Yanayojiri bungeni: Tarehe 20 Machi, 2014

Yanayojiri bungeni: Tarehe 20 Machi, 2014

Da nazani sasa tunafika mwisho wa dunia nashangaaa hao wajumbe waliochaguliwa kutoka taasisi na vyama wasiojua kiingereza wanafanya nini hapo ... kweli mwisho wa dunia utaanzia dodoma kwa nyie wajumbe msiojua mnachofanya kazi kula kodi za watanzania ...mmechaguliwa kwa ajilai ya watanzania mjue hilo
 
Kwani wakenya walijifunza kwa nani? Mi naona ilikuwa bora asiitwe huyo jamaa badala yake tungeangalia tu kwa uhalisia mahitaji na maoni ya watz yanataka nn na kuyafanyia kazi. Usije kushangaa huyo jamaa kulipa si chini ya tsh. 50,000,000 kwa hayo madudu tu

Kenya walileta baadhi ya watalamu kutoka ulaya. Fuatilia acha kulalamika.
 
Macho yanakodolewa kweli huenda somo linaeleweka vizuri.
 
Hv hawajui kma bunge hlo limeshirikisha watu wa kada mbalimbali ambao miongoni mwao hawajui kithungu.
Waache ubabaishaji...endelea kutafsiriii
 
Nimegundua, ile lugha ya kiswanglish inayotumika bungeni huwa ni geresha tu, wamekuja wanaotema umombo wabunge wanatoka kapa-hasa Mwigulu yaani ndo haelewi kinachozungumziwa kabisa...! Anawaza CDM tu!
 
lugha si tatizo kwa watz kwani wanajua lugha mbalimbali za kiafrika iwe kibena, kizaramo, kimakua, kindengereko
na lugha ya kimakonde kutoka msumbiji wanakijua sasa unafikiri lugha gani wasioijua ya AFRIKA?

mwacheni amosi aongee kingereza-kikamba wala msitafsiri kwani watz wanakijua nacho.
 
Da nazani sasa tunafika mwisho wa dunia nashangaaa hao wajumbe waliochaguliwa kutoka taasisi na vyama wasiojua kiingereza wanafanya nini hapo ... kweli mwisho wa dunia utaanzia dodoma kwa nyie wajumbe msiojua mnachofanya kazi kula kodi za watanzania ...mmechaguliwa kwa ajilai ya watanzania mjue hilo

Kiingereza ndio utumbo gani? Acha kuwa mfuasi wa tamaduni za watu wewe.
 
Kiingereza ndio utumbo gani? Acha kuwa mfuasi wa tamaduni za watu wewe.

Kizungu ndio lugha ya dunia acha kujipa moyo, na umasikini huu wote tuna jeuri ya kusema kiingereza lugha ya 'tamaduni za watu'?


Sent from Mchina
 
Nimemuona Bw Lusinde kaamua kuchapa tuu usingizi maana hakuna hata moja linaloingia huku Mh Majimarefu yeye anakata kucha anaona bora huyu jamaa amalize na kuondoka. Hii ni fimbo ya pili kwa wabunge wengi wa CCM.


Sent from my iPad using JamiiForums
 
Ni kama kuna jamaa anawatafsiria mkuu. "Nje ya Tanzania, Mtanzania ni BUBU"

Zile mbwembwe za kina Lusinde huko zinakuwa kama zimepigwa sindano ya ganzi. Wao wamezoea ndiyooooo!


Sent from my iPad using JamiiForums
 
Wanajamvi.

Nimefanikiwa kushuhudia asilimia kubwa ya Wabunge wa Bunge la Katiba wakilalamika kuhusu matumizi ya lugha ya kiingereza kwenye uwasilishaji wa Mh. Amos Wacko.

Baada ya kuona ombi lao halikubaliwi kwa kigezo cha kuleta mtiririko mzuri wa kile anachokitoa Mh. Amos Wacko.
Wabunge wameingia mitini kiaina kwa kusinzia ama kutokujitokeza kupeleka majina ya kuomba kuuliza swali. Hadi muda huu ni wabunge kumi tu kati ya mia sita ndo wameomba kuuliza maswali au kuchangia.

Pia kimetolewa kisingizio cha kwa kuwa mjadala unaangaliwa na kusikilizwa na wananchi kupitia vyombo vya habari inabidi tafasiri itumike ili watu wengi waelewe.

Swali langu ni: Mbona kila siku muda wa saa mbili asubuhi TBC1 kituo cha Taifa kinaungana na CCTV na wanatangaza kwa kiingereza? Au matangazo hayo hayatuhusu wabongo?
Pia: Kwani wajumbe walikuwa hawajui kama Mh. Amos Wacko atakuja kushusha nondo kwa lugha ambayo siyo yao?

Mwenye uelewa anisaidie.
 
jaman acheni kushabikia kinachofanywa hapo ni sahihi kabisa.maana bunge linatazamwa na watu wengi wanaojua kimombo na wasiojua. vp kuhusu babu yako ambaye haelewi lugha.tatizo mmezoea kuponda
 
Hivi kweli inakuingia kichwani bunge la tanzania kutumia lugha ya kigeni kingereza na wakati wananchi wengi hawana ufahamu wa kujua lugha hiyo.Leo katika bunge letu la tanzania kuna semina ya katiba lakini semina hiyo inatolewa kwa lugha ya kiengezea,hii semina je inawahusu wasomi peke au wananchi?
 
Wakuu,
Naangalia Bunge la Katiba Hapa.
Kuna jamaa anatoa Semina kwa wabunge wetu, lakini jamaa anatoa Semina kwa Ung'eng'e.
My Take.
Sidhani kama hili somo akina Ole Sendeka linawaingia kwa Maana ya5 Kuelewa
 
Ila leo naona wabunge walio wengi hasa wa mlengo ule wa maji ya bendera wanapiga soga tu hasa huyu Mkenya anapomwaga nondo zake.
 
Back
Top Bottom