KIM JONG
JF-Expert Member
- Jun 11, 2013
- 213
- 57
Wanajamvi,
Moja ya watu wanaokumbukwa sana kutokana na kutoa lugha kali na pengine za matusi ili kulazimisha hoja alikuwa ni mkuu wa kitengo cha propaganda wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Bwana Richard Tambwe Hiza. Ninamkumbuka sana pale alipokuwa ni mwanachama wa Chama cha Wananchi CUF ambapo aligombea ubunge mara kadhaa katika jimbo la Temeke kupitia tiketi ya chama hicho bila mafanikio.
Ninamkumbuka sana wakati ule akiwa CUF akijitahidi sana kujenga hoja zenye mashiko na zinazovutia ingawa mara zote alizogombea ubunge alishindwa. Naamini mwaka 2005 kama ushindani ungekuwa wa haki na bila uchakachuaji pengine engeweza kutawazwa kuwa mbunge wa kwanza wa CUF kushinda jimbo la Temeke.
Baada ya uchaguzi wa 2005 Tambwe Hiza aliingia kwenye ulingo wa kutunishiana misuli na baadhi ya viongozi ndani ya chama chake na baadaye tukasikia kuwa amerudi CCM. Jambo hilo liliudhi wapenda mageuzi (wapenda mabadiliko na maendeleo) wengi kwani lilitukumbusha usaliti wa aina hiyo ulioishawahi kufanywa na Mwenyekiti wa CCM wa sasa wa mkoa wa Kigoma Dr. Aman Walid Kabourou kwa kuhama chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na kuhamia CCM. Inaaminika kuwa Dr. Kabourou alikunja kibindoni mwake kitita cha mamilioni ya shilingi kwa usaliti huo! na damage aliyoifanya Dr. Kabourou kwa Chadema na wapenda mabadiliko wote nchini ilikuwa kubwa sana hasa tukizingatia ushawishi binafsi aliokuwa nao wakati huo katika mkoa wa Kigoma.
Mara Tambwe Hiza naye akatangaza kurudi CCM (Sijui naye alikunja ngapi?). Alizungushwa katika majukwaa ya mikutano mbalimbali ya CCM na baadaye akalipwa fadhila ya kupewa cheo ambacho mwanzoni hakikuwepo, yeye pamoja na Bwana Msabaha (aliyetokea CUF pia), cheo kilichokuja kujulikana baadaye kama Mkuu wa Kitengo cha Propaganda wa Chama cha Mapinduzi (CCM).
Hapo ndipo ninapomkumbuka sana kwani kuanzia hapo alipagawa! Alikuwa akitoa maneno makali na hata yenye kashfa kujaribu kukitetea na kukilinda chama chake kipya cha CCM hata pale ambapo haikustahili hata chembe. Alilazimisha sana hoja zake zionekane ni bora ingawa hata kwa mtu wa kawaida kabisa aliona ni pumba tupu. Baadaye akaanza kuporomosha matusi ili kuhalalisha ushabiki wake (ushabiki bandia). Baada ya miezi kadhaa ikadhihirika kuwa haikuwa propaganda bali ni hoza za kutumia nguvu na matusi.
Nilisikia mara ya mwisho kuwa aliugua shinikizo la damu akalazwa hospitali hapa hapa Bongo lakini tokea wakati huo sijamsikia tena. YUPO WAPI TAMBWE HIZA?
Moja ya watu wanaokumbukwa sana kutokana na kutoa lugha kali na pengine za matusi ili kulazimisha hoja alikuwa ni mkuu wa kitengo cha propaganda wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Bwana Richard Tambwe Hiza. Ninamkumbuka sana pale alipokuwa ni mwanachama wa Chama cha Wananchi CUF ambapo aligombea ubunge mara kadhaa katika jimbo la Temeke kupitia tiketi ya chama hicho bila mafanikio.
Ninamkumbuka sana wakati ule akiwa CUF akijitahidi sana kujenga hoja zenye mashiko na zinazovutia ingawa mara zote alizogombea ubunge alishindwa. Naamini mwaka 2005 kama ushindani ungekuwa wa haki na bila uchakachuaji pengine engeweza kutawazwa kuwa mbunge wa kwanza wa CUF kushinda jimbo la Temeke.
Baada ya uchaguzi wa 2005 Tambwe Hiza aliingia kwenye ulingo wa kutunishiana misuli na baadhi ya viongozi ndani ya chama chake na baadaye tukasikia kuwa amerudi CCM. Jambo hilo liliudhi wapenda mageuzi (wapenda mabadiliko na maendeleo) wengi kwani lilitukumbusha usaliti wa aina hiyo ulioishawahi kufanywa na Mwenyekiti wa CCM wa sasa wa mkoa wa Kigoma Dr. Aman Walid Kabourou kwa kuhama chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na kuhamia CCM. Inaaminika kuwa Dr. Kabourou alikunja kibindoni mwake kitita cha mamilioni ya shilingi kwa usaliti huo! na damage aliyoifanya Dr. Kabourou kwa Chadema na wapenda mabadiliko wote nchini ilikuwa kubwa sana hasa tukizingatia ushawishi binafsi aliokuwa nao wakati huo katika mkoa wa Kigoma.
Mara Tambwe Hiza naye akatangaza kurudi CCM (Sijui naye alikunja ngapi?). Alizungushwa katika majukwaa ya mikutano mbalimbali ya CCM na baadaye akalipwa fadhila ya kupewa cheo ambacho mwanzoni hakikuwepo, yeye pamoja na Bwana Msabaha (aliyetokea CUF pia), cheo kilichokuja kujulikana baadaye kama Mkuu wa Kitengo cha Propaganda wa Chama cha Mapinduzi (CCM).
Hapo ndipo ninapomkumbuka sana kwani kuanzia hapo alipagawa! Alikuwa akitoa maneno makali na hata yenye kashfa kujaribu kukitetea na kukilinda chama chake kipya cha CCM hata pale ambapo haikustahili hata chembe. Alilazimisha sana hoja zake zionekane ni bora ingawa hata kwa mtu wa kawaida kabisa aliona ni pumba tupu. Baadaye akaanza kuporomosha matusi ili kuhalalisha ushabiki wake (ushabiki bandia). Baada ya miezi kadhaa ikadhihirika kuwa haikuwa propaganda bali ni hoza za kutumia nguvu na matusi.
Nilisikia mara ya mwisho kuwa aliugua shinikizo la damu akalazwa hospitali hapa hapa Bongo lakini tokea wakati huo sijamsikia tena. YUPO WAPI TAMBWE HIZA?