Zanzibar haina uwezo kuchangia sawa na Bara’

Zanzibar haina uwezo kuchangia sawa na Bara’

Mkuu ndo maana nikasema nyinyi hamuwezi kufanya maamuzi magumu bado munataka kutunyonya kama nchi ndogo na pato lake dogo haiwezi kuchangia katika serekali ya muungano kwanini bado munanganga nayo si iwacheni halafu how many times wazanzibar washaonyesha hisia za wazi kwamba muungano hatuutaki mfano ni jumbe huyo huyo ulomtaja ndo aloingia matatizoni kwasababu ya kuhoji muunga wangapi wengine wameingia matatizoni kwa kuhoji muungano HADI SASA MUUNGANO KUUHOJI NI DHAMBI NA SHERIA HAIRUHUSU KUZUNGUMZIA KUUVUNJA na ndo maana unakuta tunatumia ujanja kama kuuvunja ni kesi basi leteni muungano wa wa mkataba unakuta wengine wanajitoa fahamu hawajui eti nini muungano wa mkataba halafu sisi wazenji tumeuzunguza wazi kabisa kama muungano hatuutaki na baraza la wakilishi wameongea kwamba hauna faida na sisi.


HATA KAMA KUNA BAADHI YA WAZANZIBAR WANATAKA MUUNGANO LAKINI MUUNGANO GANI si huu wa kudharauliana kwamba kijinchi kadogo sijui uchimvi gani sasa kama mulijua nchi ndogo ilikuaje mukaungana nao nyinyi mababu hapo ndo utaona kwamba mulikua hamna dhamira njema na hilo tuliliona mapema tulipomaliza kuungana tuu mwaka mmoja tuu mukaanza kubadilisha na kuongeza vitu kwenye mkataba wa muungano na mwisho wake mzee karume alivyoshtuka mukaona ahh ataharibu kila kitu ndo MR X akamaliza kila kitu.


SWALI lini nyinyi watanganyika (jina hamlitaki munataka tanzania bara) mulokaa bungeni mukaongea kwamba muungano hauna faida kwenu tuachane nao hamuwezi na wala hamutaweza sisi ndo tutakaouvunja muungano kwasababu kuna jambazi moja linajifanya kubwa na janja.


TUACHIWE TUPUMUE MIAKA 50 INATOSHA YA UNYONYAJI
Hapana ndugu yangu hakuna anaye wng'ang'ania.

Tume ya Warioba mumetaka usawa wa wajumbe.
Badala ya kudai kura ya maoni ninyi mkaamua kuwachagua akina Ally Saleh wa BBC. Sasa hivi kimyaa

Ninyi mnadai muungano wa mkataba. Sasa kama hamtaki muungano mnataka mkataba wa nini wakati mnatakiwa mkaijenge znz ya kabla ya mwaka 1963.

Bunge la katiba mumedai wajumbe zaidi. Khaa! sasa kama hamtaki muungano mnataka wajumbe waje kufanya nini?
Mlipeleka wajumbe wa tume kwa Warioba wakafanye nini. Mnataka mkataba wa nini.

Ndugu yangu, hebu onyesha wapi Tanganyika ina mnyonya mzanzibar!

Sheni kauliza hivi katika 4.5 mnazopata za pato la taifa ninyi mnachangia kiasia gani?
Mwenyekiti wa kamati ya fedha anasema mapato yenu ni bilioni 240 kwa mwaka. Kwa bajeti ya ulinzi na uslama ambayo ni zaidi ya bilioni 1,300 ina maana kuwa znz bila kuondoa hata senti tano katika 240 haiwezi kuenedha wizara hizo kwa miezi 3.
Hapo nina maana bila kuondoa hata senti tano ya mshahara wa Sheha au ndege za kubeba mikaa kutoka Pemba.

Bajeti ya znz ya mwaka 2013 mapato ya ZBR ni bilioni 100. Hebu onyesha wapi unanyonywa tena naomba uzungumzie TRA

Hebu tueleze wapi mnanyonywa hasa.
 
Nguruvi3,

Duh! Yaani kweli jamaa yetu safari hii umedhamiria kutuhamisha hapo Tanganyika kwa haraka mno! Kwi! Kwi!

Yaani ndugu yangu JokaKuu maskini,kakwita hata two-seconds hazijafika, umeshakuja jamvini na kutoa hukumu yako kali kabisa!

Lakini kumbuka yakuwa hata Nyerere kipenzi chako,akifufuka leo,basi mtu wa kwanza kumkaba koo itakua ni wewe...maana wewe ndo mmojawapo ya Vinara vya kuendeleza tashtit na taarifa za urongo ili kukandamiza na kudhihaki huo "Muungano"!

Ahsanta.

Cc;Mag3

Al akhy gombesugu asaalam aleykum.
Nguruvi3 akiona mada inawahusu wazanzibar anahisi kuchanganyikiwa na chuki yake ni kwanini Zanzibar wanapata fungu kutoka Tanganyika kama ipo au ni jina tu.

Lakini simshangai huku A town tunasema ana roho ya kwanini,kama sijakosea kuna siku ulikuwa unalalamika eti kwani Zanzibar inapata fungu kutoka bara wakati kunawatu pale mtwara wanaishi maisha magumu! hili lilinishangaza sana.

Nguruvi unataka kuniambia kama hilo fungu wasingepewa Zanzibar,Mtwara na mikoa mingine wangekuwa wanaishi maisha mazuri?

Nguruvi hivi hilo fungu ni pesa za walipa kodi tu au pia kuna msaada kutoka kwa wanaoitwa wahisani?

Ahsanta.
 
Technically Tanganyika ndiyo Tanzania.

Anayelalamika kuhusu Tanzania ni znz. Kama Tanganyika ingekuwa na serikali basi ingekuwa rahisi kufanya ufanyavyo.Lakini Rais wa muungano ndiye ni rais wa znz pia kiufundi.

