Ngwananzengo
JF-Expert Member
- Jul 28, 2012
- 1,911
- 1,320
Ni kweli siku hazigandi. Katika awamu ya Tatu tulimwona Mama Anna Mkapa akizunguka huku na kule kwa mwamvuli wa "Fursa sawa kwa wote".
Hakuchi Hakuchi mwisho hucha, Muda ulipofika Mama Anna Mkapa akaondoka na Mama Salma Kikwete akashika usukani. Yeye kama ilivyokuwa kwa mtangulizi wake alizunguka huku na kule kwa mwamvuli wa WAMA. Lengo na nia ni kuwainua wanawake na kuchochea juhudi zao katika kujiletea maendeleo.
Awamu ya Tano imeingia kwa kishindo. Tofauti na awamu mbili za nyuma "First lady" wa awamu hii hajionyeshi kama ni mtu mwenye kupenda kuonekana. Hili lilijionyesha katika kampeni za uchaguzi lakini linadhidi kudhihirika kadri Muda unavyosonga.
Swali la kujiuliza "Yupo wapi First Lady"? Je, angali anajipanga kuona aifanyie nini jamii au atakuwa kimya kama wakati wa kampeni?
Hakuchi Hakuchi mwisho hucha, Muda ulipofika Mama Anna Mkapa akaondoka na Mama Salma Kikwete akashika usukani. Yeye kama ilivyokuwa kwa mtangulizi wake alizunguka huku na kule kwa mwamvuli wa WAMA. Lengo na nia ni kuwainua wanawake na kuchochea juhudi zao katika kujiletea maendeleo.
Awamu ya Tano imeingia kwa kishindo. Tofauti na awamu mbili za nyuma "First lady" wa awamu hii hajionyeshi kama ni mtu mwenye kupenda kuonekana. Hili lilijionyesha katika kampeni za uchaguzi lakini linadhidi kudhihirika kadri Muda unavyosonga.
Swali la kujiuliza "Yupo wapi First Lady"? Je, angali anajipanga kuona aifanyie nini jamii au atakuwa kimya kama wakati wa kampeni?