Yussuf Manji, Omba Toba

Yussuf Manji, Omba Toba

Hakuna anaeomba mabaya isipokuwa Mwenyezi Mungu kaahidi, anayedhulumu huzidishiwa hasara.

Manji hakuombewa mabaya, Manji kashtakiwa kwa Mwenyezi Mungu.

Na sasa tunamkumbusha aombe toba.
Huo ni uongo Manji hakudhulumu BAKWATA ndiyo waliowadhulumu. Hata hivyo yampatayo Manji yengempata tu awe ameshitakiwa kwa Mungu au hajashitakiwa as long as haonewi
 
Huo ni uongo Manji hakudhulumu BAKWATA ndiyo waliowadhulumu. Hata hivyo yampatayo Manji yengempata tu awe ameshitakiwa kwa Mungu au hajashitakiwa as long as haonewi


Taarifa hii imfikie yeyote anayehusika.
 
Mimi nilijifundisha kung fu hapo YWCA Dar 70s.

Wanaojilipua na kufanya vitendo vya kigaidi ni hatari zaidi ya Manji.Waombeeni hao nao wapate Mikosi na mabalaa ili wapotee kwenye uso wa dunia ya wastaarabu.
 
Faiza elewa Manj sio wa kulaumiwa asilimia 100. Bakwata na hao masheikh ndio wa kulaumiwa kwani Mali nyingi za waislam inayosimamiwa na bakwata zimeuzwa kinyemela.
Manji alitakiwa ajitambue na sio jeuri ya Pesa kwa waislamu wenzake.. Hivi leo watu wachache kama ilivyotokea kwa Bakwata watangaze kuuza mali yoyote ya wakfu, wewe kama unajitambua unaweza kununua kweli.? Ilhali unajua kuwa mali ikitolewa kwa ajili ya Umma au Wakfu ni haramu mtu kununua. Manji aliangalia faida zaidi ya mali kuliko hasara kwa waislamu kupoteza mali zao

Acha yampate yenye kumpata, kwangu sina uwezo wa kumsamehe ila mungu aliyemuumba ndo anajua zaidi waja wake
 
Wanaojilipua na kufanya vitendo vya kigaidi ni hatari zaidi ya Manji.Waombeeni hao nao wapate Mikosi na mabalaa ili wapotee kwenye uso wa dunia ya wastaarabu.


Tunaomba usiku na mchana na waeshaanza kumalizana wenyewe kwa wenyewe.
 
Yussuf Manji, ni matumaini yangu kuwa ujumbe huu utakufikia popote ulipo.

Binafsi kama Muislam mwenzako nnachukuwa fursa hii kukukumbusha kuwa hakuna kitu bora kama kukiri na kukubali makosa yako na kuomba toba.

Toba nnayokushauri kuiomba hapa, si kwa serikali wala kwa watawala. Toba nnayokukukumbusha mimi kuiomba ni kwa Mola wako Muumba mbingu na ardhi.

Manji uliwakosea sana Waislam kipindi cha nyuma kiasi, kwa kutumia fedha zako kununulia viwanja vya wakf vya Waislam, na kuwa mkaidi kila uliposemeshwa kuhusu hilo.

Viwanja hivyo ambavyo historia inaonyesha kuwa vilikuwa vijengwe chuo kikuu cha kwanza Tanganyika (hilo halikufanyika lakini hilo ni simulizi jingine kabisa ambalo Alama Mohamed Said anaweza kulisimulia vizuri zaidi).

Ulifatwa na Waislam wakikuomba kuwa mkataba ulioingia na BAKWATA ni wa kidhalimu na haufai lakini kwa ukaidi wako hukuwasikiliza na uliwatoa njiani na kuendelea na mkataba wako.

Sakata la viwanja hivyo lilipelekea Waislam kufungwa, kupigwa na kujeruhiwa mpaka walipoona kuwa hawakuwezi kwa ajili ya kutumia fedha zako na nguvu ya baadhi ya waliokuwa BAKWATA, Waislam wakafikia maamuzi makali ya kuwa sasa wanakushtaki kwa Mwenyeezi Mungu.

Miaka imepita ukidhani kuwa shtaka hilo halina meno kwako, lakini leo tunashuhudia ukigeukwa kila upande.

