Barubaru
JF-Expert Member
- Apr 6, 2009
- 7,161
- 2,325
Nadhani unaona ushahidi mwenyewe, hivi jamii inapoamini kuwa waziri wa mambo ya nje anatoa VISA hapo kuna kitu gani kwa lugha nyepesi.
Jamii inapoamini kuna ghost minister wa mambo ya nje wa SMZ hapo kuna nini kwa lugha yenu.
Nitajie kongamano, warsha, jumuiko, kiongozi au mzanzibar yoyote ambaye katika mjadala wa muungano ameshaweka namba na kuzijadili.
Nionyeshe wapi Maalim, Jusa, Manosur, Ahmed Rajab, Himid n.k. wamewahi kutamaka namba za kuendesha muungano uwe wa mkataba, uswiss, ujerumani na china n.k niambie wapi. Never
Wao ni kupanga nafasi za vyeo na ajira tu, utamaduni wa starehe na kubebwa tu
gombesugu hivi mtu anapochangia 0 na kutaka apewe 50 mtu huyo anajua hesabu kweli?
Watu wanalala hawajui bili ya umeme
Wanalipiwa mishaharaa
wanasomeshewa watoto
Wanapewa ulinzi wasiojua gharama zake
Halafu wanapewa 4.5 ambayo ni kubwa kuliko walichovuna kwa miezi 12(240) buree!
Wanapewa nafasi kwasababu ya uzanzibar na si academic qualification
Bado wanasema wanataka zaidi hata kile wasichochangia. Bilioni 240 ndizo zipo mbele yetu
Mwambie Barubaru taarifa ya JFC ipo hapo tunamsubiri afungue kinywa, keshakimbia kwasababu kuna namba
Ninafurahi sana mnaponishambulia mimi binafsi na si hoja zangu kwasababu mnajua ni ukweli.
Nitapiga mfupa mimi sina haya na kupe.
Narudia bila kumung'anya maneno ukitaka kuongea na mzanzibar ongea hadithi, ngano, mahoka na uzushi. Ukitaka aondoke katika jamvi mtupie namba 1-10. Na urafiki unaweza kwisha.
Tuacheni tupumue jamani, zigo la karafuu miaka mingi migongo imepinda. Tuacheni chonde chonde
Nguruvi3.
Ahali yangu kila wakti nakwambia acha kukurupuka na chuki zako hizo . Je umeshindwa kuisoma hiyo iliyowekwa ni RIPOTI YA STADI YA VYANZO VYA MAPATO YA MUUNGANO. Sasa nilichokwambia utafute ni RIPOTI YA MAPATO YA MUUNGANO ambayo inatoka kila mwaka. Hiyo itakuongoza.
Lakin sikuweza kukuacha hivi hivi hata hiyo nimeiweka hadhwarani uone namna waZnz wachache (chini ya 1.4 mil) wana makusanyo makubwa kuliko wa Tz (zaidi ya 45 mil). Pitia jedwali la 2 uone hayo.