Yathibitika: kuoa wake wengi huongeza umri….!

Yathibitika: kuoa wake wengi huongeza umri….!

Mtambuzi

Platinum Member
Joined
Oct 29, 2008
Posts
8,809
Reaction score
15,441
21came600.1.jpg


Imebainika kwamba kuna ukweli mkubwa kuwa wanaume wenye kufanya mapenzi halali kwa wingi au mara nyingi huishi muda mrefu zaidi. Hii ina maana pia kwamba, labda wanaume wenye wake wengi huishi muda mrefu zaidi, kuliko wale wenye mke mmoja.

Kuna wazee wengi ambao ninawafahamu wenye umri mkubwa sana. Lakini nikichunguza kwa makini naona kama wengi kati yao walikuwa au wameoa wake wengi. Inawezekana kuwa hiyo ni nasibu (coincidence)tu ya mambo, lakini kwa sehemu kubwa haionyeshi hivyo.

Ngoja nikupeni mfano wa mzee mmoja kule nchini India. Huyu mzee alifariki akiwa na umri wa miaka 84 kufuatia ajali ya gari hapo mnamo mwaka 2005. Alikuwa ameoa wanawake 91. Mzee huyu, Udaynath Dakhinaray, alianza kuoa mke wa kwanza wakati akiwa shuleni, lakini ndoa yake ilivunjika. Baada ya ndoa kuvunjika alijiapiza kwamba, ni lazima angeoa wanawake 100 katika maisha yake.

Kwa bahati mbaya, wakati akiwa na mke wa 91 alipata ajali ya gari na alifariki baadaye, bila kukamilisha ndoto yake. Lakini kufikia miaka 84 na bado kuwa na nguvu, huenda ni ushahidi kwamba, kuoa wake wengi kuna faida kwenye suala la umri.

Lakini kama ambavyo imekuwa ikisemwa siku zote, afya inayotokana na tendo la ndoa huwajia wale tu ambao wanalifanya kihalali. Hapa naomba Mzee wa Kugegeda mzabzab anisome kwa makini. Usije ukaanza kuhangaika kutafuta umri mkubwa kwa kuparamia vibinti na kuvigegeda, tutakuzika ukiwa kijana mbichi bado.

Hebu jaribu kuvuta kumbukumbu zako uwaweke mawazoni mwako wazee wote unaowafahamu, wawe hai au wawe wamekufa. Halafu jaribu kufikiri ni wangapi wamefikisha umri wa miaka 80. Najua utashangaa kwamba, ni karibu wote walikuwa wameoa wanawake wengi.

Kuna wanaosema, hiyo inatokana na ukweli kwamba, hao wanaooa wake wengi hawako wengi. Ina maana kwamba, fikiria kuhusu wazee wenye wake au waliokuwa na wake wengi, halafu fikiria wale ambao hawana wake wengi, halafu upige hesabu kwa slilimia ya wale walio hai na waliokufa, halafu weka majibu yako hapa.
 
Last edited by a moderator:
Akili zingine bure kabisa. Mzee wa India kufikisha miaka 85 kunahusianaje na kuoa wake wengi? Papa anayejiuzulu ana miaka 85 na hana mke hata mmoja, sasa huo nao tuuite uchunguzi?

Unachoshindwa kuelewa wewe ni kwamba jamii za watu waishio vijijini ndio zina taratibu za kuoa wake wengi, at the same time huko vijijini hakuna junk foods na mapochoharibu kama ya huku mijini kwa hiyo watu wanafaida ya natural life.

Umeanza na kusema IMEBAINIKA halafu badala ya kuweka takwimu za uchunguzi unatoa mifano ya wazee wawili unaowajua.
 
... Ufa mapema kwa BP.
Nenda makaburini ukakamilishe research yako. Bilashaka utakuja na majibu yanayoridhisha.
 