Aibu ya kushikwa na kuwekwa ndani pekee si ndogo kwa mtu wa "caliber" yako. Licha ya kupimwa na kukutwa kuwa u mlevi wa madawa, tumeona sakata la Oysterbay likikutia hasara kubwa sana, tumeona wafanyakazi wako wakifungiwa kuingia kwenye ofisi zao, tunasikia akaunti zako zinafungiwa kila kukicha.

Kama hiyo haitoshi, tunasikia umepatwa na matatizo ya moyo. Mwenyezi Mungu anasema katika Qur'an tukufu:

Qur'an 2:10. Nyoyoni mwao mna maradhi, na Mwenyezi Mungu amewazidishia maradhi. Basi watakuwa na adhabu chungu kwa sababu ya kusema kwao uwongo. Maelezo

Kwa yote hayo bado tu hujashtuka ni kwanini yakukute yote hayo? Nakusihi, zingine zote ni sababu lakini ukweli unabaki kuwa ukweli, Waislam wameitikiwa dua zao dhidi yako.

Yussuf Manji tunakutaka usiwe katika wale ambao:

Qur'an 2:7. Mwenyezi Mungu amepiga muhuri juu ya nyoyo zao na juu ya masikio yao, na juu ya macho yao pana kifuniko. Basi watapata adhabu kubwa. Maelezo

Kwa kuwa Mwenyezi Mungu ni wingi wa kusamehe na hachoki kusamehe, tunakutaka uombe toba kwa mola wako, umtake radhi, uwatake radhi na Waislam na uwarudishie viwanja vyao na mali zao, tena usithubutu kuvirudisha kwa wale wale waliokuuzia, itakuwa haina maana kabisa. Virudishe kwenye taasisi za Kiislam zenye kumuogopa Mwenyezi Mungu au tumia viwanja hivyo hivyo kuanzisha Manji Islamic Trust Fund na uiendeshe mwenyewe kwa manufaa ya Waislam.

Fata nasaha hizo uone mambo yatavyokunyookea.

Jikumbushe:

Maimamu kumsomea Manji Ahla-badri

Mjue Sheikh Ponda Issa Ponda na Kundecha

Waislamu wataka jengo lao toka Quality Group | Bongo5.com

MKATAMBUGA: WAISLAMU WAMELOGWA NA NANI?

Manji hakuna wakukuokoa katika haya na hayatokwisha ukifanya dharau isipokuwa wewe mwenyewe, anza kwa kumrudia Allah na kumuomba toba.

Na Mwenyeezi Mungu ndiye ajuwae zaidi.

Matajiri huwa wako busy sana kutafuta sidhani kama anaweza soma au kutekeleza Barua yako, achilia mbali kuingia hapa jamii forums .. wao wana Focus sana ndo character yao kubwa na ndo imewafikisha hapo walipo
 
Yussuf Manji, ni matumaini yangu kuwa ujumbe huu utakufikia popote ulipo.

Binafsi kama Muislam mwenzako nnachukuwa fursa hii kukukumbusha kuwa hakuna kitu bora kama kukiri na kukubali makosa yako na kuomba toba.

Toba nnayokushauri kuiomba hapa, si kwa serikali wala kwa watawala. Toba nnayokukukumbusha mimi kuiomba ni kwa Mola wako Muumba mbingu na ardhi.

Manji uliwakosea sana Waislam kipindi cha nyuma kiasi, kwa kutumia fedha zako kununulia viwanja vya wakf vya Waislam, na kuwa mkaidi kila uliposemeshwa kuhusu hilo.

Viwanja hivyo ambavyo historia inaonyesha kuwa vilikuwa vijengwe chuo kikuu cha kwanza Tanganyika (hilo halikufanyika lakini hilo ni simulizi jingine kabisa ambalo Alama Mohamed Said anaweza kulisimulia vizuri zaidi).

Ulifatwa na Waislam wakikuomba kuwa mkataba ulioingia na BAKWATA ni wa kidhalimu na haufai lakini kwa ukaidi wako hukuwasikiliza na uliwatoa njiani na kuendelea na mkataba wako.

Sakata la viwanja hivyo lilipelekea Waislam kufungwa, kupigwa na kujeruhiwa mpaka walipoona kuwa hawakuwezi kwa ajili ya kutumia fedha zako na nguvu ya baadhi ya waliokuwa BAKWATA, Waislam wakafikia maamuzi makali ya kuwa sasa wanakushtaki kwa Mwenyeezi Mungu.

