraja umbali wa kilomita 42 (au hata zaidi) kwani Zanzibar iko kati ya Maili 16-31 sawa na kilomita 25-50 hivi (kutegemeana na eneo unalosimama kutoka bara). Hii ina maana tukiangalia mahali ambapo ni shortest distance. Hivyo swali la kama inawezekana kiteknolojia au vinginevyo limeshabiwa. Kwa upande wetu ni swali la kisiasa zaidi - je tuna viongozi ambao wanaweza kubuni, kusukuma na kusimamia mpango huu?


UPDATE - OKTOBA 23, 2018

Wachina wamezindua daraja jingine leo hii ambalo lina umbali wa maili 34 (zaidi ya kilomita 60). Je, wamewezaje? Daraja hili jipya linaenda kuviunga visiwa vya Hong Kong na Macau na China Bara... Unguja na Pemba ziungwe na Bara kwa namna hii?

View attachment 908357
Siku ukigombea nitakupa kula zangu na familia yangu na ndugu zangu ....nimekua nikifikilia hiki kitu ...nikaamua kusesearch uzi wa kuhusu idea ya kujenga daraja n nikauona ....big up mkuu
Kunywa Pepsi big ntalipa
 
Back
Top Bottom