Pili, Tanganyika muda mrefu wamekaa kimya hadi siku za karibuni waliobaini kuwa uongo wa kunyonywa haupo.
Kashafa na maudhi ndivyo vinasukuma suala hili.

Fikiria, Tanganyika na Watanganyika wamebaguliwa sana visiwani katika kila jambo.
Hakuna siku wamesema wanalipa kisasi vinginevyo waznz wapaato laki 4 wangeonja adha na maudhi ya ubaguzi

Kwa mantiki hiyo anayelalamika kuhusu kunyonywa ni mznz na sisi tunawasaidia kuwaambia znz inawezekana kabisa nje ya muungano, wasichotaka kukifanya ni kuondoka katika muungano unao wanyonya, wanabweka tu

Pamoja na hayo tunaweka mezani kuwa kama wanadhani wananyonywa na sisi tunajua wananyonya na pengine kwa uzumbu kuku wetu hatujui hivyo, sasa ni wakati waamue kusuka au kunyoa. Kwa bahati mbaya hawajui wafanyae nini.

Kinachosikitisha ni pale wanapotaka muungano, tukiwambia tukae meza moja tuzungumzie kitu cha kwanza katika karatasi zao ni vyeo na ajira. Tukiwaambia vipi gharama wanakimbia na kusema hawawezi.
Sasa unadai vipi kitu usichogharamia?

Nafasi imetolewa kuhusu kuandika katiba. Wao walichokiona ni wingi wa wajumbe na si kura ya maoni.
Tanzania haiwezi kudai kura ya maoni yake yenyewe kwasababu humo ndani lipo jina(lipo jina tu) la znz. Kufanya hivyo ni kuwaonea.

Kura ya maoni ya Tanzania inaweza kukataa au kukubali muungano lakini je ni haki kwao kwa kuzingatia idadi yao?

Popote duniani mwenye malalamiko ndiye anapewa nafasi ya kufanya hivyo

Ireland wamepewe fursa ya kuamua hatima yao ndani ya British empire
Sudan kusini wamepewa fursa hiyo wakajitenga
Eritrea wamepewa fursa hivyo wakafanya kweli
Timor mashariki wamepewa fursa hiyo
Hata Tibet wanadai fursa hiyo na si China
Puerto Ricco wamepewa fursa hiyo wakaamua
Quebec wamepewa fursa hiyo wakaamua

Zanzibar wamepewa fursa hiyo, wanchomoa chomoa kwa maneno.
Wakiwa Pemba midomo mipana sana wakivuka bahari kimya.

Huwezi kusema muungano mbaya wakati una wajumbe katika tume ya Warioba.
Huwezi kusema hutaki muungano wakati unadai wajumbe zaidi wa bunge la katiba.
Kinachoonekana ni kubabaika bila kujua wanataka nini.

Pengine nikuambie kuwa Tanganyika walitaka kura ya maoni, kwabahati mbaya wao ndiyo Tanzania hivyo nguvu yao ina limitations na vikwazo. Znz wangeweza kutokana na mifano hapo juu ya nchi nyingine.
Wamechomoa, hawataki! kelele tu

Kama rasimu ya katiba ingefuata utaratibu suala hili lingeisha vizuri sana.
Leo tungekuwa tunaongelea matatizo ya Tanganyika bila kelele za kipuuzi.
Kwabahati mbaya hilo halikutokea.

Hata hivyo pamoja na kutokubaliana na utaratibu na tume ya Warioba in general bado kuna elements nzuri sana za kuutua mzigo.

Katika mambo 22 sasa yamebaki 7 na wala si 11 ya awali.
Katika yale yaliyoondolewa mengi yalikuwa zigo la karafuu mgongoni mwa Mtanganyika.

Kama ikitokea serikali 3 basi Mtanganyika atakuwa ametua sehemu ya mzigo.
Kinachotakiwa kwa Mtanganyika ni kuhakikisha kuwa hiyo serikali ya 3 inachangiwa sawa.

Kama wanadai vyeo, kupokezana uongozi kama urais, kudai ajira sawa LAZIMA waje mezani kujadiliana wakiwa na kitu na si porojo hadithi na uongo kama wa Membe kutoka VISA, waziri wa mambo ya nje asiyekuwepo au kunyonywa kwa kuibiwa sh bil 240 ambazo hazitoshi hata kuendesha wizara ya akina mama na watoto.

Ndio maana tunawambia Watanganyika wae macho na mbinu za hawa jamaa za kudai bila kuchangia.
Kwanini Mtanganyika alipe kodi na kodi hiyo iende kumsomesha mtoto wa nchi jirani huku ikimwacha mtoto wa kitanganyika akitaabika. Why!

Kama hawataweza kuchangia hiyo serikali ya muungano, basi wakae kimya tutawaambi wapi washiriki.
Huwezi kutoa 0 na mwenzako 10 halafu mkadai kugawana sawa sawa mapato! hesabu hizo mwisho Chumbe.

Utaratibu wa vyeo na ajaira uambatane na kuchangia gharama. Hilo lazima walitambue na hakuna hoja itakayojengwa kwa usawa, nchi udogo au nini. Kinachotakiwa ni kitu wala si maeneno na pelepele zisizo na mashiko.

Nilivyokuelewa ni kuwa kurudishwa kwa serikali ya Tanganyika itakuwa ni afueni kubwa kwa Mtanganyika.

Ikitokea kuwa suala la kuundwa serikali tatu limekwama (kwa sababu bado hakuna uhakika wa kurejeshwa Tanganyika) unawashauri kitu gani Watanganyika ili wautue "mzigo"?

Kuna plan B?
 
Technically Tanganyika ndiyo Tanzania.

Anayelalamika kuhusu Tanzania ni znz. Kama Tanganyika ingekuwa na serikali basi ingekuwa rahisi kufanya ufanyavyo.Lakini Rais wa muungano ndiye ni rais wa znz pia kiufundi.