Miaka imepita ukidhani kuwa shtaka hilo halina meno kwako, lakini leo tunashuhudia ukigeukwa kila upande.

Aibu ya kushikwa na kuwekwa ndani pekee si ndogo kwa mtu wa "caliber" yako. Licha ya kupimwa na kukutwa kuwa u mlevi wa madawa, tumeona sakata la Oysterbay likikutia hasara kubwa sana, tumeona wafanyakazi wako wakifungiwa kuingia kwenye ofisi zao, tunasikia akaunti zako zinafungiwa kila kukicha.

Kama hiyo haitoshi, tunasikia umepatwa na matatizo ya moyo. Mwenyezi Mungu anasema katika Qur'an tukufu:

Qur'an 2:10. Nyoyoni mwao mna maradhi, na Mwenyezi Mungu amewazidishia maradhi. Basi watakuwa na adhabu chungu kwa sababu ya kusema kwao uwongo. Maelezo

Kwa yote hayo bado tu hujashtuka ni kwanini yakukute yote hayo? Nakusihi, zingine zote ni sababu lakini ukweli unabaki kuwa ukweli, Waislam wameitikiwa dua zao dhidi yako.

Yussuf Manji tunakutaka usiwe katika wale ambao:

Qur'an 2:7. Mwenyezi Mungu amepiga muhuri juu ya nyoyo zao na juu ya masikio yao, na juu ya macho yao pana kifuniko. Basi watapata adhabu kubwa. Maelezo

Kwa kuwa Mwenyezi Mungu ni wingi wa kusamehe na hachoki kusamehe, tunakutaka uombe toba kwa mola wako, umtake radhi, uwatake radhi na Waislam na uwarudishie viwanja vyao na mali zao, tena usithubutu kuvirudisha kwa wale wale waliokuuzia, itakuwa haina maana kabisa. Virudishe kwenye taasisi za Kiislam zenye kumuogopa Mwenyezi Mungu au tumia viwanja hivyo hivyo kuanzisha Manji Islamic Trust Fund na uiendeshe mwenyewe kwa manufaa ya Waislam.

Fata nasaha hizo uone mambo yatavyokunyookea.

Jikumbushe:

Maimamu kumsomea Manji Ahla-badri

Mjue Sheikh Ponda Issa Ponda na Kundecha

Waislamu wataka jengo lao toka Quality Group | Bongo5.com

MKATAMBUGA: WAISLAMU WAMELOGWA NA NANI?

Manji hakuna wakukuokoa katika haya na hayatokwisha ukifanya dharau isipokuwa wewe mwenyewe, anza kwa kumrudia Allah na kumuomba toba.

Na Mwenyeezi Mungu ndiye ajuwae zaidi.
Ujumbe mzuri na si kwa Manji tu na kwa waislam wote wasiojielewa, na wako wengi mali na vyeo vianawadanganya thank you sister.
 
Wanajukwaa kuna wengi hua mnasoma tu kwa Mzee Mohamed Said story za kariakoo na jinsi vijana wa mzizima walivyokua mnasahau wakazi wa mzizima miaka ile kufika bara tu ilikua ni kosa la jinai , zaidi watu wa bara kufika mjini na kujitutumua hasa wale viongozi na vijakazi hadi kuambiwa utalijua jiji , nasema haya kwa baadhi yenu kutoijua nchi na hiyo Dar mmefika kusoma chuo tu mjitahidi sana kua na adabu kwa watu kama akina Faiza Foxy.
 
Wakati ukiwaza kutoka bariadi, kasulu, mbinga, ndungu, moshi, karagwe ufike Dar kutafuta maisha vijana wa mzizima walitahayari kuiacha mnazi mmoja na jiji kwenda bondeni au mamtoni kusaka maisha iwe kwa kuzamia au kihalali , jukwaa lisitufanye tudhihaki watu,
 
Kibri ya akina Manji sio ya jana wala juzi ni ya muda mrefu sana na alidharau taasisi za kiislaam na kuuvuruga uislam kwa kadri alivotaka yeye na hakusikia wala kuambiwa zaidi ya kuwasikiliza maimam na masheikh walokunywa nae kahawa. Sasa afuate ushauri na Kwa kua Mwenyezi Mungu Mwingi Wa Rehma ni Mwenye huruma pia atamsaidia na kumwondolea mzigo alionao.
 
Back
Top Bottom