Yupo wapi mwanaharakati huyu wa UDSM?

Yupo wapi mwanaharakati huyu wa UDSM?

Ha ha ha ha ha ha jamaa yangu sana huyu,Mkerewe wa Mwanza...huyu jamb anamwaga sumu kwa Wanafunzi huko Magu,jamaa ni Mwalimu wa History na GS...anamwaga sumu ni balaa kwa watoto,alikoswakoswa sana katika taflani ya Odwang Odor(?)
Me nimemkumbuka sana huyu Mganda Odwagi Odor.
Mwenye habari kumuhusu huyu jamaa atujuze.

Nilipewa simulizi take kwa ufupi na Dada yangu aliyepitia Udsm enzi hizo.

Mwenye kumjua huyu mganda atujuze zaidi.
 
Odwangi Odor hakuwa mtz ...nakumbuka aligombea urais udsm akapigwa chini
 
Kijicho nishawai kumuona pande fulani za Golani nyuma ya chuo huku karibu na msewe!!!!amechoka kinyama na hajarudishwa chuo mpk leo!!!!!!anakaa na mwanaharakati mwenzie anaitwa Bocassa!!maisha yao ni magumu sana!!Bocassa baada ya kufukuzwa chuo sasa ni dereva bodaboda!

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
Aisee alshababu yuko wapi na yule mdada waliongoza mgomo 2010
 
Nakumbuka hata mie nilifunga geti pale mabibo. Na kandamana from mabibo to chuo na tukakaa mataa katikati
 
Kawambwa aliungua na jua wanafunzi walishusha kivuli alichokuwa ameandaliwa, Tuliwarushia FFU/Police chupa za maji wakati wanamrunda Kawamba aondoke eneo la tukio. Walirusha mabomu ya machozi balaa... Siku ile nilikoswa koswa na bomu la machozi likaanguka pembeni yangu (Sita sahau aisee).
Uchaguzi uliofuata nikagombea urais wa DARUSO.......a.k.a Jembe, nilitingisha sana bahati mbaya nilikua CONAS na mpinzani wangu mkuu alikua CASS tena BAED unategemea nn hapo.....??? All in all bado harakati zinaendelea Mungu akituweka hai 2020 tutaunguruma mahali, nawasalimu wadau wote mlioko humu
 
Dah, sitaisahau UD katika maisha yangu 2006-009 ilikuwa ni Kama chuo cha nyota za medani jeshini. Kila mtu alikuwa fighter utake usitake nature inakufanya upambane.

Kila semester palikuwa na harufu ya mgomo na kufukuzwa chuo, watoto wa mama na mboga saba waliumia sana kipindi hiki hasa wale wa hall 7
 
Rich alianzia kazi Bukoba na nilikuwa nafundisha naye shule moja ila kwa sasa kahama yupo Mwanza Pamba sekondari....Jamaa ni mwanaharakati hadi leo....
Owawa pia yupo ofisi ya CAG Bukoba
 
Kijicho nishawai kumuona pande fulani za Golani nyuma ya chuo huku karibu na msewe!!!!amechoka kinyama na hajarudishwa chuo mpk leo!!!!!!anakaa na mwanaharakati mwenzie anaitwa Bocassa!!maisha yao ni magumu sana!!Bocassa baada ya kufukuzwa chuo sasa ni dereva bodaboda!

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Japo simkumbuki Kaemba lakini Udsm ya 2006-2010 ilikuwa balaa tupu kila semista lazima mgomo na maandamano na kila mwaka chuo kufungwa... peoplez kama Mtatiro(PM), Deo Daud (rais), Odong, Bush, Dady Igogo, Owawa, Silinde, Aristotle, n.k ziliyumbisha utawala wa chuo na serikali. karibu kila mwanachuo alikuwa mwanaharakati naikumbuka Red guard ya Mtatiro nikiwa first year tulifanya makubwa ya kuwatia mboko students na malekchara wapinga migomo. katika uwepo wangu udsm chuo kilifungwa mara 2 sababu ya migomo tukarudishwa nyumban 2007 na 2008. saa hizi sijui matatizo yameisha chuoni au wanafunzi radicals ndo wameisha??
Radical watoke wapi ,sasa hivi mashoga wengi.

Imagine hadi leo wanafunzi hawajapata field allowances.

Wanafunzi wa siku hizi wanadhani watapewa hela na haki zao na serikali kwa kukodisha matarumbeta na nyimbo za kuisifu


Poor them
 
Huyu alishababy yupo wapi na kabinti kamoja hivi kaa arusha pamoja na sokwe huyu kaemba nazani yupo uvinza halmashauri ila sijui yupo idara gani.
 
Ha ha ha ha ha ha jamaa yangu sana huyu,Mkerewe wa Mwanza...huyu jamb anamwaga sumu kwa Wanafunzi huko Magu,jamaa ni Mwalimu wa History na GS...anamwaga sumu ni balaa kwa watoto,alikoswakoswa sana katika taflani ya Odwang Odor(?)
Yeah alikoswa koswa .Alikuwa noma sana huyu jamaa.Nyakati za migomo mtatiro Alikuwaga anamtumia sana Ku mobilize man power
 
Kuna watu uharakati wao ulihamasishwa na mob psychology ya UDSM, nje ya UD! they are nothing!. Wako wapi kina Sikitiko Kapile , Emile Kivugo, kina Bazigiza baada ya UDSM?!.
P.
But sio Kwa Kaemba mkuu.He was something else
 
Magu shule gani? Lkn mie simfaham. Kwangu mie maarufu walikuwa owawa, mtatiro, bushi, na odwaa! Ni harakati zao zilifanikisha kuwepo kwa means testing results, ni harakati zao wanafunzi wa vyuo private walianza kupata mikopo na ni harakati zao hadi div iii walianza kupata mikopo. Kabla ya hapo ilikuwa 1 kwa social science na 2 kwa science na ualimu.
Hao kina Owawa and company, Kaemba alikuwa right hand man wao. Harakati zao zisingeweza kufanikiwa bila amsha amsha ya watu kama Kaemba
 
Tulikutakaga story zake nasikia alimchallenge sana kipara??

raisi msaliti aliyepita kwa kishindo
Wakati Kipara anakuwa Rais , Kaemba Alikuwa tayari amemaliza chuo coz Kaemba alimaliza 2009 na Kipara alikuwa Rais 2010/2011.

Ila walikuwa wanajuana coz wote watoto wa Mwanza, Kaemba mkerewe Kipara msukuma ..

And wakati Kipara anaanza first year alikuwa mwanaharakati mzuri sana. Alikuja kuchange baada ya kuingia madarakani
 
huyo odwang alikuwaga mtoto wa joseph koni wa lord resistance army??maana nilikuwaga bado sijajiunga hapo ila story zake nilipata juu juu
Hapana ulikuwa uzushi tu but his father alikuwa mpinzani wa M7 na inasemekana Alikuwa na mkwanja mrefu sana. Hata ishu ya Odong kufukuzwa chuo na.kurudishwa Uganda inasemekana kulikuwa na mkono wa M7 pia
 
Hivi kwann wana harakati wengi wanatokea collage nyingine na sio CoET, au huko kwa wenzetu shule yao nyepesi paka wanapata mda wa kutosha kufanya na uarakati.
 
Back
Top Bottom