Yanayojiri bungeni: Tarehe 20 Machi, 2014

Yanayojiri bungeni: Tarehe 20 Machi, 2014

Yaani bunge letu lingekuwa linaendeshwa kwa Kiingereza kama Kenya ,mijadala ingekuwa inachukua muda mfupi sana,mambo ya ''Muongozo wa spika n.k ''yangepungua ama kuisha kabisa,wachangiajia wangekuwa wachache sana na utoro Bungeni ungeongezeka.

Hahahahahahahahahaaaaa!
Sasa mkuu hapo tungepata katiba gani?
 
Ila leo naona wabunge walio wengi hasa wa mlengo ule wa maji ya bendera wanapiga soga tu hasa huyu Mkenya anapomwaga nondo zake.

Ila sijaelewa kazungumzia nini specifically ambacho tunaweza kujifunza kutoka kwao, kwa mfano kura ya Wazi au Siri na mambo mengine!
 
Nimegundua, ile lugha ya kiswanglish inayotumika bungeni huwa ni geresha tu, wamekuja wanaotema umombo wabunge wanatoka kapa-hasa Mwigulu yaani ndo haelewi kinachozungumziwa kabisa...! Anawaza CDM tu!
Japo sipendi ushabiki wa kisiasa naa mini mwigulu yuko vzr, labda useme Sendeka, Lukuvi na wasira hao na shaka nao
 
Hizi kamera za Star TV zingezimwa tu maana zinawaumbua walio wengi kwa kua naona wanapiga soga wakati hotuba inaendelea
 
kwa hili nadhani walikurupuka kimtindo. Kuanza kujadili kama atumike mtafsiri au la wakati zoezi linaendelea inaondoa umakini wa kile kinachoongelewa. Ni muhimu awepo mfasiri ili hata wananchi wanaofuatilia wapate kuelewa kinachoongelewa.
 
Wanajamvi.
Nimefanikiwa kushuhudia asilimia kubwa ya Wabunge wa Bunge la Katiba wakilalamika kuhusu matumizi ya lugha ya kiingereza kwenye uwasilishaji wa Mh. Amos Wacko.

Baada ya kuona ombi lao halikubaliwi kwa kigezo cha kuleta mtiririko mzuri wa kile anachokitoa Mh. Amos Wacko.
Wabunge wameingia mitini kiaina kwa kusinzia ama kutokujitokeza kupeleka majina ya kuomba kuuliza swali. Hadi muda huu ni wabunge kumi tu kati ya mia sita ndo wameomba kuuliza maswali au kuchangia.

Pia kimetolewa kisingizio cha kwa kuwa mjadala unaangaliwa na kusikilizwa na wananchi kupitia vyombo vya habari inabidi tafasiri itumike ili watu wengi waelewe.

Swali langu ni: Mbona kila siku muda wa saa mbili asubuhi TBC1 kituo cha Taifa kinaungana na CCTV na wanatangaza kwa kiingereza? Au matangazo hayo hayatuhusu wabongo?

Pia: Kwani wajumbe walikuwa hawajui kama Mh. Amos Wacko atakuja kushusha nondo kwa lugha ambayo siyo yao?
Mwenye uelewa anisaidie.
 
Macho yanakodolewa kweli huenda somo linaeleweka vizuri.

Kukodoa macho si kuelewa Mkuu! Hao wanashangaa tu!
Na usikute robo ya wajumbe ndio tu wanaoelewa sawa sawa! Teh teh teh!
Chezea elimu ya Tz weye!
 
naona kuna mkenya anaongea kizungu chenye lafudhi ya kabila la waluhya.
 
Nimefurahi kusikia kwamba kutoka kwa Mwanasheria Mstaafu wa Kenya, Amos Wakko kwamba Kenya nafasi nyingi mfano: Katibu Mkuu, Mwanasheria Mkuu, Jaji Mkuu, Wakuu wa Taasisi zote za Umma, wanaomba ajira kama wafanyakazi wengine wowote wale. Na Interview kwa nafasi muhimu mfano Jaji Mkuu hufanywa kwenye TV Live. Hii ni jambo muhimu sana, tunahitaji kuwa nalo maana rushwa na wizi wa rasilimali utapungua katika Ofisi za Umma. Kila mtu yuko huru kufanya kazi kwa utaalamu bila kuogopa aliyemteua...
 
Ona wabunge wetu walivyo wanyonge Leo.no kuzomea wala kuomba mwongozo.shkamoo mzungu
 
naona the likes of maji marefu wameamka baada ya mtafsiri kuanza kutoa tafsiri ya maelezo ya mgeni toka kenya.lol
 
Aya mamemba yanayochangia humu yanareta kuzuga tu! Wengine hatupo kwa tv wala radio, tunazama hapa tujue nini kinajadiliwa ninyi mmeng'ang'ana wajumbe hawajui kingreza!
Ninyi mnaojua kingreza tuambieni yanayosemwa huko!
 
Kwa mara ya kwanza nimesikia meza kugongwa muda huu baada ya mkarimani kuleta kwa kiswahili, kumbe wajumbe walikuwa hawamuelewi Mh. Wacko.
 
....profesa maji marefu (Ngonyani) na yule mwakilishi wa wachawi (Kingunge) siwaoni hapo bungeni...
 
Back
Top Bottom