Pili, Tanganyika muda mrefu wamekaa kimya hadi siku za karibuni waliobaini kuwa uongo wa kunyonywa haupo.
Kashafa na maudhi ndivyo vinasukuma suala hili.

Fikiria, Tanganyika na Watanganyika wamebaguliwa sana visiwani katika kila jambo.
Hakuna siku wamesema wanalipa kisasi vinginevyo waznz wapaato laki 4 wangeonja adha na maudhi ya ubaguzi

Kwa mantiki hiyo anayelalamika kuhusu kunyonywa ni mznz na sisi tunawasaidia kuwaambia znz inawezekana kabisa nje ya muungano, wasichotaka kukifanya ni kuondoka katika muungano unao wanyonya, wanabweka tu

Pamoja na hayo tunaweka mezani kuwa kama wanadhani wananyonywa na sisi tunajua wananyonya na pengine kwa uzumbu kuku wetu hatujui hivyo, sasa ni wakati waamue kusuka au kunyoa. Kwa bahati mbaya hawajui wafanyae nini.

Kinachosikitisha ni pale wanapotaka muungano, tukiwambia tukae meza moja tuzungumzie kitu cha kwanza katika karatasi zao ni vyeo na ajira. Tukiwaambia vipi gharama wanakimbia na kusema hawawezi.
Sasa unadai vipi kitu usichogharamia?

Nafasi imetolewa kuhusu kuandika katiba. Wao walichokiona ni wingi wa wajumbe na si kura ya maoni.
Tanzania haiwezi kudai kura ya maoni yake yenyewe kwasababu humo ndani lipo jina(lipo jina tu) la znz. Kufanya hivyo ni kuwaonea.

Kura ya maoni ya Tanzania inaweza kukataa au kukubali muungano lakini je ni haki kwao kwa kuzingatia idadi yao?

Popote duniani mwenye malalamiko ndiye anapewa nafasi ya kufanya hivyo

Ireland wamepewe fursa ya kuamua hatima yao ndani ya British empire
Sudan kusini wamepewa fursa hiyo wakajitenga
Eritrea wamepewa fursa hivyo wakafanya kweli
Timor mashariki wamepewa fursa hiyo
Hata Tibet wanadai fursa hiyo na si China
Puerto Ricco wamepewa fursa hiyo wakaamua
Quebec wamepewa fursa hiyo wakaamua

Zanzibar wamepewa fursa hiyo, wanchomoa chomoa kwa maneno.
Wakiwa Pemba midomo mipana sana wakivuka bahari kimya.

Huwezi kusema muungano mbaya wakati una wajumbe katika tume ya Warioba.
Huwezi kusema hutaki muungano wakati unadai wajumbe zaidi wa bunge la katiba.
Kinachoonekana ni kubabaika bila kujua wanataka nini.

Pengine nikuambie kuwa Tanganyika walitaka kura ya maoni, kwabahati mbaya wao ndiyo Tanzania hivyo nguvu yao ina limitations na vikwazo. Znz wangeweza kutokana na mifano hapo juu ya nchi nyingine.
Wamechomoa, hawataki! kelele tu

Kama rasimu ya katiba ingefuata utaratibu suala hili lingeisha vizuri sana.
Leo tungekuwa tunaongelea matatizo ya Tanganyika bila kelele za kipuuzi.
Kwabahati mbaya hilo halikutokea.

Hata hivyo pamoja na kutokubaliana na utaratibu na tume ya Warioba in general bado kuna elements nzuri sana za kuutua mzigo.

Katika mambo 22 sasa yamebaki 7 na wala si 11 ya awali.
Katika yale yaliyoondolewa mengi yalikuwa zigo la karafuu mgongoni mwa Mtanganyika.

Kama ikitokea serikali 3 basi Mtanganyika atakuwa ametua sehemu ya mzigo.
Kinachotakiwa kwa Mtanganyika ni kuhakikisha kuwa hiyo serikali ya 3 inachangiwa sawa.

Kama wanadai vyeo, kupokezana uongozi kama urais, kudai ajira sawa LAZIMA waje mezani kujadiliana wakiwa na kitu na si porojo hadithi na uongo kama wa Membe kutoka VISA, waziri wa mambo ya nje asiyekuwepo au kunyonywa kwa kuibiwa sh bil 240 ambazo hazitoshi hata kuendesha wizara ya akina mama na watoto.

Ndio maana tunawambia Watanganyika wae macho na mbinu za hawa jamaa za kudai bila kuchangia.
Kwanini Mtanganyika alipe kodi na kodi hiyo iende kumsomesha mtoto wa nchi jirani huku ikimwacha mtoto wa kitanganyika akitaabika. Why!

Kama hawataweza kuchangia hiyo serikali ya muungano, basi wakae kimya tutawaambi wapi washiriki.
Huwezi kutoa 0 na mwenzako 10 halafu mkadai kugawana sawa sawa mapato! hesabu hizo mwisho Chumbe.

Utaratibu wa vyeo na ajaira uambatane na kuchangia gharama. Hilo lazima walitambue na hakuna hoja itakayojengwa kwa usawa, nchi udogo au nini. Kinachotakiwa ni kitu wala si maeneno na pelepele zisizo na mashiko.





Mkuu,

umeandika kwa jazba zaidi kuliko hekima unajaribu kukubali TANGANYIKA NDIO TANZANIA kwa misingi ngani nitakuuliza maswala mawili tuu.

