Leonard Robert
JF-Expert Member
- Apr 22, 2011
- 11,064
- 7,196
wazo zuri ila jamaa watapuuza kwan limetolewa jf.
Tujenge kwanza daraja la kuunganisha Unguja na Pemba!
Hivi mnafikiria huko China hakuna ufisadi? Au China viongozi wote ni wazuri na wazalendo?
Bila ya shaka utakuwa umesikia leo taarifa ya lile daraja refu zaidi kupita bahari limefunguliwa huko China leo. Daraja hilo liitwalo Daraja la Qingdao Jiazhou lina urefu wa kilometa 42 (sawa na umbali wa mbio za marathoni) kama mile 26 hivi. Daraja hilil la China la kisasa kama picha zinavyoonesha limejengwa kwa gharama ya dola bilioni 1.5 (karibu na shilingi za Kitanzania Trilioni 2 na ushee). Daraja hili lilianza kujengwa mwaka 2006 na limekamilika mwaka 2011 kama ilivyotarajiwa.
(Picha zote na AP na Reuters)
Tunajifunza Nini?
a. Bahari si kikazo cha kuunganisha sehehu mbili za nchi moja.
b. Gharama ya kujenga daraja kama hili kuunganisha Tanzania moja ziko ndani ya uwezo wetu na ninaweza kuargue kuwa tunaweza kufanya kwa fedha zetu wenyewe japo utaalamu na wataalamu tunaweza kuwashirikisha rafiki zetu wa China - tukiwapa BAES!
c. Gharama ya dola bilioni 1.5 ni sawa na fedha zilipotea katika ufisadi kwa mwaka mmoja uliopita tu. Tukichanganya fedha zilizopotea kwa miaka kumi iliyopita tungeweza kabisa kuunganisha Zanzibar mara tatu - kutokea Tanga kwenda Pemba, kutoka Dar (au Bagamoyo-the closest points to the mainland from Unguja?) na Pemba na Unguja! - by the Way kwa miaka kumi iliyopita ufisadi umegharimu zaidi ya bilioni 10 (dola!!)
d. Kwenye kile kinachoitwa Mpango wa Maendeleo ambao uko tayari kutumia shilingi trilioni 42 hakuna mpango wa kuthubutu kama huu.
e. Tunapoelekea miaka 50 ya Uhuru hakuna kitu kitakachoonesha Muungano wetu kuwa umehimiri vishindo na matatizo kama kuzinduliwa kwa daraja la Muungano (Union Bridge) japo sehemu yake mwaka 2014 huku likikamilika 2015.
f. Naamini ujenzi wa daraja/madaraja ya kuunganisha Zanzibar na Bara utasaidia sana katika kuleta maendeleo visiwani na kuusogeza ule udugu wa damu kati yetu karibu zaidi kwani kwa mara ya kwanza bahari itaondolewa kama alama ya kutengana kwetu, watu wa Zanzibar na bara wataweza kwenda nchini mwao wakati wowote na mahali popote bila kutishiwa sana na masuala ya usalama kama ilivyo sasa.
g. Bara nako kutanufaika sana na kufunguliwa kwa njia hii mpya.
Maswali ya Kutafakari:
Je kuna uongozi wowote ndani ya CCM wenye mawazo ya namna hii au mwitikio wa kwanza 'hatuwezi?
Je, Rais Kikwete anaweza kuja na mpango kama huu madhubuti wakati daraja la kuunganisha Kigamboni na Kivukoni tu pale limeshindikana hadi hivi sasa licha ya kuwa katika mipango kwa muda mrefu?
Je, yawezekana wazo hili haliwezi kuletwa, kutetewa wala kusimamiwa na viongozi wetu wa sasa - kwani hawana uwezo wa kulisimamia kama Nyerere alivyosimamia kujengwa kwa reli ya Uhuru (of course lazima nirushe dongo kidogo tu!)?
Je, yawezekana Chama cha Mapinduzi kimepoteza kabisa uwezo wake wa kuthubutu mambo makubwa na sasa kimeamua kufanya mambo madogo kama "mabarabara ya juu kwa juu"?
Je, tusubiri uongozi mpya ambao utakuwa tayari kuliunganisha taifa letu.
Jambo pekee ambalo tuna uhakika nalo kwa kuangalia China ni kuwa inawezekana kuunganisha kwa daraja umbali wa kilomita 42 (au hata zaidi) kwani Zanzibar iko kati ya Maili 16-31 sawa na kilomita 25-50 hivi (kutegemeana na eneo unalosimama kutoka bara). Hii ina maana tukiangalia mahali ambapo ni shortest distance. Hivyo swali la kama inawezekana kiteknolojia au vinginevyo limeshabiwa. Kwa upande wetu ni swali la kisiasa zaidi - je tuna viongozi ambao wanaweza kubuni, kusukuma na kusimamia mpango huu?
Ndugu yangu hizi ni kelele za mfa maji, taarifa za kiintelijensia zinaonesha kuwa kuna mkakati wa nguvu (tena una ufadhili wa nchi moja ya Kiskandinavia) wa kuvunja muungano kwa ajili ya mafuta na inasemekana tukigawana maji ya bahari ndugu zetu watapata eneo kubwa la kina kirefu!
Stimulus package ya Tanzania ilikuwa around Tsh 1.7 trillions. Ukijumlisha na hivi vijicent vinavyopotea EPA, Kagoda, Meremeta, Rada, Vasco da Gamma travels, vitafunwa na ndugu na jamaa wote wanaohusika, Tanzania inaweza kabisa kugharamia Daraja kama hili. In fact umbali wa DAR-Zanzibar ni 40km. (2km less than huu umbali wa daraja china). But being a nation cursed with non-visionary leadership tutaendelea kusoma China leo, Cambodia kesho, Malayasia keshokutwa. Maybe we should try the other household- CDM that is!
muungano ukivunjika? daraja nalo lipigwe mizinga?
akili za magambaDaraja kati ya Tanzania na Msumbiji ni kwa sababu hizi mbili ziko kwenye Muungano?
naona ndio uzuri wa kujijengea reputation ya u GT angeweka hu uzi hapa mwingine angeonekana anaongea pumba na mashambulizi kibao.
Tusifikiri kidogo, tusijifunge kwenye kufikiri vidogo; CCM imetufanya tufikiri kidogo, viongozi wetu hawafikiri tena makubwa! wanataka ya wastani! Well mataifa ya kisasa hayajengwi na watu wenye kufikiri kidogo au kwa wastani! Muungano ukivunjika mnaweka vituo vya mpaka na forodha katikati ya bahari kwenye hizo barabara! au hili linahitaji ugenius kulifikiria nalo? Au Muungano ukivunjika maana yake Zanzibar inazama baharini!?
Umeweza kufahamu hilo kwa muda mfupi uliopo hapa au ulikuja upya baada ya hiyo mitikisiko unayosema? Ndugu yangu kunataka moyo kubaki humu unless ............!