Oa wake watano pasua kichwa kama l...1 uone kama hata 38 utafika wewe hii its aplicabo kwa miaka ya nyuma 47yrs baki not this decade Mtambuzi kabla hujapost may you pliz activate your reasoning capacity HAVE ANICE WEEKEND
images


October 3, 2012 was the second anniversary of the death of Ancentus Ogwella Akuku, who was better known as Akuku Danger.
A Wikipediaentrance repeats the popular story that Akuku was nicknamed "Danger" because "women were very attracted by his handsome looks". He died on October 3, 2010, aged 94.
The Wikipedia post says Akuku Danger married his first wife in 1939 and became a polygamist at the age of 22.
In his life, Akuku married over 100 wives, divorced 85 on grounds of infidelity, and sired 160 children. He outlived 12 of his wives, marrying the last one in 1992.
Also, that there were so many children in his family that Akuku established two primary schools solely to educate his brood, as well as a church for his growing family to attend. I hadn't heard those details before.
There are no longer men like Akuku Danger in Kenya, or elsewhere in Africa or the world, for that matter.
The times have changed so much that in some parts of the world, if you portray yourself as a model citizen and are a leading member of your church, then it is discovered you have a secret mistress, you will have to resign your job, move away from the neighbourhood, or even emigrate in shame.
 
Akili zingine bure kabisa. Mzee wa India kufikisha miaka 85 kunahusianaje na kuoa wake wengi? Papa anayejiuzulu ana miaka 85 na hana mke hata mmoja, sasa huo nao tuuite uchunguzi?

Unachoshindwa kuelewa wewe ni kwamba jamii za watu waishio vijijini ndio zina taratibu za kuoa wake wengi, at the same time huko vijijini hakuna junk foods na mapochoharibu kama ya huku mijini kwa hiyo watu wanafaida ya natural life.

Umeanza na kusema IMEBAINIKA halafu badala ya kuweka takwimu za uchunguzi unatoa mifano ya wazee wawili unaowajua.

Huyu naye ni wa kijijini au....?

polygamy_1490320c.jpeg
 
Utafiti bado haujakamilika..na kwa sababu waoaji wa wake wengi sio wengi nyakati hizi..nachelea kusema hii research haijakamilika.....
 
Afu ulijuaje anamtokea lara 1?
huyu mzee acha tu!
Oa wake watano pasua kichwa kama l...1 uone kama hata 38 utafika wewe hii its aplicabo kwa miaka ya nyuma 47yrs baki not this decade Mtambuzi kabla hujapost may you pliz activate your reasoning capacity HAVE ANICE WEEKEND
 
Last edited by a moderator:
Unazeeka vibaya wewe baba. Unataka kujustify nini?

haya karibu urojo.

Na ukimwambia mama yako mama Ngina kama nimeandika hii makitu humu jF utanitambua......

Mie nalikuwa nafanya resech tu hapa JF kama jambo hilo lina ukweli wowote lakini kwa umbea najua utayapeleka, nakwambia utanitambua nikisikia umesema..............LOL
 
Afu ulijuaje anamtokea lara 1?
huyu mzee acha tu!
Uuuuuwiii, we binti mbona unataka kunitoa roho, unajifanta FBI eh....!

Nasema ukome kabisa kunifuata fuata, nasema koma kabisa, usinione nikisalimiana na mtu tayari ushayabeba.... Looo!!!!!!!!!
 
Nahsi kama nimekuona sehemu....ulikuwa umevaa nguo!..ryte?
BTW mwambie babaako kama anataka si atumie tu 'The boss guide ya kuwa na nyumba ndogo' kuliko kujustify visivyojustifaika.....

Unazeeka vibaya wewe baba. Unataka kujustify nini?

haya karibu urojo.
 
Disagree...
Babu na bibi yangu walifariki wakiwa na miaka 84 one wifebone husband.

Ila tukiangalia kwa miaka hii kuoa wwke wengi kuna possibility ya kufa mapema, magonjwa na mikikimikiki ya kutunza wake.
Hapa Mtambuzi....mmmmmm.
 
ahahahhahahhahaha kusa jua janja ya nyani!
kuuuumbeee ndo mana uliongeza yule mwingine siku ileeeeeeeeeeeeeeeeee!
:A S 100: hapo hapo subir
 
Back
Top Bottom