You are not my type

You are not my type

ni ubinadamu tu..kutumia maneno mazuri kama mtu sio wa 'viwango' vyako..

.kumuambia mtu sio type yake mie naona ni dharau!...

unamuacha mtu feeling inadequate....

..anawaza saa zote hao wa type yako sijui wakoje? lol
Miss Becky sidhani kama uko sahihi, type sio kiwango, mnaweza kuwa viwango sawa lakini si type moja, mnaweza kuwa type ileile ila viwango tofauti
 
Hizo ni dharau za kiwango cha masters....eti sio aina ya mtu ninayetaka kuwa naye unanjua kiundani?
Aisee kwani mtu hadi anaamua kukataa au kukubali si maana yake amekukagua, then anasema huyu yes au no
 
Wengi wao unakuta mtu umemtingoza first time and anakujibu " You are not my type
Kwani mnakuwa mmefahamiana siku hiyo hiyo? Kama alikuwa anakufahamu mienendo yako siku nyingi. Ila si busara hata kidogo kutamka hivi hata kama mtu humkubali
 
Ila kuna wanawake wanajua kukataa hadi unajisikia poa aiseeh.

Sasa wewe unaanza maneno kibao ooh sijui sio type yangu mara nini yote ya nini.
Anaweza asikuambie ila ukasikia amesema kwa watu
 
Ni kweli blaki woman hata mimi nimesema kwamba si busara kumtamkia mtu hivyo lakini yapo na yanatamkwa, unaweza usitamke wewe ila ukatamkiwa
Yapo sana hapa tunakumbushana kuona sio maneno mazuri je ukiambia utayachukuliaje? Kwakweli ni neno litakalo kutesa maana unaweza kujiona sio mtu wa kawaida hahahah binadamu wana maneno ya karaha sana
 
Yapo sana hapa tunakumbushana kuona sio maneno mazuri je ukiambia utayachukuliaje? Kwakweli ni neno litakalo kutesa maana unaweza kujiona sio mtu wa kawaida hahahah binadamu wana maneno ya karaha sana
Hahaha ila haya huwa wanayasema mabinti wadogo, watu wazima tunayasema kiutu uzima
 
Hahahaha

Mwanamke akisema wewe sio type yake anamaanisha hujui kutongoza ...

Wakati mwanaume anamaanisha kweli wewe sio type yake..

Toka lini mwanamke akajua anataka nini .Atakaza hapo weeee na dharau juu.Akijua badae upo bank utasikia mbona upo kimya sikuhizi umechukia nilivyokwambia vile hahahaa,akaja kujua una gari utasikia hivi wewe unashughulika na nini????wanawake wachache sana wakikwambia hiyo kauli unaweza take it serious...

Binafsi nikiambiwa hivo najipanga nimekosea wapi kwenye kutongoza,je nimeshindwa wapi kuji marketing mpaka huyu mwanamke kanishinda??
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom