DELETED ACCOUNT
JF-Expert Member
- Mar 25, 2010
- 9,805
- 15,470
Unajua Yanga au kama ninavyopenda kuwaita Deportivo de Utopolo ni wapuuzi sana.
Baada ya kuona Simba inafanya vizuri kimataifa, kwenye ranking, uzinduzi na ushiriki wa AFL, fainali ya CAFCC, tuzo ya mashabiki bora na kuchangia pakubwa katika kuipandisha ligi ya Tanzania, wao wanaona kama wanasahaulika hivi au hawaimbwi kwa lolote, wanajaribu kupata vitu ambavyo watu wasiojielewa wakisaidiwa na chawa wao watasema "bila Yanga hili lisingetokea". Hizi ni propaganda.
CRDB waliingia mkataba na TFF katikati mwa msimu wa FA msimu uliopita. Kama ambavyo kawaida mikataba mingi ilivyo, mwaka wa kwanza pesa inakuwa ndogo na inaongezeka kwa jinsi miaka inavyokwenda. Kwa mfano, mwaka jana walitoa milioni 250 tu wakati msimu huu wametoa bilioni 1. Mkataba wa CRDB na TFF ulikuwa unaongezeka sana kwenye msimu huu wa 2024-25 na hata zawadi ya bingwa itakuwa kubwa zaidi. Zawadi inaweza kuwa hata hiyo milioni 200 waliyojipachikia katika deni la mwaka jana.
Kwa kujua hilo, Yanga wametengeneza hili zengwe ili mwisho wa siku zawadi ya mwaka huu ikitangazwa waonekane wao ndiyo waliipigania hadi zawadi ikaongezeka wakati ilikuwa katika mipango ya TFF.
Yanga wasingeweza kukacha kucheza fainali ya CRDB Cup dhidi ya Singida, kombe pekee msimu huu lililobaki ambalo wana uhakika wa kulichukua mpaka sasa.
Nasemaga siku zote, Yanga nawajua kama kiganja cha mikono yangu na hakuna janja janja yao ambayo naweza kushindwa kuifahamu.
Baada ya kuona Simba inafanya vizuri kimataifa, kwenye ranking, uzinduzi na ushiriki wa AFL, fainali ya CAFCC, tuzo ya mashabiki bora na kuchangia pakubwa katika kuipandisha ligi ya Tanzania, wao wanaona kama wanasahaulika hivi au hawaimbwi kwa lolote, wanajaribu kupata vitu ambavyo watu wasiojielewa wakisaidiwa na chawa wao watasema "bila Yanga hili lisingetokea". Hizi ni propaganda.
CRDB waliingia mkataba na TFF katikati mwa msimu wa FA msimu uliopita. Kama ambavyo kawaida mikataba mingi ilivyo, mwaka wa kwanza pesa inakuwa ndogo na inaongezeka kwa jinsi miaka inavyokwenda. Kwa mfano, mwaka jana walitoa milioni 250 tu wakati msimu huu wametoa bilioni 1. Mkataba wa CRDB na TFF ulikuwa unaongezeka sana kwenye msimu huu wa 2024-25 na hata zawadi ya bingwa itakuwa kubwa zaidi. Zawadi inaweza kuwa hata hiyo milioni 200 waliyojipachikia katika deni la mwaka jana.
Kwa kujua hilo, Yanga wametengeneza hili zengwe ili mwisho wa siku zawadi ya mwaka huu ikitangazwa waonekane wao ndiyo waliipigania hadi zawadi ikaongezeka wakati ilikuwa katika mipango ya TFF.
Yanga wasingeweza kukacha kucheza fainali ya CRDB Cup dhidi ya Singida, kombe pekee msimu huu lililobaki ambalo wana uhakika wa kulichukua mpaka sasa.
Nasemaga siku zote, Yanga nawajua kama kiganja cha mikono yangu na hakuna janja janja yao ambayo naweza kushindwa kuifahamu.