1)Kama Tanganyika ndio tanzania kwa misingi ngani na nani alokubali hayo jee znz na tanganyika walikubaliana wapi na kubadilisha hayo japo uwezo huo munao na mumezoea kufanya hivyo,kwasababu neno Tanzania limeundwa kutokana na muunganisho wa nchi mbili kama isemavyo katiba ya asili ya 1977 ibara ya kwanza (i)Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya watu wa Zanzibar zitaungana nakua jamhuri ya muungano(UNITED REPUBLIC OF TANZANIA) kwa mujibu wa vifungu vya mkataba wa muungano.SERIKALI YA TANZANIA NI KIUMBE KILICHOTOKANA NA MKATABA WA MUUNGANO,1964 BAINA YA TANGANYIKA NA ZANZIBAR (jumbe)yaani kila siku barubaru anaaninda ukiwa mroho usiwe mchoyo(barubaru JF) kama sijakosea


2)Kwanini katiba bado inaandika TANZANIA BARA na TANZANIA VISIWANI badala ya Tanzania pekee na (2a) Jee nchi jirani zikitaka kujiunga mutziitaje mfano wa Kenya ama uganda.

WAZANZIBAR WASASA SI WALE WALOLALA TUACHIWE TUPUMUWE MIAKA 50 YATOSHA HATWEBUUUUU MUUNGANO
 
Sasa anataka report ya JFC ili kupata nini zaidi? Pili, yeye hajaweka lakini anadai iwekwe, na nani. Kama anadhani kuna jambo kubwa katika JF Barubaru aliweke hadharani.

Mwenyekiti wa kamati ya fedha ya BLW kasema mapato ya znz ni bilioni 240.
Nimeweka bbajeti ya znz kwa mwaka 2013 katika uzi mwingine.
Inaonyesha mapato ya ZRB na TRA ambayo kwa pamoja na mapato hayajafikia bilioni 500.

Rais sheni kasema wznz wasidharau hiyo 4.5 wanayopata katika muungano. Akauliza znz inachangia kitu gani hadi ilalamike?

Ukisoma bajeti ya znz mambo yafuatyo hayamo
Ulinzi na usalama (ambao wenyewe tu unaweza kuchukua 1/2 ya 240)
Mambo ya ndani (1/4 ya 240)
Elimu ya juu (1/8 ya 240)

Na bado wana access katika mambo yasiyo ya muungano kama afya.

JFC itasaidia nini kwa hesabu za bilioni 240!

Hakuna usawa kati ya Tanganyika na znz hata siku moja. Ni mwendawazimu peke yake anayeweza kudhani kitu kama hicho kipo.

Hawa watu ni kuachana nao, hatuwezi kuishi kwa malalmiko kila siku. Hatuna tunachopoteza.
Tuwaache wajenge Dubai yao ya wakati wa Sultan. Znz yenye uchumi imara inawezekana kabisa lakini lazima wawe tayari kujikomboa kwa kuukata muungano si kudai idadi ya wajumbe bunge la katiba, kamati ya Warioba, vyeo au ajiira.

Let them go !

Nguruvi3,

Mara zote nakueleza ACHA KUNUNG'UNIKA. na ndio maana wakt mwingi nakuwa mzito kufanya mnakasha na wewe. sababu unafikiria uchumi ni kama siasa unapiga bla bla tu.

Na hilo ndio linalokupelekea kudharai Timu za wataalamu wa nchi hizo mbili zinazokaa pamoja kuangalia mapato yenu yooote na matumizi yake na kungalia mgawanyo unaweza kufanyikaje. Ripoti yao ni muhimu sana kwa mtu anayetaka kujua mengi ya kiuchumi wa nchi hizo mbili ikiwemo kujua kila mtu anachangia nini, misaada, mikopo na kila kitu na kufanya mnyumbuliko wake.

Ndugu yangu acha kunung,unika pitia data uone mambo sio maneno ya kijiweni.

Pole sana
 
Hii nyuzi haihusu mambo ya dini. Unachotaka kufanya ni kutuondoa katika mada na ukweli. Tafadhali kama huna hoja kaa kimya.
Tumechoka kusikia habari zako zisizo na mshiko.

Joint financial committee report imewekwa wazi. Hicho ndicho unatakiwa uchangie kwasababu umeomba siku nyingi sana.
Pili, mwenyekiti wa kamati ya fedha ya BLw kasema hamuwezi kuchangia, hilo ndilo unatakiwa uzungumzie
Tatu,

Tafadhali sana usichafue uzi kwa hoja zisizo husika, kama una hoja tofauti anzisha uzi.


Tatizo lako sio kukurupuka na chuki lakin pia kupenda kunung'unika bila kutoa majibu sahihi na hilo linanipa sana kigugumizi kufanya mnakasha na wewe. Kwani kila kitu ni siasa tu hupendi data hata kidogo

Nimeuliza ni uzi gani ambao mumeweka Hiyo ripoti ya JFC. Kwani nina hamu kubwa sana niwape darsa la uchumi kupitia kwa data hizo ili muondokane na hiyo dhana kuwa Znz inawanyonya.

Naomba niwekee hiyo ripoti tuanze kuisasambua page by page.

Lakin vile vile kama ungekuwa unapitia Bajeti zenu za JMTz za kila mwaka utaona hizo 1.2 Bil zinazoelekezwa katika makanisa ambazo ziliidhinishwa na hiyo MoU. na vile vile hiyo misamaa ya kodi ina jedwali maalum utagundua hayo. Kama ni mas'ala ya dini kwanini yanawekwa kwenye bajeti zenu?

usikurupuke jamaa na acha kunung'unika kila wakti badala ya kusoma na kutafuta data.

Pole sana.

 
Hapana ndugu yangu hakuna anaye wng'ang'ania.

Tume ya Warioba mumetaka usawa wa wajumbe.
Badala ya kudai kura ya maoni ninyi mkaamua kuwachagua akina Ally Saleh wa BBC. Sasa hivi kimyaa

Ninyi mnadai muungano wa mkataba. Sasa kama hamtaki muungano mnataka mkataba wa nini wakati mnatakiwa mkaijenge znz ya kabla ya mwaka 1963.

Bunge la katiba mumedai wajumbe zaidi. Khaa! sasa kama hamtaki muungano mnataka wajumbe waje kufanya nini?
Mlipeleka wajumbe wa tume kwa Warioba wakafanye nini. Mnataka mkataba wa nini.

Ndugu yangu, hebu onyesha wapi Tanganyika ina mnyonya mzanzibar!

Sheni kauliza hivi katika 4.5 mnazopata za pato la taifa ninyi mnachangia kiasia gani?
Mwenyekiti wa kamati ya fedha anasema mapato yenu ni bilioni 240 kwa mwaka. Kwa bajeti ya ulinzi na uslama ambayo ni zaidi ya bilioni 1,300 ina maana kuwa znz bila kuondoa hata senti tano katika 240 haiwezi kuenedha wizara hizo kwa miezi 3.
Hapo nina maana bila kuondoa hata senti tano ya mshahara wa Sheha au ndege za kubeba mikaa kutoka Pemba.

Bajeti ya znz ya mwaka 2013 mapato ya ZBR ni bilioni 100. Hebu onyesha wapi unanyonywa tena naomba uzungumzie TRA

Hebu tueleze wapi mnanyonywa hasa.




Mkuu,


Sisi tumetoa maoni yetu kama tunataka mkataba jee nyinyi Watanzania bara(Watanganyika) mumesema nini katika maoni yenu??


Kuonesha onyanyaji wa mtanganyika ni rahisi la kwanza kujiuwa na kujitangaza yy ni Tanzania wakati yy ndo mshirika wa muungano la pili kuongeza mambo kwenye mkataba wa muungano tatu kulazimisha viongozi wetu kujiuzulu kana kwamba wao ndo wametuchagulia unataka zaidi ama...... chama kuingiza katiba yake katika sheria za nchi na pia chama kuwa msemaji wa serikali ya muungano badala ya serikali mbili.


Munatugaia 4.5 sisi hatuchangii sawa jee tunajua Tanganyika inachangia ngapi na inachukua ngapi ilikufa baada ya kuzaliwa tuu??? Raisi shwena kusema tunagaiwa haki yake maana nyinyi ndo mulomuweka pale unafikiri atatetea znz na wananchi wake kumchagua mumchague nyie atutetee sisi mhh.

Bajeti yetu ni 240 b hushangai ww kama mtanganyika kuungana na watu ambao bajeti yao ni ndogo population yao ndogo kuliko hata mkoa wenu mmoja halafu hiyo ni bajeti yetu jee na ile ya misaada ya nje ambayo munatumia jina la Tanzania kuchukulia nyinyi bajeti yenu tangu mupate uhuru munagaiwa kama ombaomba na nyenzo mnazo,mwisho ndo maana mukaambiwa muwe wasagaji tuu muzidi kugaiwa na mwisho wake nafikiri unaujua utakuaje kuomba omba kila siku.


TUACHIWE TUPUMUWE MIAKA 50 INATOSHA YA UTUMWA
 
Al Akhiy,Barubaru,

Wajua,hapo umegusia kitu cha ukweli na undani mwingi mno.

Lakini wenyewe Wabara aka Watanganyika wanakuwa wakali mno ukigusa hayo maslahi ya Kanisa...sasa hivi huu mnakasha watauvuruga na wataanza kutuita sisi ni "Wadini"/"Magaidi"!? Dah! Yaani tafrani tupu!

Ngoja tuwakurubishe hawa waungwana wawili akina Mag3 na Nguruvi3 hapa jamvini,tuone watakuja na sarakasi zipi kwalo!? Kwi! kwi!

Ahsanta.


hawana lolote hao zaidi ya porojo za kisiasa tu na hawana moja katika ilmu ya uchumi na hawataki kudarsishwa.

Hata hiyo Joint Finance Commission ni mimi wakwanza kuwaeleza tena niliwasaidia mpaka kuwaambia afisi zao ziko wapi waende kuangalia hizo ripoti badala ya kuleta vijineno vya kwenye vilabu vya ulevi.

Upande wangu nipo tayari kuwadarsisha kila ninapopata wasaa japo wakti mwingine nakua mzito sababu kuuubwa WAO NI WATU WA KUNUNG'UNIKA KILA WAKTI. na hakuna dhambi mbaya kuliko dhambi ya kunung'unika ,( Allah atuepushe nayo).

lakin mdogo mdogo wataelewa tu. Sijakata tamaa katika kuwadarsisha
 
hawana lolote hao zaidi ya porojo za kisiasa tu na hawana moja katika ilmu ya uchumi na hawataki kudarsishwa.

Hata hiyo Joint Finance Commission ni mimi wakwanza kuwaeleza tena niliwasaidia mpaka kuwaambia afisi zao ziko wapi waende kuangalia hizo ripoti badala ya kuleta vijineno vya kwenye vilabu vya ulevi.

Upande wangu nipo tayari kuwadarsisha kila ninapopata wasaa japo wakti mwingine nakua mzito sababu kuuubwa WAO NI WATU WA KUNUNG'UNIKA KILA WAKTI. na hakuna dhambi mbaya kuliko dhambi ya kunung'unika ,( Allah atuepushe nayo).

lakin mdogo mdogo wataelewa tu. Sijakata tamaa katika kuwadarsisha
Imewekwa hapo, toa darsa mchumi.

Sisi hatuna porojo tunakwenda kwa namba.
Bilioni 240 ndizo zipo mbele yetu, sasa tujiulize ngapi zinaingia katika muungano.

