Yanga ifungiwe na FIFA kushiriki mashindano yo yote ya kimataifa kwa kuchangia CCM!

Yanga ifungiwe na FIFA kushiriki mashindano yo yote ya kimataifa kwa kuchangia CCM!

Ileje

JF-Expert Member
Joined
Dec 20, 2011
Posts
11,798
Reaction score
18,037
Mimi ni mpenzi wa Yanga lakini nimechukizwa sana kwa club hii kujihusisha na mambo ya siasa!

Kwamba kwa kuwa Yanga ilishiriki katika kupigania Uhuru wa Tanganyika siyo sababu ya kujihusisha na mambo ya siasa!

Eng. Herse anatumia Yanga kwa maslahi yake binafsi ya kisiasa, kwa hiyo natoa wito kwa wapenzi wote wa soka kupinga vikali kitendo hicho.

Huyu Msomali Eng. Herse anapaswa kufukuzwa katika uongozi. Aidha natoa wito kwa wapenzi wote wa soka kupiga kelele hadi Yanga ifungiwe na FIFA kushiriki mashindano yo yote ya kimataifa ili iwe fundisho kwa vilabu vingine duniani!
Screenshot_20250813-125139~2.png
 
Waandikie FIFA barua ambatanisha na ushahidi wa tuhuma zako kisha tafuta wakili msomi mahiri mithili ya Tundu Lissu au Kibatala asimamie shoo.
 
Waandikie FIFA barua ambatanisha na ushahidi wa tuhuma zako kisha tafuta wakili msomi mahiri mithili ya Tundu Lissu au Kibatala asimamie shoo.
Huyu Msomali Eng Hersi ameivuruga kabisa Yanga! Hapaswi kuendelea kuwa madarakani!
 
Mimi ni mpenzi wa Yanga lakini nimechukizwa sana kwa club hii kujihusisha na mambo ya siasa!

Kwamba kwa kuwa Yanga ilishiriki katika kupigania Uhuru wa Tanganyika siyo sababu ya kujihusisha na mambo ya siasa!

Eng. Herse anatumia Yanga kwa maslahi yake binafsi ya kisiasa, kwa hiyo natoa wito kwa wapenzi wote wa soka kupinga vikali kitendo hicho.

Huyu Msomali Eng. Herse anapaswa kufukuzwa katika uongozi. Aidha natoa wito kwa wapenzi wote wa soka kupiga kelele hadi Yanga ifungiwe na FIFA kushiriki mashindano yo yote ya kimataifa ili iwe fundisho kwa vilabu vingine duniani!
View attachment 3440009

Kwani hatuwezi kuhamasishana kuwafungia hawa sisi wenyewe kwa kuachana nao kivyetu vyetu? Kwani ni lazima kuwashabikia wao?
 
Mimi ni mpenzi wa Yanga lakini nimechukizwa sana kwa club hii kujihusisha na mambo ya siasa!

Kwamba kwa kuwa Yanga ilishiriki katika kupigania Uhuru wa Tanganyika siyo sababu ya kujihusisha na mambo ya siasa!

Eng. Herse anatumia Yanga kwa maslahi yake binafsi ya kisiasa, kwa hiyo natoa wito kwa wapenzi wote wa soka kupinga vikali kitendo hicho.

Huyu Msomali Eng. Herse anapaswa kufukuzwa katika uongozi. Aidha natoa wito kwa wapenzi wote wa soka kupiga kelele hadi Yanga ifungiwe na FIFA kushiriki mashindano yo yote ya kimataifa ili iwe fundisho kwa vilabu vingine duniani!
View attachment 3440009
pole yanga na ccm wana symbiotic relationship,ukuona vipi we jiondoe tu yanga
 
Sio huyo peke yake, hata wafanyabiashara nao hawaruhusiwi kuchangia vyama vya siasa...maana wataanza kujihusishq na pembe za ndovu na madawa ya kulevya na kulipa Kodi wataanza kusuasua na uongozi usiwafanye chochote maana watakuwa wanakumbuka fadhila tu...huko kwenye mpira ndio balaa...kwenye upendeleo na kwenye maamuzi
 
Kimsingi viongozi wa Yanga wasifikiri mashabiki/wanachama wote wa Yanga ni ccm. Wakumbuke hiyo timu inapata mafanikio siyo kwa sababu tu ya hizo pesa zao za ufisadi! Ila ni kwa sababu ina mashabiki wengi, na wasio fungamana na ccm, rangi ya mtu, kabila lake, dini yake, nk.
 
Kwani hatuwezi kuhamasishana kuwafungia hawa sisi wenyewe kwa kuachana nao kivyetu vyetu? Kwani ni lazima kuwashabikia wao?
Kanuni zipo zifuatwe Yanga wafungiwe misimu kadha na sisi mashabiki tutaunga mkono!
 
Mimi ni mwanachama hai wa CHADEMA,ila naipenda YANGA haijalishi wameichangia CCM. amani,umoja,upendo na mshikamano huletwa kwa mambo kama haya. hongera yanga kwa kitendo hiki cha kiungwana,hata nyie simba ichangieni CCM. VYAMA visitugawe watanzania.
 
Kanuni zipo zifuatwe Yanga wafungiwe misimu kadha na sisi mashabiki tutaunga mkono!

Kwa hiyo ninyi ni kuunga mkono tu, Wala siyo kulianzisha? Ndiyo maana wamejawa kibri!
 
Najaribu kuwaza hivi wanasheria wa yanga hawakuliona hili kuwa haliluhusiwi katika soka au ni kutaka kuiingiza club katika mgogoro na fifa na ulimwengu wa soka bila sababu. "Mgema akisifiwa tembo hulitia maji". Haya tumeshayatilinganya tusubiri yajayo. Hatujifunzi tu yaliyotokea CHAN. Yanga mmetukosea sana mashabiki wenu. Simba unadhani ni mjinga kutokujihusisha moja kwa moja anajua miongozo inataka nini katika mpira. Kwa hili eng umeukosea sana mpira.
 
Hoja ni kuwa wamekiuka kanuni za FIFA hivyo wanastahili adhabu kali bila huruma!
nomeona kanuni zinapitishwa sasa siwezi kusema kama ni za jweli au laa,pili hizo kanuni hazina locus standi
 
Kwa hiyo ninyi ni kuunga mkono tu, Wala siyo kulianzisha? Ndiyo maana wamejawa kibri!
Kwa nini unaamini katika vurugu badala ya majadiliano?
 
Back
Top Bottom