Mdogo wangu alifeli pale Muhimbili akiwa mwaka wa 3, alilia sana. Kilichotuumiza hata sisi familia ni kwamba kijana alikuwa vizuri sana kichwani, form four alipata div one ya point 8, form six PCB akagonga BBB (pointi sita). Tuliumia sana. Tukakaa naye na tukawa tunamchunga kila siku tukiogopa angejidhuru. Baada ya mwaka mmoja nyumbani alibadilika sana, kwanza aliyachukia kabisa yale masomo na hakutaka kuyasikia tena. Akajiunga chuo kikuu kingine kwa BA community development. Baada ya miaka 3 akamaliza na kuunga MA na baadaye PhD. Sasa hivi ni consultant wa kazi za world bank na mashirika mengine ya UN, yuko vizuri mara nyingi kuliko wale waliofaulu ile kozi ya Muhimbili aliyofeli, na ni nguvu yetu sasa kwenye familia.
Na Muhimbili walizidi sana kuwafelisha vijana wazuri, kumbe kozi zao hata hazina tija, wanaozifaulu tunawaona wanalialia tu njaa mitaani na kusimangwa hadharani na wanasiasa kuwa ni wezi wa dawa! Kwa hali ilivyo katika taaluma hiyo, mtu akifeli mtihani anatakiwa amshukuru Mungu kwa kumtoa kwenye lindi la dhiki!