Tukimaliza hapo tujadili haya
Lini znz imekuwa na bajeti ya ulinzi na mambo ya ndani tangu 1964
Ni ipi bajeti ya elimu ya juu tangu mwaka 1964
Ni ipi bajeti ya znz kwa nishati ya umeme tangu mwaka 1974
Nini bajeti ya SMZ kwa wafanyakazi wa muungano
Nini mchango wa SMZ kuendesha taasisi kama SUMATRA kupitia IMO
Nini mchango wa SMZ katika tume ya Warioba
Nini mchango wa SMZ katika wabunge wajao Dodoma kutoka BLW na SMZ
Ni upi mchango wa ZNZ katikam kuendesha serikali ya muungano kupitia ofisi ya makamu wa rais
Bilioni 32 kwenda znz kutoka ofisi ya makamu wa rais ni sehemu gani ya mapato ya taifa.
 
Mkuu,


Sisi tumetoa maoni yetu kama tunataka mkataba jee nyinyi Watanzania bara(Watanganyika) mumesema nini katika maoni yenu??


Kuonesha onyanyaji wa mtanganyika ni rahisi la kwanza kujiuwa na kujitangaza yy ni Tanzania wakati yy ndo mshirika wa muungano la pili kuongeza mambo kwenye mkataba wa muungano tatu kulazimisha viongozi wetu kujiuzulu kana kwamba wao ndo wametuchagulia unataka zaidi ama...... chama kuingiza katiba yake katika sheria za nchi na pia chama kuwa msemaji wa serikali ya muungano badala ya serikali mbili.


Munatugaia 4.5 sisi hatuchangii sawa jee tunajua Tanganyika inachangia ngapi na inachukua ngapi ilikufa baada ya kuzaliwa tuu??? Raisi shwena kusema tunagaiwa haki yake maana nyinyi ndo mulomuweka pale unafikiri atatetea znz na wananchi wake kumchagua mumchague nyie atutetee sisi mhh.

Bajeti yetu ni 240 b hushangai ww kama mtanganyika kuungana na watu ambao bajeti yao ni ndogo population yao ndogo kuliko hata mkoa wenu mmoja halafu hiyo ni bajeti yetu jee na ile ya misaada ya nje ambayo munatumia jina la Tanzania kuchukulia nyinyi bajeti yenu tangu mupate uhuru munagaiwa kama ombaomba na nyenzo mnazo,mwisho ndo maana mukaambiwa muwe wasagaji tuu muzidi kugaiwa na mwisho wake nafikiri unaujua utakuaje kuomba omba kila siku.


TUACHIWE TUPUMUWE MIAKA 50 INATOSHA YA UTUMWA
Haa hivi si mnasema muungano mbaya unawanyonya, sasa mnataka mkataba wa nini tena wakati mnalilia mamlaka kamili.

Pili, katika mambo yaliyoongezwa nitajie matano tu ambayo Tanganyika inanufaika nayo
Je, sasa hivi yamerudishwa hadi 7 kuna unafuu kwa nani hapo.

Tatu, Tanganyika inachangia 96% kwasababu ndiyo iliyobeba muungano. Mwenyekiti wa kamati ya fedha wa SMZ amethibitisha kuwa kwa miaka 48 hamjaweza kuchangia ndio maana anasema mkiweka kugawana sawa znz haitaweza.

Nne, jibu la kumchagua rais wa znz ni rahisi! hakuna rais asiye na jeshi. Rais wa znz hana jeshi na wala wzn hawaelewi hili. Mwenye jeshi ndiye mwenye nchi, na jeshi ni la Tanganyika. Hakuna bajeti ya ulinzi na usalama ya SMZ tangu mwaka 1964. Period.

Misaada inagawiwa znz
1. Angalia bajeti ya znz na mapato halafu ujiulize bilioni 500 za ziada zinatoka wapi iwapo mapato ni bilioni 240.
2. Wanafunzi zaidi ya 1000 wanapata pesa kutoka Tanganyika
3. Ile mishahara inayokuja huko inatoka hazina Dar. Muulize Salmin Amour, Karume
4. Bilioni 32 zisizo na audit kwenda znz hazipo katika mambo ya muungano. Ni msaada wa Tanganyika kama ilivyo 1-3
5. Ule umeme munaowasha bure unalipiwa na Mtanganyika, hamjawahi kupia umeme wengine tangu mzaliwe
6. Wale watu wanaopata ajira kwasababu ya uzanz ni sehemu nzuri ya matumizi ya misaada
7. Wale wabunge wanaokuja Dodoma wabalipiwa gharama na Tanganyika siyo SMZ hata kama hawana kazi pale Dodoma
8. Zile pesa za ulinzi na usalama haziteremki kama mvua ni kodi za watu ambao ni Watanganyika, SMZ inachangia nini?
 
Barubaru hebu sasanbua tunakusubiri mchumi.

JokaKuu usiiondoe maana hiyo ndiyo utatupa ukweli. Hawa kwa hadithi hawawezekani, ukitaka kumpata mzanzibar mtupie namba.


Yaani hizo kashfa,stereotypes na prejudices ndo ulizofundishwa!?

Hivi ni kweli kwa yakini unayaamini hayo uloandika hapo;yakuwa Wazanzibar hawajui asilan hisabati/takwimu!? Duh!!

Pole yako!

Mufti Barubaru naUlamaa Boko Haram...tafadhali wala nyie msichambue lolote/chochote,maana sie "hatujasoma" pia ati ni "wavivu" wa kusoma..."hatujui! kusoma wala kuandika!? Ndo yaleyale!

Al Akhiy,hawa jamaa zetu hamuwawezi kwa malumbano yaso tija,shughulikeni nao tu pale mjisikiapo mna fursa/wasaa wa kuchezea...khasa huyu Nguruvi3!

Ahsantani.
 
gombesugu,

..barubaru hawezi kuleta taarifa za Joint Finance Committee ya Tanzania.

..anafahamu kwamba taarifa hizo zinasema kitu kilekile kilichoelezwa na huyo mwakilishi.

..hivi kwani kuna ajabu gani ktk maneno ya mwakilishi? wa-Tanganyika tuko milioni 40++, wa-Zanzibari hamzidi millioni 3, sasa mtuweza vipi kuchangia sawa na sisi?

..mwisho nawaomba msilete mambo ya dini. masuala ya MOU yana thread yake maalumu, hapa siyo mahala pake.



JokaKuu,

Hishma yako Mkuu!

Wewe ni katika jamaa wachache ambao ninawaheshimu mno humu-JF...yaani nakhis una sifa takriban zoote njema!?

Najua wewe si mdini asilan,japo ni Mkristo mwadilifu/mtiifu.

Yaonyesha pia ni mzalendo mwenye mahaba kwa Taifa lako na Wananchi wenzio wengine bila ya kujali imani/itikadi zao.

Nakusihi,pia ufahamu yakuwa mimi binafsi wala Mufti Barubaru,pia si wadini asilan! Nilishawahi kujieleza kitambo wakti ule ndo mgeni najiunga kwenye hizi tafran za humu-JF...nafikiri bado wakumbuka!?

Pia sisi hatuna haja wala dhamira ya kuleta/kusababisha mihemuko au chuki zozoote ya kidini humu mitandaoni au kwingineko.

Historia yangu binafsi humu-JF,inanihukumu kukemea kwa nguvu zoote na kulipiza "mashambulizi" pale tu inapolazim!


Hapo kwenye bayana yako ati unadai,yakuwa kuzungumzia hayo mabilioni ya MOU kwenda huko Makanisani,haina haja kwasababu ni "mambo ya udini"!?

Mbona kwa mujibu wa mufti Barubaru,yaelekea hizo senti zimo/zimeorodheshwa mpaka kwenye Bajeti ya JMT!?

Pia kwa msomi/mwanataaluma mwadilifu,kuzungumzia/kuhusisha habari zozote za Zanzibar na imani/dini yao sidhani kama ni jambo baya asilan!?

Kumbuka ile ni nchi yenye raia wake ambao takriban 100% ni Waumini wa Kiislam!

Yaani ni sawa uzungumzie kuhusu khabar zozote kuhusu Poland,Austria,Northen Ireland,khalaf ati uka-ignore/discourage kutaja/kuhusisha japo kiduchu ile impact ya Christianity kwenye politics,social economic and/or environment issues of those particular societies!?

Au ufanze hivyo hivyo kwa Maldives au Brunei,khalaf uache kabisa kutaja/kuhusisha impact ya Islam kwenye hizo nchi na watu wake!?

Kwa hiyo hapo kuhusu Zanzibar na imani/dini-Uislam havitengamani asilan...kuanzia kwenye anthropology,philology,Statistics,healthy,Politics na mangineyo mangi mno!

Labda tu,naezasema yakuwa,wewe binafsi ulisema vile kwenye hiyo bayana yako kwa khofu ya wale wenye mihemuko na chuki za kidini wasijevamia na kulivuruga hili jamvi na Topic yetu hii!?

Pia umetusihi ati,kama tunahitajia kuzungumza hizo khabar/Bajeti ya MoU na Makanisa,basi tufatute kuna thread yake humu humu JF!?

Sasa hapo mbona unakua selective ndugu yangu JokaKuu!?...kwani hata haya yoote tuyazungumzayo sasa,mbona pia yameshazungumzwa na kujadiliwa humu humu JF,tena kwa undani mno na pana threads lukuki kwayo!?

Kama ume-notice japo kiduchu...mie binfasi pia nashindwa kuchangia too deep/into insights,sababu sina latest and most viable informations regarding local politics at home,I think I mentioned this before!? Believe me,this is not an excuse at all! Kwi! Kwi!

Ndo maana,waona hata uchangiaji wangu yanilazim niwe na tahadhari kiduchu.

Hata hivyo,kuna machache ninayafahamu kiundani sitasita kuchangia humu.

Niwia radhi kwa lolote ambalo labda itakua hukupendezewa nalo kwenye huo uchechefu wangu.

Ahsanta.
 
Muungano ni serikali 1 hizo pesa mnazodai ilipewa jmt mlipata wapi wakati hamuwezi kuchangia gharama za muungano miaka nendarudi.
 

Joka kuu.

Ahsante sana kwa Uliyotuwekea LAKIN ULICHOWEKA SIO RIPOTI YA MAPATO YA MUUNGANO NA ZNZ. Bali umetuwekea RIPOTI YA STADI YA VYANZO VYA MAPATO YA MUUNGANO.

Ulichokiweka kinaonyesha mapato ya muungano tu hivyo itakuwa taabu sana kujuwa mapato ya Znz ambayo akina Nguruvi3 wanasema ni Bil 240.

Lakin kwa kusaidia kidogo hebu pitia jedwali la 2 ambalo linaonyesha makusanyo ya ushuru wa forodha. hapo utaona Znz wanakusanya zaidi kutokana na idadi yake ya watu ukilinganisha na Tanganyika ambayo ina idadi kubwa ya watu.

lakin cha kujifunza hapo katika stadi hii ni mapendekezo ambayo yameweka bayana haya:

Stadi hii imetoa mapendekezo mbalimbali ya kuboresha Vyanzo vya Mapato ya Muungano vilivyopo, na kupanua wigo wa kodi kwa lengo la
kuongeza Mapato ya Muungano. Mapendekezo hayo ni pamoja na yafuatayo:-
i)
Kuweka utaratibu utakaowesha kutenganisha mapato ya Muungano na yasiyo ya Muungano, kwa Asasi ambazo hazina utaratibu huo.
ii)
Kukuza mapato ya ndani ya Kodi na yasiyo ya Kodi kwa lengo la kuongeza mapato ya Muungano, ili kukabiliana na tishio la upungufu wa mapato yatokanayo na Ushuru wa Forodha kutokana
na Tanzania kuwa mwanachama wa Jumuiya za ushirikiano wa Kikanda.
iii)
Sera na Sheria zinazotoa vivutio vya uwekezaji kwa kutoa misamaha ya kodi kupitiwa upya kwa lengo la kuziba mianya ya upotevu wa mapato.


