Mheshimiwa Rais wa Serikali ya Jamhuri wa muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi..,Chama tawala na Chama Imara Tanzania amaliza hotuba yake kwa kuwaambia kuwa anaamini kuwa "RAIS WA TANZANIA MWAKA 2025 YUPO KWENYE UKUMBI HUU LEO HII"
Na hivi sasa anaelekea nje ya Ukumbi ambapo atapiga picha ya pamoja na wageni waalikwa kwa ajili ya ukumbusho na kisha ataendelea na majukumu yake mengine ya kuijenga na kiimarisha Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Inashangaza sana. Hata juzi kwenye hotuba yake wakati akifunga uchaguzi wa UWT alisema hilohilo, kuwa lengo la CCM ni kushinda. Inashangaza kuwa hajaongelea wajibu wa chama tawala kuhakikisha kinaunda serikali ambayo iyawatumikia wananchi. Au labda kwa sababu ni uchaguzi wa chama ndio maana amezungumzia hayo na kuacha jukumu kubwa wananchi wanalolitarajiaKushinda tu?.....Kushinda kivipi?......Na vipi kuwahudumia wananchi? Ndio maana alitoaahadi 100 za uwongo
mngejuahuo mkutano pekee una wajumbe wapatao 1300.achilia mbali wale waliopo ngazi za chini ambao wanaishia kwenye matawi kata na mashina.wewe peke ako ndio uko huko lakini vijana wenye akili timamu wapo ccm
Well saidHuo mnada wao haujaisha tu? Wasiwatafutie watu lawama bure,hakuna kijana yeyote mwenye akili atakayeshawishika kujiunga na hicho chama.
Hapana, uchaguzi ulishaanza na sasa unakaribia kumalizikaWanachaguana usiku nini??
Huo mnada wao haujaisha tu? Wasiwatafutie watu lawama bure,hakuna kijana yeyote mwenye akili atakayeshawishika kujiunga na hicho chama.
Well saidKwa style hii naona upinzani utapwaya baada ya uchaguzi mkuu 2015.Tunahitaji CCM kiwe chama kizuri kutukosoa baada ya uchaguzi mkuu lakini naona matumaini yanafutika.Labda CUF ijiimarishe au wafanye allince ya upinzani na CCM baada ya uchaguzi mkuu ili waunde kambi imara
Mheshimiwa Rais atoa hotuba kali kwa vijana ambayo inalenga kuwajenga na kuwataka wafanye tathmini ya kutosha kwa wagombea wa nafasi mbalimbali za uongozi wa ngazi ya Taifa ya Jumuiya hiyo ya Vijana.
Alianza kwa kuwakumbusha Ibara ya 5 ya katiba ya chama cha mapinduzi ambayo inaeleza MALENGO NA MADHUMUNI ya CCM.,ambapo imeelezwa kwenye ibara hiyo kuwa madhumuni ya CCM ni "kushinda katika uchaguzi wa serikali kuu na Mitaa"
Lakini pia akaeleza kuwa CCM kinategemea Jumuiya yake hii kufanya kazi ya siasa miongoni mwa vijana wa TANZANIA na kuwashawishi wakubali kuwa wanachama na wapenzi wa CCM. Akasisitiza kuwa matumaini makubwa ya msingi kuliko yote ya Chama Cha Mapinduzi ni kuona jumuiya yake hii inakuwa MKOMBOZI wa vijana.
Akawataka wahakikishe kuwa wanapata Mwenyekiti, Makamu mwenyekiti na viongozi wengine ambao wataongoza vyema,watakaoongoza juhudi za kuendeleza, kutetea na kulinda maslahi ya CCM. Viongozi wanaoijua na kuipenda jumuiya ya Vijana.
Na pia akawataka baada ya uchaguzi wajipange kutimiza wajibu wao kwa jumuiya yao na Chama kwa Ujumla..,
HOTUBA INAENDELEA....