 
Yaani hizo kashfa,stereotypes na prejudices ndo ulizofundishwa!?

Hivi ni kweli kwa yakini unayaamini hayo uloandika hapo;yakuwa Wazanzibar hawajui asilan hisabati/takwimu!? Duh!!

Pole yako!

Mufti Barubaru naUlamaa Boko Haram...tafadhali wala nyie msichambue lolote/chochote,maana sie "hatujasoma" pia ati ni "wavivu" wa kusoma..."hatujui! kusoma wala kuandika!? Ndo yaleyale!

Al Akhiy,hawa jamaa zetu hamuwawezi kwa malumbano yaso tija,shughulikeni nao tu pale mjisikiapo mna fursa/wasaa wa kuchezea...khasa huyu Nguruvi3!

Ahsantani.
Nadhani unaona ushahidi mwenyewe, hivi jamii inapoamini kuwa waziri wa mambo ya nje anatoa VISA hapo kuna kitu gani kwa lugha nyepesi.
Jamii inapoamini kuna ghost minister wa mambo ya nje wa SMZ hapo kuna nini kwa lugha yenu.

Nitajie kongamano, warsha, jumuiko, kiongozi au mzanzibar yoyote ambaye katika mjadala wa muungano ameshaweka namba na kuzijadili.

Nionyeshe wapi Maalim, Jusa, Manosur, Ahmed Rajab, Himid n.k. wamewahi kutamaka namba za kuendesha muungano uwe wa mkataba, uswiss, ujerumani na china n.k niambie wapi. Never
Wao ni kupanga nafasi za vyeo na ajira tu, utamaduni wa starehe na kubebwa tu

gombesugu hivi mtu anapochangia 0 na kutaka apewe 50 mtu huyo anajua hesabu kweli?
Watu wanalala hawajui bili ya umeme
Wanalipiwa mishaharaa
wanasomeshewa watoto
Wanapewa ulinzi wasiojua gharama zake
Halafu wanapewa 4.5 ambayo ni kubwa kuliko walichovuna kwa miezi 12(240) buree!
Wanapewa nafasi kwasababu ya uzanzibar na si academic qualification

Bado wanasema wanataka zaidi hata kile wasichochangia. Bilioni 240 ndizo zipo mbele yetu
Mwambie Barubaru taarifa ya JFC ipo hapo tunamsubiri afungue kinywa, keshakimbia kwasababu kuna namba

Ninafurahi sana mnaponishambulia mimi binafsi na si hoja zangu kwasababu mnajua ni ukweli.
Nitapiga mfupa mimi sina haya na kupe.

Narudia bila kumung'anya maneno ukitaka kuongea na mzanzibar ongea hadithi, ngano, mahoka na uzushi. Ukitaka aondoke katika jamvi mtupie namba 1-10. Na urafiki unaweza kwisha.


Tuacheni tupumue jamani, zigo la karafuu miaka mingi migongo imepinda. Tuacheni chonde chonde



 
Kama serikali 3 ni mzigo wasioweza kuubeba, wakati huohuo serikali 2 zinaonekana kama zinawanyonya ila hazina madhara kwa watu wa Tanganyika (kichekesho), basi turidhie serikali moja. Serikali moja ndio suluhisho pekee kwani kama ilivyo kwa mzanzibar, itakuwa pia sawa kwa mtanganyinka kufaidi matunda yote ndani ya jamhuri. Haitaishia kuwa hiki ni chetu na hivi ni vyetu.

Serikali moja itaondoa msururu wa maraisi, makamu wa maraisi, mawaziri, wabunge/wawakilishi n.k Itakuwa ahueni ya kufa mtu, ila wenye uroho wa madaraka watakuwa wamechinjiwa baharini.

Je, hao wahafidhina wapo tayari kuiona Tanzania moja?
 
Yaani hizo kashfa,stereotypes na prejudices ndo ulizofundishwa!?

Hivi ni kweli kwa yakini unayaamini hayo uloandika hapo;yakuwa Wazanzibar hawajui asilan hisabati/takwimu!? Duh!!

Pole yako!

Mufti Barubaru naUlamaa Boko Haram...tafadhali wala nyie msichambue lolote/chochote,maana sie "hatujasoma" pia ati ni "wavivu" wa kusoma..."hatujui! kusoma wala kuandika!? Ndo yaleyale!

Al Akhiy,hawa jamaa zetu hamuwawezi kwa malumbano yaso tija,shughulikeni nao tu pale mjisikiapo mna fursa/wasaa wa kuchezea...khasa huyu Nguruvi3!

Ahsantani.

Al Akhiy Gombesugu.

Unajuwa wenzetu wanapita zile skuli za jumapili (sunday school) na skuli za st.. st.. na hata vyuo vya st.. st.. hivyo hawajui kitu zaidi ya kulalama na kunung'unika tu.

Hebu fikiri unamwambia mtu tupe ripoti ya mapato ya Muungano na Znz yeye analeta stadi kisha anasema Ripoti si vichekesho hivyo.

Lakin tartibu nafikiri DATA zinawaingia na kuona ukweli na wenyewe watajiona kuwa wanachemka.

Shukran mkuu kwa maandiko yako.
 
gombesugu,

..OK, nimekuelewa kuhusu msimamo wako kwambo MOU ni sehemu ya mjadala huu.

..sasa nina maswali yafuatayo:

1. je Znz ina uwezo wa kuchangia masuala ya muungano sawa na Tanganyika?

2.je Znz ina uwezo wa kuchangia MOU na masuala ya muungano sawa na Tanganyika?

..mwisho, kwa msaada niwasilisha ripoti ya Joint Finance Committee ambayo Barubaru aliomba tuiwasilishe.

http://jfc.go.tz/downloads/mapato.pdf

cc Nguruvi3
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom